gossip

STORI NZIMA YA KIDOA KUMKIMBIA MAMA YAKE NA KWENDA KUISHI KWA MWANAUME WAKE



MUUZA nyago anayefanya poa Bongo, Asha Salum ‘Kidoa’ anadaiwa kumkimbia mama yake aliyekuwa akiishi naye maeneo ya Kinondoni na kwenda kuishi na mwanaume (jina linahifadhiwa kwa sasa) maeneo ya Tabata jijini Dar.

Chanzo makini kimetutonya kuwa, tangu mwanadada huyo awe staa, amekuwa si mtu wa kukaa na mama yake badala yake amekuwa kiruka njia, usiku anaenda klabu, mara kasafiri kwenda nje lakini siku zote analala na kuamkia kwa mwanaume huyo.

“Unajua Kidoa siku hizi kamkimbia kabisa mama yake, muda mwingi yupo kule Tabata kwa bwana wake wakati bi mkubwa alishazoea kuishi naye,” kilidai chanzo hicho kwa bongohotz.com

Baada ya kuzipata nyeti hizo, Bongohotz.com ilimtafuta Kidoa ambapo alikiri kuwepo Tabata kwa ‘mtu’ wake akieleza kuwa, bi mkubwa huwa anakwenda kumuona mara mojamoja.
Post a Comment

Post a Comment