BIKIRA

BIKIRA YANGU - 5 - Swahili Viuhapa

featured image


viuhapa


Chombezo : Bikira Yangu
Sehemu Ya Tano (5)

ILIPOISHIA
“Noo!”
Catherine alishtuka kutoka usingizini akiwa ndani ya ndege hakuelewa ni wakati gani usingizi ulimpitia na kulala fofofo! ndoto aliyokua akiota ilimshtua sana ni
CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
kweli alivyogeuka kuangalia siti za nyuma Mwarabu hakuwa bado amerudi kwenye siti yake. Alifungua mkanda wake wa kiti na kuanza kutembea taratibu

mpaka chooni!…

SONGA NAYO.

Ndani ya moyo wake bado alimuwekea mashaka mwarabu aliyeingia ndani ya ndege ni kweli alimuona mahali, lakini hakuweza kukumbuka ni wapi na ni lini,

alichotakiwa kufanya ni kumuangalia kila hatua anayopiga.
Ndoto aliyotoka kuiota kuwa ndege imelipuka baada ya kutekwa nyara kisha bomu kutegwa, ndiyo iliyomfaya azidi kuingiwa na hofu sana dhidi ya mtu

huyo,hapo ndipo alipoamua kusimama na kutembea mpaka msalani kumfuatilia, macho yao yaligongana!.
“Asalam aelekuy”
Alisalimia Mwarabu huyo alivyoonana na Catherine baada ya kutoka msalani.
“samahani sijui tunafahamiana?”
“Hapana wenda umenifananisha”
“okay”
Bado Catherine alizidi kumuwekea mashaka mwanaume huyo mpaka ndege inakanyaga Ardhi ya Kigali nchini Rwanda na kubadilishiwa ndege nyingine.
Walivyopanda ndege nyingine hakumuona tena na kushusha pumzi ndefu. Baada ya masaa matatu kipaza sauti kilisikika sauti ikitokea pembeni mwa spika ndogo

kutoka kwa msichana mrembo kikiwataka abiria wote wafunge mikanda yao kwani ndege inaenda kutua Tanzania Dar es salaam, uwanja wa Mwalimu Nyerere,
Catherine alitabasamu sana kusikia habari izo, abiria wote walifunga mikanda kisha kichwa cha ndege kwa mbele kuinama kidogo baada ya kutoa matairi yake,

ilivyotua ilitingishika kidogo kisha kukaa sawa ikiwa katika mwendo wa kasi sana kisha baadaye taratibu ikipunguza mwendo kasi na kusimama na ndo hapo

baadhi ya abiria waliofika kuanza kutoa mizigo yao sehemu ya juu maalumu.
Catherine ndiye aliyekua wa kwanza kutoka mlangoni akifuatiwa na Kway pamoja na mke wake Julia kushoto kwake, wote walikua wenye nyuso zenye furaha

sana. Walitembea mpaka kwenye vidirisha maalumu na kugonga passpot zao mihuri immigration kisha kupita mpaka sehemu ya mizigo, Kway alitembea mpaka

ndani ya chumba maalumu alipoacha bastola yake kipindi anaondoka kisha baada ya kukagua kama kila kitu kipo sawa aliiweka kiunoni na kuifunika na shati ili
CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
isionekane. Yalivyokamilika hayo yote walianza kutoka nje wakiwa na abiria wenzao!.
“Daaaaa…diiiiii!”
Kelele zilisikika kutoka kwa Natu akitoka mikononi mwa Hussein Molito kisha kumkimbilia Baba yake na kumrukia kwa nguvu, furaha ilirudi tena katika

familia hiyo iliyokua imetengana kwa kipindi kirefu sana, Catherine alivyopiga jicho pembeni alimuona Enock akiwa na MAMA yake mzazi wakiwa wenye

nyuso zenye furaha wote walirukiana na kukombatiana. Kila mtu alikua na furaha sana ndani ya moyo wake baada ya kukutana tena.
“Catherine mpenzi wangu pole na matatizo”
“Ahsante mpenzi”
Baada ya kuachiana na Catherine alimsogelea Kway kisha kukombatiana, huku wakipigana pigana migongoni, ni muda mchache tu walifahamiana lakini kwa

matatizo waliyopitia wakiwa nchini Uganda ilibidi wajipongeze sababu waliyashinda.
“sasa sijui nikuiteje, Mkwe au?”
Aliuliza Enock huku akicheka.
“vyovyote vile sawa Enock”
Jicho la kway lilitua kwa mtoto aliyekua ame mbeba Sabrina ambaye bila kuuliza mtu yoyote Yule usingebisha ukiambiwa kuwa ni mtoto wa Kway sababu

walifanana kwa kila kitu, aligeuza shingo yake na kumtizama Mke wake Julia aliyekua amembeba Natu wakiwa wenye furaha kisha kushusha pumzi!.
“Sabrina”
Aliita Kway kwa ujasiri ilikua ni lazima waweke mambo sawa siku hiyo hiyo kabla haijapita.
“Abee”
“naomba nimuone Mtoto”
Hakukua na mtu yoyote mwenye kipingamizi cha aina yoyote ile kila mtu alikua kimnya, hata kwa Julia pia, alionyesha furaha pia na kumchukua Mtoto huyo

Christopher aliyekua teyari keshaanza kuota Meno alikua mweupe Mzuri na mwenye afya.Kwa pamoja walikombatiana wakiwa wenye furaha sana.
“Sasa Baba Mkwe, kabla ya kufika kwako,najua umechoka naomba tutafute sehemu nzuri tufurahi sote kwa pamoja”
Alishauri Enock na wote kumuunga Mkono. Kway na familia yake waliingia kwenye gari ya Hussein Molito huku Catherine pamoja na Mama yake kuingia

Kwenye gari ya Enock na wote kuanza kuongozana Marcedez Benz mbele nyuma Landcruiser vx.
Safari yao ilikomea Kwenye Bar ya Mtoto wa BECKER iliyokua Kimara Suka.
Tajiri aliyesifika kwa kumiliki vituo mbali mbali vya redio na t,v ndani na nje ya nchi, japo alikua kijana mdogo lakini alikuwa mwenye mafanikio kutokana na

juhudi zake za kazi, hapo ndipo walipojenga urafiki na Enock Mwasha siku chache wakipeana ushauri kuhusiana na Maisha, habari zilizo mchanganya Mtoto wa

BECKER ni kitendo cha Enock kuunguliwa kwa nyumba yake kubwa, aliguswa sana na kumuhaidi kuwa atakuwa naye bega kwa bega mpaka mambo yatakapo

kuwa sawa!.
Siku hiyo ilikuwa ni furaha sana kwao walikunywa na kula walivyoridhika kila mtu aliwasha gari na kuondoka sababu usiku ulikua tayari umeingia.
**
“Enock mpenzi pole na matatizo uliyopata”
Alisema Naomi siku hiyo akiwa ofisini kwa Enock baada ya kuzuga kuwa amefika kutokea mkoani Mwanza, ukweli ni kwamba hakua safarini,ndani ya moyo

wake alikua na visasi vikichanganyika na hasira.
“nilisikia bado Baba yako anakuwinda?”
“ndio Naomi, hapa nashindwa cha kufanya sijui nifanye nini?”
“kwani yuko wapi?”
“yupo kisiwani unguja navyosikia”
“ulishaenda polisi kutoa mashtaka?”
“hapa navyokwambia ndiyo nimetoka kituoni”
“wamesemaje?”
“ndio wameenda huko wiki iliyopita kumkamata”
“sawa..!sasa akishakamatwa itakuaje?”
“Nitaacha sheria ifate mkondo wake”
“vipi kuhusu swala la ndoa yetu?”
Hilo ndilo swali lililomfanya Enock asitishe kubonyeza bonyeza kompyuta iliyokuwa mbele mezani kwake na kumkazia Macho Naomi.
“Lakini Naomi, huoni bado nina matatizo,wacha tulimalize hili la kwanza mambo ya ndoa yatafuata”
“usijifanye mjanja sawa, usiniletee longolongo na usanii, na uache uwongo najua kila kitu kinachoendelea kuhusu wewe na kahaba wako Catherine,sasa basi

utaozea jela hapa napokwambia namimi pia nimetoka polisi kutoa maelezo ya kifo cha Heather”
“Unasema?”
“Ndo ivyo, unatafutwa na polisi, wewe si ulimwaga ugali mimi namwaga mboga hapaliki”
Aliongea Naomi akipayuka akimaanisha kwa aliyokuwa anaongea tena akiwa mwenye hasira huku akiwa amesimama ameukunja uso wake.
Na ni kweli haikuchukua hata dakika thelathini Askari walifika ofisi za Nissan wakimuhitaji Enock, hawakumpa hata nafasi ya kuongea na kujitetea, hapo hapo

walimpiga pingu kwa nyuma baada ya kauli iliyotoka kwa Kamanda Amata mkuu wa kituo kikubwa cha Oysterbay.
Kila mtu alishindwa kuelewa ni nini kimetokea, wafanya kazi wake walizidi kunong’ona wasielewe ni kitu gani kilifanya mpaka bosi wao afungwe pingu kwa

nyuma kama muhalifu au jambazi sugu.
Hakukua na masihala hata kidogo dhidi ya polisi hawa, walimsukuma mpaka nyuma ya difenda kisha kuondoka naye mpaka kituo cha polisi Oysterbay, maelezo
CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
aliyotoa Naomi pamoja na ushahidi wote ulitosha kabisa kufanya kesi ya Enock izidi kupamba moto na kupandishwa ngazi za juu na kisha kufunguliwa kesi ya

mauaji kumaanisha kuwa anaenda kufungwa kifungo cha Maisha gerezani.
Ndugu wa Heather tayari walipata taarifa hizo na kuzidi kumlaani Enock kwa kitendo cha kumuwekea ndugu yao Heather sumu kali ya panya akiwa wodi ya

vichaa na kufa, na ndiyo ivyo Naomi alivyowaambia ndugu hao waliofunga safari kutoka Morogoro Matombo, mpaka Dar es salaam ili kusikiliza kesi hiyo

itakayo anza baada ya wiki tatu.

Jiji la Dar es salaam lilikua katika hali ya utulivu na ukimnya wa hali ya juu kila mtu alitega sikio lake,kesi ya Enock David Mwasha iliunguruma sana, historia

yake fupi iliyosimuliwa na kila mtu ilifanya ijaze mamia ya watu ndani ya mahakama ya kisutu, kila mtu alitega sikio ili kusikia kitakacho zungumzwa na

mwanaume huyu aliyekua mtoto wa tajiri mkubwa jijini Dar es salaam aliyefahamika kisha kupata kashfa ya ujambazi na uharamia vile vile.
Wengine walichukizwa sana kwa kitendo chake cha kumuuwa mke wake Heather aliyekuwa mwenda wazimu katika wodi ya vichaa Muhimbili ili awe na

mwanamke mwingine na ndiyo ivyo alivyotangaza Naomi kwa kila mtu hata katika vyombo vya habari mbali mbali vya redio, magazeti mpaka t,v.
Wanawake wengi walimchukia na kutamani hata anyongwe, walimuona Enock ni mnyama sana hana roho ya kibinadamu na hastaili kuishi Duniani.
Mnamo tarehe nane mwezi wa tisa ndiyo siku ya kesi yake kusomwa kwa mara ya kwanza hapo kisutu akisomewa mashtaka ya mauaji, Umati wa watu ulizidi

kufurika ili kusikia hukumu ya Enock Mwasha, wengi walitaka ahukumiwe kifungo cha maisha, ila wachache ndiyo walioamini kuwa kijana huyu Mdogo hana

hatia, licha ya hayo walisubiri sheria ifate mkondo wake sababu siku zote ukweli hujitenga na uwongo.
Catherine muda wote alikua akilia machozi haamini kile anachokiona na kukisikia hata yeye alishajua kuwa Enock mchumba wake hawezi kuwa huru tena ni

kifungo cha maisha ndiko anachostaili!.
Kway na Mtoto wa Becker walifika mapema siku hiyo asubuhi ya saa mbili wakiwa viti vya mbele upande wa watu wachache ambao waliamini kuwa Enock

hakuwa na hatia ya aina yoyote ile.
Ukimya ulitawala baada ya majaji kuingia, kesi hiyo iliongozwa na jaji Patrick NDILITO aliyesifika kwa roho mbaya, kila aliyemuona alishtuka hakuonesha hali

yoyote ya kucheka, nyuma yake walifuata mawakili wake waliovalia majoho meusi wakiwa na vitabu mikononi mwao tayari kwa kusikiliza kesi hiyo iliyokua

ngumu, hasa walipomuona wakili Nolan Mkwiche aliyekuwa upande wa Enock amevalia suti nyeusi,
walimfahamu sana wakili huyo aliyesomea kazi yake ya sheria nje ya nchi, alipata umaarufu sana kutokana na kufanya kazi yake vizuri, hakuwahi kushindwa kesi

hata siku moja na ndo hapo Anderson Peter alipomshauri Enock wamtafute kwa gharama yoyote ile na kufanikiwa kumpata.
Upande wa mashtaka waliruhusiwa kupanda, Naomi ndiye wa kwanza kupanda kizimbani na kuweka mkono wake juu ya Biblia kama kiapo asiongee uwongo.
“Kwa majina naitwa Naomi Cosmas Masunga, mnamo tarehe tatu mwezi wa pili mwaka huu ndipo nilianza kujuana na Enock,tukawa wapenzi lakini hakuwahi

kuniambia kuwa ana mke ili mradi anipate, ni kweli nilimpenda na alitaka kunioa, nilivyofanya uchunguzi nikagundua kuwa ana mke nilivyo muuliza akadai

kuwa nimuachie yeye kwa kuwa ananipenda sana na hayupo tayari kuniacha,ni kweli sikua na roho mbaya yoyote nikawa naenda hospitali kumuona marehemu

Heather na ndiye yeye aliniambia niwe nafanya ivyo ili nizoeleke, hapo mwanzo sikujua ana maana gani mpaka siku aliponipa chupa ya maji na kuniambia kuwa

nikampe Heather wodi ya vichaa,nilivyompa tu nikaona Heather anatoa mapovu na umauti kumkuta hapo hapo nikagundua yale maji yana sumu ya panya,

nilipomuuliza akasema ni kweli nimfichie hiyo siri nikafanya ivyo, ila baadaye nikaona siwezi kukaa na kitu hiko moyoni!”
Kila aliloongea Naomi kizimbani kiliandikwa vizuri, wakili Nolan Mkwiche alimsikiliza kwa umakini sana na kukariri yote anayosema.

Baadaye alisimamishwa Enock akiwa na pingu mpaka kizimabani, alikuwa amekonda sana ana vipelevipele usoni alitia huruma, Catherine alilia tena macho yao

yalivyogongana,
hata yeye alionekana kushangazwa na umati wa watu.
Alipewa Biblia na yeye kuweka mkono wake kama alivyofanya Naomi kisha kufuatisha maneno aliyoambiwa aseme!.
“Kwa majina naitwa Enock David Mwasha mbele ya mahakama tukufu napenda kukanusha haya yote aliyoongea Naomi”
Hapo ndipo Enock alipoanza kuongea ukweli jinsi alivyompata Naomi na kudhani kuwa Catherine amefariki kwenye vita vya kongo!.
“Nilimpenda sana Naomi,kwa kujua kuwa Mpenzi wangu Catherine alifariki dunia,yeye ndiye aliyekua akinisisitiza kuhusu ndoa tutafunga lini,kabla ya hapo

nilimwambia nina Mke ila yupo wodi ya vichaa na nina mpenda, sikuwahi kumwambia aweke sumu kwenye maji kama anavyodai,kifo cha Marehemu mke
CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
wangu kilinishtua baada ya kuambiwa kuwa amekufa kwa sumu ya panya iliyokuwa kwenye chupa ya maji nilivyomuuliza aliniambia kuwa alinunua sumu ya

panya kwa ajili ya kuwatega panya na ndo ivyo alivyowaambia polisi pindi walivyomuhoji”
Maneno aliyopewa na Wakili Nolan Mkwiche kuwa akatae na kukanusha kuhusu sumu ya panya ili kesi isiwe ngumu na ndivyo alivyofanya,
ilibidi akatae kata kata kuwa hakuwa anaelewa mipango yoyote ile juu ya sumu hiyo iliyomuuwa Marehemu Heather, baada ya kuongea hayo alipanda wakili wa

upande wa kumtetea Naomi na ndugu zake Heather ambao walionyesha kumkandamiza Enock!.
“Bwana Enock,ulisema kuwa ulimpenda sana Marehemu mke wako,katika historia ya hapo nyuma inaonesha kuwa mlishawahi kuwa na ugomvi mkubwa

ukimsingizia kuwa alienda kwa waganga kukuwekea dawa, ukampiga wakati alikua na mimba, huoni hiyo inatufaya tuzidi kukuwekea mashaka kuwa wewe

ndiye ulifanya hayo mauaji?”
Wakili Faaris aliuliza kwa kujiamini sana huku akishika shika tai yake iliyokua kooni akitembea tembea.
“Ndio sikatai tulikuwa na ugomvi wa kifamilia,lakini baada ya hapo tulielewana vizuri baada ya kurudi kutoka nchini Brazil nikakuta yupo wodi ya vichaa,

sikuelewa ni kitu gani kilimpata”
“Najua kuwa unajitetea ili umkandamize mteja wangu ambaye hana hatia yoyote ile,swali lingine ulitambua kabisa kuwa una mke, kama ulivyosema mwenyewe

katika maelezo yako, ni kipi kilikufanya uwende kwa Naomi, kama mkristo navyojua mimi ni kuwa kitakacho watenganisha wanandoa ni kifo peke

yake,unaiambia nini mahakama tukufu juu ya hilo?”
Ni kweli swali hilo lilionekana kuichanganya akili ya Enock na kushindwa ni kitu gani akijibu, alivyomuangalia wakili wake alimtingishia kichwa kuwa asijibu

kitu chochote kile!.
“Ni hayo tu muheshimiwa hakimu”
Wakili Faaris alikaa kwenye kiti kisha upande wa utetezi alisimama Wakili Nolan Mkwiche akitabasamu na kumuendea Naomi.
“Naomi,nina maswali machache tu wala sio mengi, ulisema kuwa ulipewa chupa yenye maji ukaambiwa kuwa ukampe Marehemu Heather wodi ya

vichaa,kwanini haukuhoji kuwa chupa ina nini?”
“kwa sababu Enock ni mwanaume ambaye hapendi kuulizwa maswali, pia nilivyomuhoji aliniambia kuwa ataniambia baadaye nikishampa”
“Well…una habari kuwa nawewe unakesi ya mauaji,alivyokwambia kuwa umfichie siri yake nawewe ukafanya ivyo hilo ni kosa kifungu namba tatu,umemficha

muhalifu,nina uwezo pia wa kukufungulia kesi, una kataa unakubali?”
“Muheshimiwa Nolan hapo unakuwa kama unamfosi mteja wangu kukubali kosa na unakuwa kama unamtisha”
Alikatisha maongezi wakili Faaris alivyoona swali hilo litakua na utata sana.
“naomba aendelee kunijibu maswali yangu,ni kosa la mauaji vile vile kumficha muhalifu kifungu kitam-bana”
Waliendelea kulumbana mpaka Wakili Faaris alipotulizwa ili amuachie uwanja Nolan Mkwiche aulize maswali.
“kwanini polisi walivyokuhoji kuhusu hayo maji yenye sumu ukawajibu kuwa ni kwa ajili ya panya na marehemu Heather alikunywa kwa bahati mbaya

ulivyotoka,nani aliyenunua hiyo sumu wewe au Enock?”
“Ni Enock ndiye aliyenunua na kuiweka ndani ya maji kisha kunipa”
“Huoni kuwa unasema uwongo,asubuhi ya siku hiyo hiyo uliamka na kwenda dukani kwa kimario pale jirani na kununua sumu hiyo ya panya na siku hiyo hiyo

habari za msiba zika letwa,unaweza ukalizungumzia hilo,?”
Wakili Nolan Mkwiche kila alilosema alikua na uhakika nalo, ni kweli alikua na ushahidi wa kila kitu kuhusiana na kifo cha Heather, aliamini kesi hiyo ataenda

kushinda alijiamini sana.
Jaji Patrick Ndilito aligonga nyundo mezani na kesi kuhairishwa mpaka mwezi ujao tarehe kumi na saba mwezi wa kumi!.
Watu wote walitawanyika na Enock kurudishwa maabusu ili kusubiri siku nyingine ya kesi yake.
Wakili Nolan Mkwiche alimuhakikishia kuwa ataenda kushinda na kuwa huru, maana kila vithibitisho anavyo lakini alichomsistizia ni kuwa azidi kukanusha juu

ya sumu iliyokua imewekwa ndani ya maji.
“Nakuhakikishia utashinda utakuwa huru,Naomi hawezi kutoka hata kidogo Yule wakili anayemtetea hawezi kitu,cha kufanya endelea kukataa kata kata, kama

nilivyokwambia kama ukiulizwa swali liki kuchanganya usitoe jibu lolote!”
Ivyo ndivyo alivyoambiwa na wakili wake ambaye alimtafuta kwa pesa nyingi sana.Kway,Mtoto wa Becker pamoja na Anderson Peter, nao walimfata na kumpa

pole , wote walimtia moyo kuwa atashinda kesi hiyo, kwani waliamini kuwa Enock hana hatia hata kidogo.
Ndugu wa Marehemu Heather waliungana na Naomi na kuzidi kumkandamiza sana wakimtuhumu kuwa ndiye yeye aliyefanya mauaji hayo.
***
“Mambo Naomi”
“safi tu”
“Naona umeamua kumshtaki mpenzi wako lakini ni safi sana”
“ndiyo alivyokutuma Enock uje kunilaghai?”
“Hana jeuri hiyo hata kidogo,tuachane na mambo ya kesi, mimi nimekuja na mambo yangu binafsi”
“nakusikiliza”
“hapa sio pa kuyaongelea,mimi nataka nikusaidie”
Nolan Mkwiche wakili wa Enock alimtafuta Naomi na kuanza kujenga naye mazoea ya karibu sana,ndani ya siku tatu tu walikua ni marafiki wa karibu sana.
wakiwa wanaenda wote sehemu mbali mbali pamoja tena wakiongozana, jambo hilo walifanya siri sana bila ya Enock kujua lolote lile,CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Ni kweli Nolan aliamua kuwa upande wa Naomi na kuwa naye bega kwa bega na ndiyo ivyo alivyomwambia na wote walikubaliana kumkandamiza Enock, kwa

mara ya kwanza Naomi aliona ni njama tu ila baadaye alikubali sana na kufurahi.
“nataka nikufanye hii kesi ushinde,kama ukinilipa pesa nazotaka mimi naona Enock ni m-babaishaji tu ananiletea longolongo”
Alisema Wakili Nolan Mkwiche siku hiyo wakiwa ndani ya mgahawa wa samaki samaki.
“unataka bei gani kwani?”
“Laki tisa tu,Enock atanyea debe segerea”
“ina maana Enock kashindwa kukulipa izo pesa?”
“anadai haniamini hata ivyo siku izi kafulia hana pesa kachoka sana,ukinipa hiyo pesa mimi naondoka zangu namuachia hiyo kesi najua ni lazima atawekwa

ndani kifungo cha maisha,”
“umenifurahisha sana Nolan,sawa nitafanya ivyo kesho jioni nitakupa hiyo pesa,naomba usinilitee za kuleta”
“niamini nayokwambia, hii kazi sijaanza leo unajua”
Habari izo zilimfanya Naomi afurahi kupita kiasi, hakutaka kumwambia mtu wa aina yoyote ile, siri hiyo walibaki nayo yeye pamoja na Nolan wakili wa Enock,

hakutegemea kama mambo yangemnyookea kiasi hiko laki tisa haikuwa pesa kubwa kwake.
Hata ivyo kwa gharama yoyotebile ilikua ni lazima amuweke Enock ndani au waende wote Gerezani, lakini dalili zilionesha kuwa yeye atakua huru na Enock

kufungwa kifungo cha Maisha na ndiyo ivyo alivyohaidiwa na wakili Nolan Mkwiche.
Bila kujifikiria alichukua kiasi cha laki tisa kisha kumtafuta Nolan hewani, kesho yake aliwasha gari mpaka Salasala nyumbani kwa Nolan mkononi akiwa na

bahasha ya kaki iliyojaa Noti nyekundu.
Alivyofika tu alimkabidhi pesa izo.
“kwaiyo niambie cha kufanya,kabla ya kuondoka au ikitokea nimepanda kukuhoji nataka nijue ni kweli uliweka sumu ya panya na Heather kufariki?”
“Ndio mimi ndiye niliyeweka sumu ile kwenye maji,nilitaka anioe mimi Naomi”
“Ha!Ha!Ha!, sasa ilikuwaje akaghairi?”
“Alikuja sijui Demu gani sijui from no where akadai sijui alidhani amekufa,nilikasirika sana nikaamuua kufanya ivyo ana bahati sana nayeye ningemuuwa shenzi

zake”
“Duu pole sana, sasa mimi ndio naondoka ivyo sasa hivi, nakutakia kila la kheri, usimwambie mtu yoyote kuwa tulionana, sawa?”
“sawa,mimi naenda”
Naomi aliondoka akiwa mwenye furaha ndani ya moyo wake,
shukrani aliyompa Nolan haikuelezeka hata kidogo, aliwasha gari mpaka kwake na kujitupa kitandani akiwa mwenye furaha alijiona mshindi sana.

“lazima afie jela, shenzi zake”
Aliwaza Naomi.
Siku zilikatika na majuma kusonga hatimaye mwezi kuisha na tarehe ya kesi ya Enock kufika.
Watu walikusanyika mahakamani umati wa watu ulifurika kila mtu alitega sikio, Bado Enock aliendelea kukanusha kuhusu mauaji ya marehemu Heather

aliyoshutumiwa kuwa yeye ndiye aliweka sumu hiyo kali ndani ya chupa ya maji na kumtuma Naomi, alikataa kata kata.
Alivyopanda Naomi alizidi kumkandia akiongeza chumvi dalili zilionesha kuwa anaenda kushinda kesi hiyo.
Kilichomchanganya Enock na kila mtu ni baada ya kutokumuoana wakili Nolan,
hawakuelewa nini kimetokea isipokua kwa Naomi yeye alijua kila kilichotokea,alitabasamu na kuona mambo yanaenda kama yalivyopangwa.
Picha ilionesha kuwa anaenda gerezani

kilimchomjia kichwani ni milango ya gereza inafunguka nayeye kutupwa ndani gerezani akihukumiwa kifungo cha Maisha, machozi yalianza kumlenga, Dunia

aliona ipo chini juu,juu chini alimtizama Naomi kwa macho ya huruma, alishaelewa kuwa yeye ndiye mkandarasi wa matatizo yake yote yanayomtokea mpaka

yeye kufungwa, alitamani muda urudi nyuma ili aweke mambo sawa lakini ilishindikana!.
Ghafla kila mtu aligeuza shingo yake nyuma na kushangazwa baada ya kumuona Mwanaume mnene kiasi aliyekua amevalia suti nyeusi kutokeza,
Enock alitabasamu na kujipa tena moyo baada ya kumuona Mkombozi wake amefika Wakili Nolan Mkwiche.
Naomi alishindwa kuelewa ni kitu gani kimetokea moyo ulimwenda kasi.
Nolan Mkwiche aliweka begi lake dogo mezani kisha kupita mbele na kumkazia macho Naomi aliyekua akitokwa na jasho mwilini mwake anatetemeka.
Bila kuongea chochote alitoa kamera na kinasa sauti kisha kukiweka mezani,kila mtu alitega sikio lake kusikiliza.
“NDIO MIMI NDIYE NILIYEWEKA SUMU KWENYE MAJI,NILITAKA ANIOE MIMI NAOMI,…”
Sauti ya Naomi ndiyo iliyosikika kutoka kwenye kinasa sauti.

Watu wote walikuwa katika hali ya utulivu wa hali ya juu,wakitaka kujua hukumu ya Enock ambaye leo hii ana shtakiwa kwa kosa la mauaji ya kumuwekea

sumu ya panya Mke Wake Heather akiwa wodi ya vichaa Muhimbili,
Mchumba wake Naomi ndiye aliyefungua kesi hiyo akishirikiana na Ndugu wa marehemu Heather, kila mtu alimchukia Enock wanawake walimuwekea vigenge

na kumteta wakitaka afungwe kifungo cha maisha au anyongwe kabisa,
kilichowauma zaidi ni kitendo cha kusikia alimpiga mke wake enzi za uhai wake alivyokuwa mjamzito akidai kuwa alimuendea kwa waganga.
“Huyu kaka afungwe ningekuwa mimi ni jaji nisingesikiliza hiyo kesi,ni kufungwa tu”
“wamlete hapa tumpige ata viboko,huyu angekuwa kule Mexico angenyongwa yaani nashaangaa hii nchi yetu ya Tanzania mtu kama huyu anapumua bado”
“Mimi kaniudhi kwa kweli”
Hayo ndiyo maneno yaliyosikika mitaani kutoka kwa baadhi ya watu waliosikia habari izo.
Kila mtu alitega sikio lake kusubiri hukumu ya Enock, wengi waliomba afungwe kifungo cha maisha.
Wakili Nolan Mkwiche ndiye alikuwa akisubiriwa kama mtetezi wa Enock dakika kumi sasa zilipita bila kutokeza mahakamani, hawakuelewa nini kimempata, CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

ndugu wa upande wa Enock walizidi kuingiwa na Mashaka walishajua maana yake kuwa ni lazima Enock afungwe kifungo cha maisha kutokana na kukosa

kithibitisho na utetezi wa aina yoyote ile.

Ghafla Wakili Mkwiche aliingia akiwa ana tabasamu sana kisha kuweka kinasa sauti pamoja na mkanda wa video uliowachukua yeye na Naomi wakiwa katika

maongezi. Alitumia njama hiyo ili kumkamata Naomi kirahisi na kweli alifanikiwa kabisa, hakukuwa na haja yoyote ile ya kuzidi kumuweka Enock kizuizini.
Jaji aligonga Nyundo mezani na Naomi kuhukumiwa kifungo cha Maisha jela kwa kosa la kuuwa kwa kukusudia huku Enock akiachiwa huru aende,
machozi ya furaha yalimtoka Enock hakuamini hata yeye kile anachosikia kutoka kwa JAJI aliyekuwa kushoto kwake kwa juu, alishaamini kuwa anaenda

kutumikia maisha yake yote Gerezani,hapo ndipo Askari magereza walimuendea NAOMI na kumfunga pingu kisha kuondoka nae huku akiwa analia machozi

mengi mfululizo.
Tayari waandishi wa habari walikuwa nje na kamera zao walitaka kujua ni kitu gani kimetokea, Catherine muda wote alikua ni mwenye furaha kupita maelezo

yaliyojitosheleza.
“Enock Mpenzi”
“Naaam Catherine”
“nakupenda sana”
“Hata Mimi”
Muda wote walikumbatiana kwa furaha wakiwa na amani ndani ya mioyo yao. Mtoto wa Becker, Kway, Mama Catherine pamoja na Anderson Peter muda wote

walikuwa wenye furaha wamemzunguka wanampongeza sana, hata wao aliwashukuru kwakuwa naye bega kwa bega.
“Namshukuru Mungu sana kwa kuuonyesha ukweli, Nolan nashukuru sana kaka najua umefanya kazi kubwa sana,jioni la leo naomba uungane kwenye sherehe

nitakayo fanya kwenye ukumbi wa Meeda pale sinza, tafadhali usikose”
Enock aliongea akiwa mwenye furaha muda wote anatabasamu alijiona ni Mshindi sana, ndani ya akili yake aliwaza ndoa atakayo funga na Catherine na ndiko

hiko kitu kilichobaki na wala sio kitu kingine,
Karandinga la magereza lilifika mahakama ya kisutu kisha Naomi kutupwa akiwa na wafungwa wengine,
walitizamana na Enock na kuingizwa ndani ya gari hilo maalumu linalobeba watu waliohukumiwa vifungo kisha kuwapeleka magerezani.
Enock na ndugu zake huku Catherine akiwa pembeni Waliingia ndani ya magari yao kisha kuondoka,moja kwa moja walifika nyumbani kwa Anderson Peter ili

abadili nguo, Siku hiyo ilikuwa ni siku ya furaha sana ndani ya moyo wake,hakuweza kufurahi mwenyewe siku hiyo, aliwapigia simu wafanya kazi wake wote

pamoja na ndugu jamaa na marafiki zake ili waweze kuungana katika ukumbi wa Meeda uliopo sinza.
***
Watu walizidi kufurika wakiudhuria sherehe ndogo iliyoandaliwa na Enock baada ya kupitia matatizo yote na kukaa mahabusu miezi kadhaa, alishajua teyari

anaenda kusota Gerezani lakini alimshukuru Mungu wake aliye juu sababu bado alikua akimpigania na kuyapigania maisha yake kwa ujumla.
Hapo ndipo alipoamua kuandaa ukumbi ili waweze kusherekea siku hiyo aliyoiita siku ya ushindi!.
Magari ya kifahari yalizidi kufurika hata paking kukosekana ni kweli Enock alikuwa ni mtu wa kupendwa na watu sababu ya upendo wake aliweza kujuana na

watu wote tofauti.

Mtoto Wa Becker ndiye aliyeteuliwa kuwa mshehereshaji siku hiyo ya tafrija ndogo akiwa amevalia suti nyeupe mpaka viatu alivaa vyeupe, sherehe ilizidi

kunoga ilivyofika saa nne ya usiku!.
“Mr. Enock Mwasha napenda kukuita mbele ili uweze kuongea machache D.j Msindikize na ngoma kali”
Alisema Mtoto wa Becker huku akitabasamu Kisha Mwanaume Mrefu maji ya kunde kusimama mpaka mbele ya Mtoto wa Becker na kuchukua kipaza sauti,
Mziki ulizimwa ili kila mtu aweze kumsikiliza Enock aliyekuwa ameandaa sherehe hiyo kama shukrani kwa watu wote waliompigania mpaka hapo alipofika na

watu wote walioonyesha kuwa naye bega kwa bega!.
“Well…NAPENDA kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyetupa Pumzi yake bure,Atukuzwe yeye naomba kidogo tufumbe Macho yetu ili tumkumbe Mama yangu

kipenzi na tuweze kumuombea huko alipo apumzike kwa Amani kwa sababu siwezi kumsahau Marehemu Mama yangu,angekuwepo hai nafikiri angefurahi sana!

Naamini kimwili hayupo nasi ila tupo naye kiroho”
Watu wote waliyafumba macho yao na ukimnya kutawala kama dakika tano nzima kisha Enock kuendelea kuongea.
“Leo nina mengi ya kuongea,lakini napenda nifupishe ili tuendelee na tafrija ya leo tunywe tufurahi kwa ujumla, kuna muheshimiwa napenda nimuite hapa mbele

yenu na huyu ndiye aliyefanya sisi tujumuike sote, naomba nimuite Mr.Kway hapa mbele najua hamtaelewa ila mtajua kwanini”
Kway alishtuka hata yeye hakutegemea kama angeitwa, alimgeukia Mke wake Julia kisha kusimama na kwenda mbele kisha baadaye Catherine kuitwa pia.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Napenda leo kutangaza Rasmi mbele yenu Catherine ndiye mchumba wangu ninaenda kumfika pete ya uchumba, nampenda sana huyu Mwanamke, tumepitia

mengi sana, na huyu mnayemuona hapa ni Baba Mkwe wangu”
Catherine aliyekuwa mbele alipigwa na butwaa moyo unamdunda sana hata yeye hakuamini kuwa anaenda kufikwa pete ya uchumba, jambo Hilo Enock

alilifanya Siri sana,hapo hapo alitoa pete mfuko wa nyuma.
“Catherine will you Marry me?”
Aliuliza Enock, Catherine alishindwa kuyazuia machozi yake ya furaha, alijikuta analia huku akiweka mikono yake kinywani moyo ulimwenda mbio sana

haamini kama leo hii yupo na Enock tena wamerudi kwenye furaha, alichotakiwa yeye ni kujibu swali aliloulizwa ili zoezi hilo litokee.
“Y..es Ye..s Enock”
“NAKUPENDA CATHERINE!”
Kwa heshima yote Enock alipiga magoti na kumvalisha pete Catherine mwanamke ambaye anampenda kuliko mwanamke yoyote yule chini ya jua la Mungu, na

ndiye mwanamke aliyeamini kuwa aliyechaguliwa na Mungu,
Hata yeye hakuamini kuwa ameweza kufanikisha hatua hiyo, ni mambo mengi sana walipitia mpaka kuuwa watu na kuchukiana hata na Baba yake mzazi kisa

mwanamke huyo.
Kilichosikika ni kelele kutoka nyuma na makofi kila mtu alifurahishwa na kitendo hiko alichokifanya Enock, walikumbatiana wote wawili wakiwa wenye furaha

mioyoni mwao,
sherehe ilizidi kupamba moto wageni waalikwa walizidi kunywa na kula na wegine kusaza hata chakula kubaki kingi.

Upendo ulizidi mara dufu walizidi kuoneshana mapenzi ya dhati kila sehemu wakiongozana kilichokua kina subiliwa hapo ni harusi kubwa sana,
Enock aliipania sana Harusi hiyo ivyo alifanya kazi kwa bidii ili apate pesa nyingi, alitaka ndoa yake iwe historia na izungumziwe na kila mtu huku taratibu

akitafuta nyumba ya kuishi, Mungu si Athumani alipata nyumba kubwa iliyokua ikipigwa mnada kwa bei rahisi sana maeneo ya Kibaha, licha ya kuwa mbali na

mjini lakini ilikua na kila kitu ndani na uwanja mkubwa, baada ya kumaliza malipo ya nyumba hiyo alianza taratibu kuikarabati, baadaya wiki mbili kukatika

ilikua teyari ina vitu vya thamani ndani.
“Darling,nataka leo ukaione nyumba yangu mpya”
Enock alimwambia Mchumba wake siku hiyo akiwa ofisini.
“nitafurahi sana Mpenzi wangu”
“unanipenda Cate?”
“ofcourse yes”
“Nafurahi kusikia ivyo mke wangu mtarajiwa,subiri nimalizie hii kazi hapa kisha tuongozane mpaka nyumbani kwangu, hope utapapenda!”
“mpenzi, kila unachokipenda wewe mimi nakipenda pia”
“okay sawa”
Ni kweli baada ya shughuli kuisha Enock alisimama kisha kumshika Catherine na wote kuongozana mpaka kwenye maegesho ya magari.

Wafanyakazi wake wote walishamjua Catherine kuwa ndiye Mke wa bosi wao hata wao walimpenda sana Catherine, muda wote alikua akitabasamu na kuongea

na kila mtu hakuringa, kila mtu alikiri kuwa mwanamke huyo ni mzuri hana mfano wake alijaaliwa kila sehemu,
akitembea basi hata wanawake wenzake ni lazima wageuze shingo zao.
Enock alizidi kumtunza, hata yeye aliweka kifua mbele akitembea naye popote pale tena hutanua mikono yake, alijiona ni mwanaume mwenye bahati kumpata

mwanamke huyu Mzuri ambaye hata baadhi ya Makampuni mbali mbali walimtaka japo afanye matangazo, hakutaka jambo hilo litokee hata kidogo alilipiga

vita.
“jamani Herman Milinga si nilishasema sitaki hayo mambo yenu, sitaki sitaki naomba mnielewe, sawa…. hata kama okay what ever,mtamlipa pesa nzuri,hana

dhiki hiyo so please find someone else,wanawake mbona wapo wengi mjini,hamjamuona Shasharty Miss Tanzania mtafuteni huyo, lakini kuhusu Mchumba

wangu Hell no”
Enock alikata simu yake kisha kumgeukia Catherine aliyekua anatabasamu hakika alikua mzuri, Mungu alimpendelea kwa kila kitu.
Walinyoosha na kufika Ubungo, baada ya taa za kijani kuwaka na kuruhusiwa walizidi kusonga mbele mpaka walipofika Kibaha, hapo waliacha bara bara ya lami

kisha kuingia kwenye barabara ya vumbi na kukunja kushoto kisha safari yao kukomea kwenye geti kubwa jeusi,
Baada ya honi kupigwa Mlinzi alisukuma geti kubwa la kisasa lenye matairi kwa chini kisha Enock kuingiza gari mpaka kwenye maegesho maalumu na kupaki

gari lake.
“Mpenzi umejitahidi, ni nyumba nzuri naona kuzidi hata ile”
“Hapana Darling”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“kweli tena Baby”
Wote waliingia ndani na kukaa kwenye masofa, ilikua ni nyumba ya kisasa yenye seble kubwa,muda wote kulikua kuna kiyoyozi,walichokuwa wanaongelea sio

kitu kingine bali ni mambo ya ndoa yao, hapo ndipo Enock alipochukua Glass ya Catherine na kuiweka mezani kisha kumsogelea mdomoni,
wote walikutanisha ndimi zao na kuanza kubadilishana mate taratibu sana,
Hawakuwa na haja ya kuendelea kufanya tendo hilo seblen, kwa kuliheshimu tendo hilo Enock alimbeba Catherine huku wakiwa wanapigana denda mpaka

chumbani juu ya kitanda puu!

Walizidi kunyonyana ndimi zao taratibu sana hakuna aliyekua na haraka hata kidogo, Enock taratibu alimvua Catherine nguo yake ya juu kisha kuitoa blazia

aliyokua nayo hakua na jingine zaidi ya kuanza kuyanyonya maziwa ya Catherine taratibu na ulimi wake hususani juu ya chuchu zake huku mkono mmoja

akiushusha mpaka chini ya ikulu na kuanza kuipapasa taratibu sana sehemu ya juu na kumfanya Catherine aanze kujipinda,
alishuka chini kisha kuivuta sketi ya jinsi na kumfanya Catherine abakiwe na boxa peke yake,
hapo ndipo alipoitoa na kuipanua miguu yake kisha kuingiza ulimi ndani ya mgodi taratibu na kuanza kuulamba kama paka alambavyo maziwa yaliyokua juu ya

kisosi, Catherine alichukua mikono yake na kuanza kulivua shati la Enock, ndani ya dakika mbili wote walikua kama walivyozaliwa……

Mzee David Mwasha ni jambazi sugu, aliyesifika na jina lake kuvuma bara mpaka visiwa vya Zanzibar, lakini hakuchukuliwa hatua yoyote ile na jeshi la polisi

kutokana na kuwa na mkono mrefu wenye pesa ,Polisi waliomfuata walipewa hongo na kukaa kimnya, kundi la NO MITEGO lililosifika kwa upambanaji ya

michezo ya kick boxa alilidhamini nakuwalipa pesa nyingi,na ndiyo hao vijana aliowatumia kwa kazi zake za uvamizi wa bank na utekaji wa meli zenye mizigo

mikubwa kisha kuwauwa watu wasiokuwa na hatia,

alishaamua kuwa jambazi sasa na kufanya kazi za uharamia,
kundi hilo la No Mitego lilivuma sana kwa kazi hizo na kuzidi kuwakusanya watoto wa mitaani ambao hawana kazi, kundi liliposhikiliwa na polisi Mzee

Mwasha aliwakikingia kifua na kuwatolea pesa nyingi ili waachiwe huru.
Hakuweza kufanya ivyo peke yake alikua akila njama na mkuu wa kituo cha Zanzibar na ndiye huyo aliyekua akimpa michoro yote jinsi ya kufanya uvamizi na

baadaye kugawana pesa,
ivyo ndivyo ilivyokuwa, licha ya hayo yote anayofanya alikuwa bado ana kisasi na Mtoto wake Enock,Sabrina pamoja na Catherine ilikua ni lazima awauwe tena

kwa mikono yake.
Taarifa izo ziliruka mpaka jijini Dar es salaam kituo cha polisi cha staki shari na kuweka kikao kidogo, hawakutaka kulifumbia macho swala hilo, ilikuwa ni

lazima wamuweke Mwasha kituoni awe hai au amekufa, na ndipo hapo walipofunga safari mpaka Zanzibar na kupokelewa na Jeshi la polisi visiwani Zanzibar,

Mzee Mwasha alishapewa taarifa izo siku mbili nyuma kabla, ivyo nayeye alindaa jeshi lake ili kuwafunza adabu.
Walipokelewa na kufika kituo kikubwa cha polisi Madema ili kupanga mikakati yao.
“Sasa tunaanzia wapi?”
Aliuliza Kaminshna wa Dar es salaam Bonifasi Kobello.
“huyu ana patikana huko Kizingo Atiii, itabidi siye twendeee tukamkamate sasa hiviii yakheee”
Alijibu Koplo Abdul, IGP wa Kituo cha Madema kwa rafudhi ya kwao.
“sasa nafikiri vijana wako wapo tayari?”
“ndio”
“Ngusa utaongoza kikosi,tutaondoka leo usiku saa moja ya jioni ili kufanya Ambushi hiyo kimnya kimnya”
“Sawa Mkuu”
Kikao kizima walipanga jinsi ya kumkamata Mzee Mwasha na kumuweka kizuizini,Ni kweli walikuwa wamejipanga vya kutosha, saa moja ya jioni ilipofika tu

waliwasha Diffenda na magofu ya polisi kwa safari ya kuelekea msitu wa kizingo uliosifika kwa kuwa na majambazi, ambapo huko waliweka makambi yao.
Ulikua ni msitu unaotisha hakuna mtu aliyethubutu kukatiza ifikapo jioni,watu waliuwawa kila kukicha.
Baada ya kutoka kituoni Madema walinyoosha kilimani na kukuta maungio ya barabara,
waliacha barabara inayokwenda Gereza la Kinua na kufuata njia ya kwenda hospitali kuu ya Mnazi mmoja kabla ya kufika hospitali, gari zilisimama upande wa

kushoto sehemu iliyojaa na kuzungukwa na miti aina ya mikoko, kisha taa za magari kuzimwa!.
“Ndio hapa?”
“ndio hapa inabidi tushuke”
“sawa jamani kuweni makini Ngusa na vijana wako piteni upande wa kule mtaongozwa na Afande BARAKA, wewe Joshi na wenzako mtapita kushoto,sisi

wengine tupite kati kati”
“sawa Mkuu”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“sawa mkuu”
Polisi wote walikuwa makini kila mtu kashika bastola yake mkononi tayari kwa kuachia risasi, giza lilikua nene sana.
Walizidi kusonga mbele wakipita ndani ya miti hiyo ya mikoko.Ilikua ni lazima wamkamate Mzee Huyu Hatari sana, kabla hawajafika mbali walisikia milio ya

risasi inarindima upande wa magharibi, hofu ilizidi kuwatanda.
“Afande afande unanisoma kiiisshhh,Afande ova Afande Ngussa Kishhhhh Afande Mbaruku ovaa”
Hofu ilizidi kuwatanda baada ya kukosa jibu upande mwingine wa redio upepo,
Ghafla lilitokea kundi la watu wengi wakiwa wenye silaha za moto na kuwazunguka, polisi wote waliwekwa chini ya ulinzi.
“Pigeni magoti”
“yakhee tafadhali usitutoe uhaiiii, tuoneee hurumaaa hatutorudia tenaaa atiiiiii”
“Kaa kimnya”
“Nani kawatuma?”
“huyuuu hapaaaa ndiyo katoka huko baraaa sisi hatuna shidaa na nyieee hataaa kidogoooo”
“Paaa paaa paaaaa”
Pale pale kamishna Kobello aliuliwa kwa kupigwa risasi za kichwa, ni kweli watu hawa hawakuwa na masihala hata punje, walikua na roho za kinyama, kuuwa

mtu kwao ilikua ni kawaida sana na ndiyo hiyo amri waliyopewa kutoka kwa tajiri yao Mzee mwasha,
baadhi ya polisi waliinuliwa na kuwekwa mateka mpaka ndani ya nyumba kubwa ya Mwasha kwa ajili ya kuhojiwa kisha baadaye wauwawe.
“nani kawapa hiyo amri huko Dar es salaam?”
Aliuliza Mzee Mwasha.
“Mimi mimi mimi alikuja kijana mmoja kufungua kesi hiyo ni mwanao anadai anaitwa Eno Enock alafu tukapewa Amri na na Mkumbo”
“Ha ha ha ha ha,Mkumbo namfahamu nitajua cha kumfanya”
“okay, huu utakuwa kama ujumbe”
Hapo hapo baada ya kauli iyo alichukua SMG na kuwamininia risasi askari waliokuwa mbele yake, hapo ndipo ukawa mwisho wa maisha yao Na maiti zao

kutupwa barabarani,
Askari waliopewa habari izo za wenzao kuuliwa waliogopa sana. Ilibidi wasitishe kwanza zoezi lao na kumsaka Mzee Mwasha.
Kilichobaki ni kitu kimoja tu kumtafuta Enock popote alipo alishaamua kumchukia mtoto wake ki ujumla, alishaelewa kuwa akimfumbia macho atamletea

matatizo hapo baadaye,
haikupita hata siku mbili alishajua tayari ni wapi Enock anaishi na kujua kuwa alishamvalisha pete ya uchumba Catherine na ndoa ndiyo inasubiriwa,
hakutaka hilo litokee hata siku moja, ivyo ilibaki yeye kutuma watu wake wakamuuwe kabisa!.
“Sasa Thomasi,nenda kibaha,huyu ni mtoto wangu mpige risasi muuwe nadhani iyo ni kazi ndogo kwako usifanye makosa hata kidogo”
“sawa nitafanya ivyo”
“Lakini subiri kidogo…”
“Naam bosi”
“nitafutie Sabarina uniletee hapa Zanzibar hii hapa picha yake pia,huyu anaishi Tabata Bima ana duka Kariakoo pale nitakupa maelekezo ukifika Kivukoni nataka

kazi hiyo ifanyike leo hii hii,achana kwanza na Enock najua atajileta mwenyewe”
“sawa Bosi, sitokuangusha niamini, Leo hii hii mzigo wako nitakuletea”
“Nakuaminia Thomasi utaenda na Ngulumbalyo”
“sawa”
Siku hiyo hiyo asubuhi na mapema Thomasi na Ngulumbalyo walitafuta usafiri wa Boti za Azam iliyowavusha bahari ya Hindi na kufika upande wa pili

kivukoni Dar es salaam kwa kazi moja tu kumteka nyara Sabrina na kumpeleka huko Zanzibar kama walivyoagizwa na bosi Wao Mzee Mwasha, ilikua ni lazima

wafanye ivyo,
baada ya kufika walitafuta sehemu nzuri na kupiga simu kwa Bosi wao Mzee Mwasha ili wapewe maelekezo ya ziada.
“Sasa fikeni kariakoo nendeni mtaa wa siku kuu ulizieni duka linaloitwa RASA Classic,hilo duka hamuwezi kupotea hapo hapo mtajua cha kufanya”
“sawa Bosi”
“kuweni makini”
“sawa bosi tuamini uko na majeshi”
“okay”
Baada ya kukata simu zao, walitafuta piki piki zilizowapeleka mpaka Kariakoo mtaa wa siku kuu kisha kuwalipa madereva hao, haikuwa chukua dakika hata

mbili walishafika duka la Sabrina na kumkuta ana wateja wengi, pembeni yake kulikuwa kuna mtoto mdogo anatambaa hapo hapo walimtumia ujumbe mfupi

Mzee Mwasha kwa njia ya simu.
“Na mtoto pia mleteni”
“sawa Bosi”
Hayo ndiyo maagizo waliyopewa.
***
Mpaka usiku unaingia Catherine hakumuona Mama yake, alisubiri na kujua wenda itakuwa foleni za magari,
furaha yake taratibu ilianza kuisha baada ya kufika saa nne ya usiku bila kuona dalili ya gari la Mama yake,wala simu yoyote kutoka kwa Mama yake kama
CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
afanyavyo endapo ana dharura ya aina yoyote ile,
hapo ndipo alipochukua simu na kumtafuta hewani lakini haikupatikana, alizidi kuingiwa na wasi wasi mpaka inafika usiku bado hakumpata hewani, ilibidi

ampigie simu Enock amueleze kinachoendelea na kumuulizia kama aliongea na mama yake siku hiyo, Jibu la hapana lilimchanganya akili yake,
Mpaka kunakucha hakuweza kulala alitafuta daladala mpaka kariakoo kwenye duka la Mama yake lakini alishindwa kuelewa alivyokuta limefungwa

alijafunguliwa nje kuna makufuli makubwa,
alikaa hapo mpaka saa saba mchana ili kumsubiri lakini hakutokea!.
“Samahani,Jana Mama alifunga duka saa ngapi?”
Catherine aliuliza Duka la jirani.
“Mhh Catherine hujambo lakini?”
“samahani shikamoo nimechanganyikiwa hapa,mpaka nimesahau kukusalimia”
“Marahaba, Mama yako alifunga duka hapa mapema sana aliondoka na wakaka wawili alisema anaenda benki kwani vipi?”
“tangu jana hajarudi”
“unasema kweli?”
“kwanini nidanganye Anti”
“ulimtafuta kwenye simu yake?”

“hapatikani”
“Embu tusubiri tuone itakuaje”
Siku hiyo ilipita bila kufanikiwa kumuona Mama yake,kesho yake tena ivyo ivyo, hapo ndipo alipoamua kunyoosha mpaka kituo cha polisi kushtaki.
Wakiwa na Enock wote walisaidiana kumtafuta Mama yake mzazi wakizunguka kila sehemu mpaka hospitali zote,
wiki nzima ilikatika bila mafanikio ya aina yoyote yale na kumfanya Catherine azidi kuingiwa na hofu nyingi sababu hakuelewa ni wapi Mama yake alipo….

Sabrina Mama yake na Catherine kapotea haonekani, Enock na Catherine wanamtafuta jiji zima la Dar es salaam,walishazunguka mpaka mahospitalini na vituo

mbali mbali vya polisi bila mafanikio ya aina yoyote yale,

wasiwasi unazidi kuwaingia, hakuna hata mmoja wao aliyepata hata lepe la usingizi, usiku kucha walikesha wakiwasumbua polisi ni wapi walipofikia.
Taarifa zilizowasikitisha kutoka kwa koplo Jovan ni kuwa kuna ajali mbaya imetokea huko Segera mkoani Tanga, ambapo basi kubwa lililokuwa limetoka Dar

es salaam kuelekea Tanga lilipinduka na kuuwa abiria wote usiku huo huo.
“ndiyo habari iliyo tufikia sasa hivi”
Alizungumza Koplo Jovan.
“sasa mnafanyaje?”
“ngoja tusubirri kukuche ili tujue tutaanzia wapi”
“hapana mimi siwezi kusubiri nitaenda hata sasa hivi”
“sasa huo ni uamuzi wako,nimekwambia subiri kukuche tutaenda sote na eskoti ya polisi”
“mimi siwezi”
“kwaiyo?”
“nitaenda”
“utajijua,shauri yako”
Catherine hakukubali haikuwa kazi rahisi kubadilisha uamuzi ambao ameamua kuufanya, hata polisi ilionekana walishachoshwa na usumbufu wa Catherine

sababu kila siku alikua akifika kituo cha polisi kumuulizia mama yake.
Alimgeukia Enock aliyekuwa pembeni.
“Lakini Catherine”
“Abee”
“Kwanini usiwasikilize polisi”
“kuhusu?”
“usubiri kukuche Mpenzi”
“kama wewe utabaki baki, ila mimi nitaenda mwenyewe hata nikifa najua nilikua namtafuta Mama yangu isitoshe huko alipo yupo na mdogo wangu

Christopher”
“siwezi kukuruhusu uwende mwenyewe mpenzi”
Waliingiya ndani ya gari na Enock kutoa gari mbio mpaka Segera ambapo iliwachukua masaa matatu kufika.

Ni kweli walikuta watu wengi wamelizunguka basi kubwa la abiria ilikua ni ajali ya kutisha sana, baadhi ya ndugu jamaa na marafiki walishafika ili kuangalia

wapendwa wao.
Catherine na Enock waliungana nao baada ya magari ya wagonjwa kufika na kuchukua maiti za wagonjwa ili kuzipeleka hospitali ya wilaya ya Segera hapo

mkoani Tanga.
Catherine alikua na moyo mgumu pengine kupita mwanamke wa aina yoyote ile. ni kitendo cha kuingia Monchwari bila kuogopa na kuanza kuutafuta mwili wa

Mama yake pamoja na mdogo wake christopher, alizidi kufungua fungua mafriji na kuona ni kiasi gani maiti zilivyoharibika usoni.
“Daktari naomba uvute friji nione vizuri”
“sawa lakini binti huogopi?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Tafadhali naomba uvute friji”
Maisha aliyopitia nyuma hakupaswa kuogopa, alishauwa watu wengi sana alishaona maiti nyingi tofauti za kutisha hakuwa muoga tena katika maisha yake kama

hapo awali, sasa alikua ni mwanamke jasiri asiyeogopa kitu cha aina yoyote ile.
Mpaka kunakucha alishapitia maiti zote kisha kuelekea kwenye vyumba vya wagonjwa maututi bila ya kumuona Mama yake mzazi hakujua ni wapi alipo,

alichanganyikiwa sana walirudi ndani ya gari wakiwa na Enock wote wakiwa wamechoka sana.
**
“Kivipi?”
“tumekuta maiti zao kwenye hii njia ya kwenda hospitali ya kwenda mnazi mmoja Mkuu”
“hakuna aliyepona?”
“nina wasiwasi huo”
“okay! Fanya utaratibu wa kuchukua maiti zao zikahifadhiwe kisha urudi ili tuandae jeshi lingine namimi itanibidi nisimamie”
“sawa Mkuu nitafanya ivyo”
Mkuu wa polisi Nchini Tanzania Inspector Mkumbo alikasirishwa sana kupita maelezo, alimtambua sana Mzee David Mwasha kuwa ni mtu aliyeogopeka na ni

katili sana, ni kweli Mzee huyo alitokea kusumbua sana polisi alishauwa kikosi kizima, licha ya hayo alishawahi kumuweka mikononi mwake miaka mingi

iliyopita,

siku hiyo hiyo aliita kikosi cha polisi kituo kikubwa cha posta akiwa mwenye ghadhabu sana, ilikua ni lazima aende Zanzibar siku hiyo hiyo,
“nasikitishwa sana na wenzetu waliouwawa huko Zanzibar.Mungu azilaze roho zao pema peponi,hii haimaanishi kuwa tusiendelee kumsaka Mzee huyu

hatari,Jeshi la Tanzania tumekula kiapo kulitumikia taifa letu na kuwalinda wananchi wetu kiujumla,nahii ndiyo kazi yetu”
Alizungumza Inspector Mkumbo kwenye kikao hiko kisha kuendelea.
“sasa basi leo tutaenda kimnya kimnya kumkamata mzee huyu na kikundi chake kwa ujumla, awe hai au amekufa mimi mwenyewe nitaongoza kikosi,Mjuni anza

kufanya mawasiliano na jeshi la Zanzibar sasa hivi, Haruna piga simu jeshi la majini waambie tunahitaji spidi boti”
“sawa Mkuu”
Mawasiliano yalianza mara moja hapo hapo, huku baadhi ya polisi wakikusanya silaha za moto tayari kwa safari ya kwenda kisiwani Zanzibar,
Saa saba ya mchana walikua teyari, difenda ziliwashwa mpaka bandarini kisha wote kuingia kwenye boti za polisi zinazoenda kasi sana,
baada ya dakika hamsini walifika Zanzibar na kupokelewa na jeshi la Zanzibar!.
Mzee Mwasha tayari Alisha pokea taarifa za ujio wa jeshi hilo kutoka Tanzania siku hiyo asubuhi na mapema kutoka kwa mkuu wa polisi jeshi la Zanzibar,

nayeye ilibidi ajihami kama alivyofanya Mara ya kwanza aliweka watu wake na kuwapanga vizuri.
“Rodgers utapanga watu wako kule mbele kabisa mwanzoni,najua watatokea kule juu,wewe Mick utakaa huku nyuma mwanzoni mtawasubiri wote waingie

ndani kisha muwazunguke”
“sawa Bosi usijali kwa hilo hiyo ni kazi ndogo sana kwetu sisi”
“sawa kuweni makini”
Hayo ndiyo maagizo waliyopewa na mzee huyu katili mwenye roho mbaya kumzidi Shetani huko kuzimu,
alishaamua kumwaga damu kwa yoyote atakae ingia katika himaya yake, Ni kweli mzee huyu alitisha sana kuliko ugonjwa wa ukoma.

Alirudi mpaka kwenye ngome yake kubwa ambayo alikua akiishi, ilikua ikilindwa sana kama ya mfalme.
“Sabrina”
Aliita Mzee Mwasha.
“Mara ya mwisho kukuona ilikua nyumbani kwako lakini sina kumbu kumbu vizuri nilitaka kumpiga risasi Catherine, sitoweza kukuuwa mpaka wenzako

wakamilike Enock na Catherine, punguza presha bado una siku za kumuomba Mungu wako na kumuomba msamaha”
“Kwanini unafanya hivi?”
“unataka kujua?”
“ndio”
“Ramsey ndiyo anakufanya leo hii uteseke,alinikosea sana yeye ndiye kanifanya niwe hivi leo hii, nilikua mtu safi sana,ila sasa hivi nimekua na roho ya kinyama

kuliko hata Adolf Hilter natafutwa kila kona,lakini nitahakikisha wewe na wenzako mnakufa wenda nitajisalimisha polisi, una mtoto mzuri sana,Vipi Kway

hajambo?”
Sabrina alishaelewa teyari muda wowote anaenda kufa, hakuelewa ni wapi alipo, mara ya mwisho alikumbuka alikuwa posta na wanaume waliodai kuwa

wanataka kununua nguo duka zima ivyo waende bank kisha walivyofika posta hakuelewa kilichoendelea kuanzia hapo, alijaribu kuvuta kumbukumbu zake bila

kupata majibu.
CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Alivyoshtuka alijikuta yupo juu ya sofa na Christopher pembeni yake lakini tangu akae ndani ya nyumba hiyo alipata kila kitu kuanzia chakula mpaka vinywaji

alikua ni kama mfungwa huru.
Licha ya kufungiwa ndani ya chumba kikubwa alipata huduma zote,lakini alichojua yeye siku zake zinakaribia kufika za kuuwawa,alishawaza njia nyingi za

kutoroka lakini alishindwa kabisa ni wapi aanzie.
“Najua mwanao Catherine pamoja na Enock wanakutafuta sana huko walipo Ha ha ha ha ha ngoja niwapigie simu waje leo hii”
**
Licha ya kumtafuta mama yake kwa takribani wiki nzima bila mafanikio lakini hakuonesha hali ya kukata tamaa hata kidogo, aliamini kuwa mama yake yupo

mahali Fulani lakini sio salama,
alishampa taarifa izo Mpaka baba yake wa hiyari Kway hata yeye alishindwa kuelewa, habari mbaya pia zilizomchanganya ni kuwa mwanae Christopher pia

haonekani,walishaelewa teyari mapambano bado hayajaisha.
“ilikua lini?”
“ni wiki sasa imepita”
“mbona hukuniambia mapema sasa?”
“nilikua nimechanganyikiwa Dad”
“huu sasa ushakuwa mtihani,ulishaenda kutoa taarifa polisi?”
“ndio kote nimeenda lakini hakuna nilichoambulia”
“sawa basi wewe nenda nyumbani nitakupigia simu baadaye”
“sawa Dad”
Kway alimtizama Mke wake Julia aliyekua amekaa juu ya sofa ana mimba changa hakuamini kuwa angeweza tena kushika Mimba,
Mungu ndiye pekee aliyeweza kutenda miujiza,
muda wote alikua naye karibu kuliko kitu chochote kile, hakutaka akae naye mbali hakutaka yatokee yaliyotokea miaka ya nyuma!.
“Cherie. pesa nga mai(Mpenzi naomba maji ya kunywa)”
Alisema Mama Natu huku akiyatoa macho yake makubwa kisha Kway kuenda mpaka jikoni na kumpelekea mke wake Maji ya kunywa,muda wote mwanamke

huyo alideka kama mtoto mdogo wa miaka mitatu.
***
Taarifa alizopewa Catherine kutoka kituo cha polisi siku iyo zilimchanganya sana akili yake, kuwa Gari ya Mama yake ilikutwa posta mpya, hapo hapo hakutaka

kupoteza muda alikodi piki piki mpaka posta ili kuhakikisha ni kweli,
alilikuta gari la Mama yake lakini hakuelewa limefikaje mahali hapo,hakukuwa na dalili ya mtu yoyote kuwepo ndani ya gari,
lilikua katika maegesho ya magari ndani ya hotel kubwa,uchunguzi uliofanywa na polisi haukumridhisha Catherine.
Ghafla simu yake ya mkononi iliita kisha kuipokea.
“Mpenzi Catherine nakumisi sana”
Upande wa pili wa simu ulisikika baada ya kupokea simu yake, sauti hiyo haikuwa ngeni katika masikio yake lakini hakuwa na kumbukumbu nzuri ni wapi

aliisikia.
“naongea na nani?”
“Ha!Ha!Ha!Ha!Ha!Ha!Ha!,Mara hii umenisahau Mpenzi wangu unaongea na wako wa Maisha Mr.Mwasha, Darling ukisikia sauti hii unakumbuka nini?”
“unataka nini?”
“nakuhitaji mpenzi wangu,nakuhitaji uje umchukue Mama yako huku Zanzibar”
Catherine alihisi kuchoka alishusha pumzi ndefu sana na kushindwa kitu chakujibu.
“Naomba usimdhuru Mama yangu tafadhali”
“siwezi kumdhuru Mama mkwe njoo basi mpenzi wangu”
“Nakuja nakuja”
Simu kutoka kwa mzee mwasha ilimtisha sana,
ilikua ni lazima amuuwe mzee huyu ni kweli alishawahi kuwa mpenzi wake hapo miaka ya nyuma iliyopita kisha baadaye kuwindana kama paka na panya,
ilikua ni lazima atafute silaha ndipo aende Zanzibar, alikumbuka sana kuwa Kway ana bastola hapo ndipo alipofunga safari mpaka Kimara kwa msuguli,
Ni kweli alimuhadithia kila kitu Kway kuhusu kutekwa kwa Mama yake na Mzee Mwasha, Kway alivyosikia jina hilo hata yeye alitetemeka sana na kuogopa

alimjua vizuri Mzee Mwasha sio mzee wa kuchezea, alikua ni mzee katili aliyeogopeka sana,
alimtizama Natu na Mke wake Julia ambao walionekana kuwa na hofu sana, wote ilionekana wanamuhitaji, ukizingatia Mke wake Julia ni Mja mzito,

alikumbuka Mimba ya kwanza ilivyoharibika kisa Mzee Huyo Mwasha, picha nyingi tofauti zilipita kichwani kwake na kuona kitu kama filamu ndani ya

halmashauri ya ubongo wake!.
“unasemaye kuwa Mama yako amekamatwa njoo na huyo Mwasha?”
Aliuliza Julia bila Mume wake kujibu lolote.
“Ndio Mama”
“Njoo inakubidi uwende polisi ukawaeleze hilo tatizo”
“sawa Mama nitafanya ivyo”
“pole sana Catherine Muombe tu Mungu atampigania huko alipo atakua njoo salama mukabisa”
Mama Natu alimpa moyo na matumaini Catherine,CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Mahesabu ya Catherine ilikua ni lazima achukue bastola ya Kway na ni kweli alivyopiga jicho chini ya mto pembeni alipokuwa ameketi Kway aliiona kisha

kusogea na kukaa pembeni yake,
taratibu sana kwa uangalifu aliivuta kisha kuiweka vizuri kiunoni tayari kwa kwenda kisiwani Zanzibar siku hiyo hiyo jioni kwa ajili ya kufanya ukombozi

kimnya kimnya bila ya kumwambia Mtu wa aina yoyote ile

“Sawa Mama mimi ninaenda”
“nenda kituo cha polisi kawaeleze kisha uje kuniambia ni kitu gani wamekueleza”
“sawa Dad”
Catherine alisimama vizuri, tena taratibu huku akizidi kuivuta nguo yake ya juu na kuficha bastola aliyoiba,
alivyopiga hatua mbili Kway alimuita na kumfanya aingiwe na Mashaka.
“usijisikie vibaya kwamba nimeshindwa kumsaidia Mama yako,jua kuwa nipo nawewe bega kwa bega nitahakikisha atapatikana, wewe nenda kapumzike sasa

hivi mimi nitajua cha kufanya”
“sawa Dad”
Maelezo hayo tu machache yaliashiria kuwa Kway hakua anaelewa kuwa bastola yake aliyokuwa ameificha chini ya mto anayo Catherine na Muda mchache

itaenda kufanya mauaji na pengine kumuweka katika matatizo makubwa huko mbeleni.

Kitendo cha catherine kutoka nje alikodi piki piki mpaka nyumbani Kwao tabata kisha kushuka na kumlipa dereva huyo wa pikipiki,hakuwa na wazo jingine

zaidi ya kuingia ndani na kuanza kuweka vitu sawa ili siku hiyo hiyo aanze safari ya kwenda Zanzibar akamuweke Mama yake huru pamoja na Christopher.

Haraka haraka alibadili nguo na kuvaa shati refu kiasi huku chini akiwa amevaa suruali ya jinsi, alichukua bastola na kuikagua baada ya kuitoa magazine,

alivyohakikisha imejaa risasi za kutosha aliiweka kiunoni kisha kuifunika na shati tayari kwa safari ya kwenda Zanzibar kufa au kupona,
alitembea mpaka nje lakini ilionekana kuna kitu alisahau na haraka haraka kurudi tena ndani kisha kuingia jikoni na kubeba kisu kidogo cha kujikunja, aliinama

na kukiweka ndani ya kiatu aina ya ALL STAR kilichopanda juu kidogo.
Hapo ndipo alipotoka nje haraka haraka na kulifunga geti vizuri.
“Athumani”
Catherine alimuita dereva wa boda boda.
“sema Catherine”
“hapa na bandarini posta ni kiasi gani?”
“tunaendaga na elfu kumi na tano kule”
“acha zako”
“kweli tena”
“sawa nipeleke basi”
“panda twende”
Catherine alipanda pikipiki kwa nyuma kisha kumshikilia vizuri kiuno dereva,
safari nzima alikua akiwaza sana jinsi atakavyo fika huko Zanzibar ili kufanya ukombozi,
hakua na uhakika kama atashinda lakini alijiamini sana ilikua ni bora afe yeye lakini mama yake abaki huru,

Baada ya dakika hamsini walifika bandarini kisha kumlipa dereva wa pikipiki pesa yake.
“vipi una safari nini?”
“hapana kuna mtu nimekuja kumpokea”
“nikusubiri au?”
“hapana nenda tu”
Alianza kupiga hatua mbili mbili mpaka ndani na kukata tiketi za boti za Bakhresa,
Bahati nzuri alipata boti inayoondoka baada ya dakika thelathini ivyo aliketi na abiria wengine ili kusubiri dakika zifike nayeye aanze safari.
Haikuchukua hata muda mrefu mwanamke mrembo wa kipemba aliyevalia ushungi mweusi alitangaza kuwa boti imeshatia nanga ivyo wasafiri wanatakiwa

waingie ndani ya boti ili safari ianze.

Catherine taratibu alisimama na kuanza kutembea mpaka upande wa pili wa boti kisha kuingia ndani na kuketi kwenye siti yake.
Abiria wote walivyoingia ndani ya boti taratibu ilitoa nanga kisha taratibu kuanza safari yake ya kuelekea visiwa vya Zanzibar ambapo huko Catherine aliamini

kuwa Mama yake pamoja na mdogo wake Christopher wametekwa na Mzee huyu katili na hatari,

ALIYAKUMBUKA MAMBO mengi sana yaliyopita katika maisha yake, fikra zake zilirudi harakaharaka mpaka nchini Brazil tena kitandani walivyokuwa

wakifanya mapenzi na Mzee huyo ambaye alikolea katika penzi lake kisha baadaye kutokea kuchukiana sana,
alitamani siku zirudi nyuma ili aweze kubadili kilichotokea lakini hilo halikuwezekana, ukweli ni kwamba Alimchukia sana Mzee Mwasha.
Alimkumbuka rafiki yake Betty alivyomshauri awe naye kimahusiano ili wamkomoe Enock hakujua kuwa mbele itakuja kuleta uhasama,’majuto ni mjukuu’ leo

hii aliulaumu sana ushauri wa rafiki yake kipenzi Betty.
“Lazima nimuuwe huyu mzee tena kwa mikono yangu Mungu naomba unisamehe”
Aliwaza Catherine huku akiyabana meno yake kwa hasira,
Ni kweli alikua ni mwenye hasira sana kupita kiasi, moyo ulimdunda sana damu ilimuwenda kasi kuliko kawaida, alitamani afike mapema.
Baadaye Boti taratibu ilianza kupunguza mwendo wake baada ya kukata mawimbi kutokea barani Mpaka visiwa vya Zanzibar kisha kuweka nanga na kusimama

kabisa,
Abiria walianza kushuka huku Catherine akiwa ni miongoni mwa Abiria waliokua wanasafiri, kitendo cha kufika bandarini alitoa simu yake kisha kumtafuta

Mzee Mwasha hewani.
“oooh Mpenzi umefika salama?”
Sauti ya upande wa pili ilisikika.
“Ndio”
“nisubiri hapo, umevaaje?”
“shati jeusi na jinsi”
“sawa,”
Ndani ya nusu saa baada ya kuongea na simu aliwaona wanaume wawili wamesimama mbele yake wanamuangalia sana kisha kumsogelea.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Wewe ndiye Catherine?”
Aliuliza Mwanaume mmoja huku akiwa hana uhakika.
“Ndio!.. ndo mimi”
“tumeagizwa na Mr.Mwasha, karibu Zanzibar”
“yeye yupo wapi?”
“twende utamkuta huko”
Waliingia ndani ya gari kisha hapo hapo kumfunika Catherine na kitambaa cheusi usoni ili asiweze kuona njia yoyote ile.

Baada ya nusu saa alifunguliwa kitambaa cheusi, mbele yake aliona ngome kubwa na walinzi wanaolinda huku wakiwa na mitutu mikononi mwao, walimtoa

ndani ya gari kisha kupita naye mpaka kwa Mzee Mrefu aliyekua amekaa juu ya sofa anatabasamu kwa dharau.
“Huyu hapa bosi”
“sawa nendeni”
Hasira zilimkaba tena baada ya kumuona Mzee Mwasha mbele yake tena anacheka kwa dharau huku mkononi mwake akiwa na glasi ya pombe kali.
“Mama yangu yuko wapi?”
“yupo salama usijali hata kidogo, nimefurahi kukuona tena mpenzi wangu Catherine Ramsey Ha ha ha ha ha ha ha ha ha,pole na misukosuko ya maisha

ningekuwa mimi ndiye wewe ningemtafuta mwandishi wa vitabu Bwagayo aniandikie simulizi ingeuza sana,maana tangu Baba yako kifo chake wewe kuteseka

kutuchanganya mimi na Mwanangu Enock,hiyo ingetosha kuandika simulizi na kuuzika na ukapata pesa za kutosha”
Alizungumza Mwasha na kusimama kisha kumsogelea Catherine.
“lakini umechelewa sababu muda mfupi unaenda kuwa historia,Ha ha ha ha ha”
Mzee Mwasha alizidi kuongea kwa dharau sana tena kwa Majigambo, katika maisha yake tangu alivyoanza kuwa jambazi na kulindwa kama mfalme hakuwahi

kuwaza kuwa atakuja kukamatwa siku moja hata kidogo,
alishaweka ulinzi wa kutosha hasa aliposikia siku hiyo kuna jeshi la polisi linakuja kumkamata.
Hapo hapo wanaume Wawili walioshiba walimkamata Catherine na kupandisha naye ngazi mpaka juu na kumtupa ndani ya chumba kikubwa,
Alipomuona Mama yake alimkumbatia na wote kuanza kulia kwa sauti za kwikwi mfululizo!.
“Ma..ma”
Aliita Catherine kisha kutoa bastola kiunoni baada ya kupangusa machozi yake.
“Catherine usifanye ivyo”
“No Mama, lazima tutoke humu nimekuja kukukomboa wewe na Christopher niamini Mama”
“Cate hata ukifanya ivyo ni kazi bure tazama nje kuna walinzi wa kutosha unadhani tutawezakutoka?”
“Mama usiwe na wasiwasi kuhusu hilo, Mimi nitafanya kila kitu, cha kufanya jiweke tayari kwa kuwa huru”
“Lakini sawa…..”
Mama Catherine bado alikua na mashaka hakuweka matumaini juu ya mpango wa Catherine aliokua anaupanga wa kutoroka ndani ya ngome hiyo inayolindwa,
wote walishtuka baada ya usiku kuingia, walisikia milio ya risasi inarindima mfululizo,
waliogopa sana na hofu kuwatanda mioyoni mwao, milio ya risasi sasa ilizidi kusogea karibu,
walivyochungulia nje waliwaona polisi wakiwa wanarusha risasi na kupambana na jeshi la Mzee Mwasha, lakini polisi walionekana kuzidiwa na wote kuuwawa.
**
“Inpector Mkumbo”
Alisema Mwasha huku akimtizama Polisi huyo kwa macho makali, ni kweli watu hawa wawili walikua na historia, walikua wakiwindana kama paka na panya.
Mawazo ya Mzee Mwasha yalirudi nyuma kama mkanda kisha kukumbuka alivyoteswa na polisi huyo mpaka akatolewa baadhi ya meno yake mdomoni.
Hapo hapo alikunja ngumi na kumtandika nayo usoni iliyomfanya polisi huyo aende chini mzima mzima.
“Subiri siku zako za kuishi leo upo kwenye himaya yangu nimefanya kusudi kukuacha hai nataka ufe huku unateseka,Rodgers mshughulikie”
Kauli hiyo ilivyotoka kwa Mwasha tu Rodgers alianza kumpiga polisi huyo ngumi zisizo kua na idadi kamili mpaka alipopoteza fahamu zake, walimuacha hapo

hapo mpaka siku inayo fuata kisha Catherine na Mama yake kutolewa nje ili wateswe kisha baadaye wauliwe,
Catherine hakutaka jambo hilo litokee hapo ndipo alipotoa bastola yake, lakini kabla ya kufanya lolote Rodgers alimrukia na kumpiga kichwa cha puani huku

bastola ikidondoka upande wa pili na Mzee Mwasha kuiwahi!.
“Nasikia siku izi unapigana ngumi,nataka nione leo”
Alizungumza Mzee Mwasha kisha kuketi kwenye kiti akiwatizama Rodgers na Catherine waanze kupigana.
Catherine alikunja ngumi vizuri alishaelewa mtu huyo Rodgers ana mafunzo ya kutosha sababu walishawahi kupambana na kupigwa sana ivyo umakini wa hali

ya juu ndiyo ulihitajika,
aliiona ngumi inakuja na kuhepa kushoto kisha kukaa sawa, alitisha kama anarusha ngumi ya kushoto na kurusha ya kulia iyo ilizaa matunda na kumfikia

Rodgers puani hapo hapo aliruka juu na kujizungusha hewani na teke aina ya round kick lililomfanya Rodgers aende chini chali…

*****

Mama catherine ametekwa nyara na Mzee Mwasha yupo huko visiwa vya Zanzibar,huku nyuma akimuacha Mwanae Catherine asipate hata lepe la usingizi CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

akimtafuta usiku kucha bila mafanikio ya aina yoyote yale, alisharipoti mpaka vituo vya polisi lakini hawakumpa majibu yaliyomridhisha kabisa.

Baadaye anapigiwa simu na Mzee Mwasha kuwa yupo na mama yake, hapo ndipo anaamua kuiba silaha na kuamua kwenda visiwa vya Zanzibar kimnya kimnya

ili akafanye ukombozi akijiita jeshi la mtu mmoja,
alijiamini sana sababu ya mafunzo mengi ya kupigana aliyofunzwa huko Demokrasia ya kongo.
Ni kweli anafika Zanzibar na kujaribu kila aliwezalo amuweke mama yake huru lakini kwa mara nyingine anakutana na Rodgers mpiganaji wa kick boxer na

wote kukunja ngumi,
Ngumi aliyorusha Rodgers baada ya kusimama ilipita hewani baada ya Catherine kuinama chini kidogo, akiwa ameinama hakufanya makosa hata kidogo alitupa

ngumi mbili zilizomfikia Rodgers kwenye chembe ya moyo, hapo aliinuka kidogo na kuzungusha teke lililompeleka chini,
hakuwa Catherine lelemama Yule wa miaka iliyopita nyuma alikuwa ni mwanamke jasiri,
ilikua ni lazima amalize alichokianza alimuinua Rodgers na kumtwanga kichwa cha puani,
Rodgers alionesha kuzidiwa, damu zilianza kumvuja puani na midomoni mwake hana nguvu tena yupo chini amelala.
Mzee Mwasha aliyekua juu ya sofa hata yeye alishangazwa na upiganaji wa Catherine hakuamini kama mwanaume anayemuamini yupo chini kachakazwa yupo

hoi bin taaban!
Majambazi wengine wawili walifungua mlango na kumzunguka Catherine, Mzee Mwasha alitabasamu sana na kuona huo ndiyo mwisho wa catherine.
“Mshughulikieni huyo”
Tamko hilo alitoa Mzee Mwasha na kukaa sawa sawia.
Catherine hakukata tamaa aliwatizama watu wawili mwingine mbele yake kisha mwingine akiwa nyuma yake akiwa na kisu,alishusha pumzi ndefu sana na

kukunja ngumi upya kwa ajili ya mpambano mwingine.
Mama yake muda wote alikua pembeni analia hakuwa na mategemeo kuwa kama kuna uhai tena au wangekua huru kutokana na jumba hilo kubwa kulindwa na

watu wengi,hakuwa na uhakika kuwa Catherine angeweza kuwamaliza watu wote wa jumba hilo kubwa na kisha baadaye kuwa huru.

Bado mapambano makali yaliendelea, Catherine ilibidi aweke umakini sana kwa jambazi aliyeshika kisu mkononi mwake, huyo ndiye aliyemuwekea umakini wa

hali ya juu sana kuliko mwingine,
alikiona kisu kinakuja usawa wa tumbo lake,alichofanya ni kurudi nyuma lakini alijikuta yupo chini baada ya mwingine kumpiga mtama,hapo ndipo alipoanza

kushambuliwa tena upya.
Akiwa yupo chini hakutaka kukata tamaa baada ya kukumbuka kile kilichomleta Mama yake na Christopher ilikua ni lazima wawe huru,
alivyokumbuka hayo tu nguvu zilimrudia hapo hapo na kupata nguvu upya,
Ni kweli haikuchukua hata dakika kumi majambazi wote walikua chini wameuwawa baada ya mwanamke huyu jasiri kuvunja shingo zao.
“Hongera sana siku tegemea kama ni mwanamke jasiri kiasi hiko”
Alisema Mzee Mwasha akiwa na bastola mkononi.
“Any way,hiyo haimaanishi mimi kukuacha hai,lazima nikuuwe tu,kachakacha”
Mzee Mwasha alikoki bastola yake na kusimama wima,hakuwa na masihala hata kidogo kwa maneno aliyokuwa anazungumza, aliukunja uso wake kwa

ghadhabu sana,dalili zilionesha kuwa ni lazima awaondoshe duniani watu waliosimama mbele yake, alimuendea mama yake na Catherine kisha kumpiga na

kitako cha bastola
kilichompeleka mpaka chini puuh! Catherine alipotaka kusogea alitulizwa na risasi ya bega.
“Paaaaaa”
Nayeye kudondoka chini akiwa mwenye maumivu mengi sana,taratibu alianza kukata tamaa ya kuishi na kufanya ukombozi.
Alitambaa na kumsogelea Mama yake ili waagane, walikombatiana kama familia kisha kufumba macho yao na milio ya risasi kusikika.

****

“Mama Natu”

“Abee”

“ile kitu yangu iko wapi?”

“kitu ipi hiyo?”

“silaha yangu niliiweka hapa chini ya mto”

“hapana mimi siyuwe iko wapi”
CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“isiwe ikawa anayo Natu”

Usiku kucha Kway alikua na kazi ya kutafuta bastola yake bila mafanikio, hakuelewa ni wapi ameiacha aliingia makabatini bila mafanikio ya aina yoyote yale na

kushindwa kukumbuka ni wapi aliiweka, japo alikumbuka kuwa mara ya mwisho aliiweka chini ya mto hapo seblen lakini hakuwa na uhakika wa kutosha,

usiku huo huo alienda mpaka ofisini kwake na kuanza kuitafuta kila mahali, alielewa nini maana yake alielewa kivyovyote vile ni lazima ingemuweka kwenye

matatizo makubwa endapo itatumika kufanyia uhalifu wa aina yoyote ile.
Walipojaribu kumdadisi Mtoto wao Natu kuhusu hilo hawakuweza kupata jibu kamili.

“Natu mwanangu ile kitu nayoweka hapa kiunoni iko wapi?”
“Ulinikataza nisiguse Dad,itakuwa pale unapoweka”
Natu alijibu.
Hawakulala usingizi wa raha mpaka kunakucha.
“bado haijaonekana?”
Kway alimuuliza mke wake asubuhi kulivyokucha.
“hapana,lakini….”
“nini?”
“namuhisi Yule Catherine pengine atakuwa nayo”
Ni kweli hisia zake zilimtuma kuwa silaha yake anayo Catherine alikumbuka jinsi aliketi pembeni yake, alikumbuka kuwa Mama yake alitekwa nyara ivyo

kivyovyote vile alitaka silaha akafanyie ukombozi,
kabla ya kufanya lolote simu yake ya mkononi iliita.
Alivyoangalia kioo cha simu aligundua kuwa ni Enock.
“Mzee Shikamoo”
“Marahaba habari yako Enock”
“sio nzuri”
“kwanini?”
“Catherine na Mama yake wametekwa nyara”
“unasema?”
“mchumba wangu Catherine ametekwa nyara nimepigiwa simu na Baba yangu ndio yupo nao na ananihitaji niende Zanzibar”
“yaani baba yako ndiyo kawateka?”
“ndio,naomba unisaidie kitu kimoja”
“kitu gani?”
“siwezi kufanya hili jambo mwenyewe tafadhali naomba msaada wako”
“msaada gani?”
“naomba utoe taarifa polisi mimi natangulia”
“sawa lakini…tititi”
Enock tayari alikuwa amechanganyikiwa baada ya kupigiwa simu na Baba yake mzazi aliyekuwa huko kisiwani Zanzibar amejificha, anasifika hivi sasa kwa

ujambazi na uharamia,alikua ni mtu hatari ambaye hashindwi kufanya kitu na hakuna mtu wa aina yoyote ile aliyeweza kumzuia,

Jasho jembamba lilimtoka Enock alishaelewa kuwa mchumba wake huko alipo anateseka na ameshapigwa risasi,ivyo kama mwanaume ni lazima aende

ikiwezekana akamuokoe japo hakua na uhakika kama angefanikiwa,
ilikua ni bora wafe na mchumba wake kwani aliamini kila nafsi itaonja umauti.
“hata nikifa najua nilikua namtetea mchumba wangu,lakini hata ivyo mwisho wa siku tutakufa tu”
Hayo ndiyo aliyowaza Enock akiwa ndani ya boti akielekea huko visiwa vya Zanzibar,aliwaza juu ya maisha yao waliyopitia na mpenzi wake Catherine tangu

mara ya kwanza alipomuona hospitalini miaka mingi iliyopita,
kisha kuanza kumwambia juu ya hisia zake.
Alikumbuka vikwazo vingi walivyopitia mpaka kugombana na Baba yake mzazi Mzee Mwasha na kupigana mpaka risasi kisa mwanamke huyo mrembo

Catherine.

Alikumbuka mpaka watu aliowauwa na kuwadhuru. Ni kweli katika mapenzi yao walipitia mengi.
“Kaka tayari tumefika”
Sauti ya kike nyororo ya dada wa kipemba ndiyo iliyomshtua kutoka katika dimbwi la mawazo,
“okay ahsante!”
Boti tayari ilishatia nanga na Enock taratibu kuanza kushuka hakuwa na mizigo ya aina yoyote ile alienda yeye kama yeye,
baada ya kufika kituo cha basi alipiga simu ili apatiwe maelekezo,
Hapo hakukaa sana watu watatu walimfuata kisha kufanya kama walivyo mfanyia Catherine,
Gari liliondoka akiwa na kitambaa cheusi machoni ili asijue ni wapi anapelekwa.
Mpaka wanafika hakuelewa ni wapi alipo zaidi ya kuona yupo nje ya nyumba kubwa baada ya kitambaa kutolewa usoni mwake.
“Catherine yuko wapi?”
“hauna mamlaka ya kuuliza maswali”
“mnataka nini?”
“msubiri baba yako ndiyo umuulize hayo maswali yako”
Bado Enock hakuwa anaelewa ni wapi Catherine ameweka,
ila katika hali ya ghafla ulisikika mlipuko wa ajabu na kulipua nyumba,
Kwa mbali walianza kusikia mlio wa helikopta, kwa mara ya kwanza hawakuelewa ni kitu gani kinaendelea.
Hapo ndipo waliposhuhudia mtu aliyekua juu ya helkopta mlangoni ameshika mtutu aina ya AK 47 anamwaga risasi, kila mtu aliruka upande wake ili kuokoa

maisha yao.

Bomu lingine aina ya granade la mkono lilirushwa getini na kufanya mlipuko mwingine utokee,
Helkopta ilizidi kuzunguka angani huku ikizidi kuwasambaratisha walinzi wa mzee Mwasha ambao hata wao walionekana kujitetea wakirusha risasi lakini

walizidiwa nguvu,
Baada ya ukimnya kutawala Helikopta ilianza kushuka chini taratibu huku ikizidi kuzungusha mapanga boi yake na kufanya vumbi jingi kuruka.
Walishuka watu watano ndani ya Helkopta na kuingia mpaka ndani moto ulipokua unawaka kisha baadaye kutoka na Catherine aliyekua hana nguvu zake,

alipuliziwa dawa kali za usingizi na kuzirai hapo hapo kisha kuingia naye ndani ya Helkopta,
walivyo hakikisha kila kitu kimeenda sawa, taratibu Helkopta ilianza kuzungusha mapanga boi na kupaa angani huku ikizidi kutokomea.
Kifusi cha mchanga kilichodondoka kutokana na bomu lililorushwa kilimfanya Enock apoteze fahamu zake,
Taratibu aliyafumbua macho yake, cha kwanza kuona ni nyumba iliyokua ndani inateketea na moto,bila kuuliza haraka haraka aliinuka bila kujiuliza mara mbili,
CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
mawazo yake yote yalimtuma kwa Catherine mchumba wake.
“Catheriiineeeee”
Aliita na kujitosa ndani ya moto bila kujali kitu chochote kile,moshi ulikua mkali alijitahidi sana kuyatoa macho yake,alikohoa sana kutokana na kupaliwa na

Moshi uliokua mweusi sana,
Alitafuta huku akimuita Catherine lakini ghafla alimuona Mama Catherine amelala chali kabanwa na mbao,kwa haraka alimfuata na kutoa mbao iliyokua

imem-bana kisha kuuzungusha mkono wake juu ya mabega yake,
ilibidi awahi kumuweka Mama catherine nje kisha yeye arudi ndani ya moto ili kumuokoa Mchumba wake.
Zoezi hilo lilifanikiwa alimuweka mama Catherine nje na yeye kurudi tena ndani ila kabla ya kufika mbali, moto ulizidi kuwa mkali na kufanya mbao za moto

zidondoke,alivyojaribu kutoka nje alishindwa mbao zilikua teyari zimeregea na kumdondokea kichwani.

Kway na mke wake Julia aliyekuwa mjamzito sasa wapo njiani wakiwa na jeshi la polisi, hakutaka kumuacha Mume wake aende peke yake, wapo ndani ya boti

za polisi ziendazo kasi, alishatoa taarifa polisi juu ya Enock kuwa yupo visiwa vya Zanzibar na mchumba wake ametekwa nyara,Jina la Enock halikuwa Ngeni

masikioni mwao walijua sana historia yake ivyo waliungana na kuanza safari, walishajua tayari makazi ya Mzee Mwasha na eneo aliloweka kambi yake,
Na alipokua anajificha, saa tisa ya Alasiri waliwasili Visiwa vya Zanzibar kimnya kimnya bila ya kufanya mawasiliano yoyote yale na jeshi la Zanzibar kama

wafanyavyo siku zote.
Wote walivalia nguo za kiraia, walivyofika tu walitafuta usafiri wa kukodi mpaka ndani ya msitu aliokuwa anajificha Mzee Mwasha wakiwa na mitutu yao

mkononi, lakini ghafla waliona kwa mbali Helkopta ina mwaga risasi, ilibidi wasitishe kwanza zoezi lao,
Hali ilitulia baada ya nusu saa kufika kisha wote kuingia kwa pamoja, wakiwa kwenye miti miti walimuona Enock anaingia ndani ya moto kisha kukaa huko

dakika mbili nzima bila kutoka, hapo ndipo askari wawili shupavu walijitosa ndani ya moto huo mkali ili kumuokoa kijana huyo,
Ni kweli walifanikiwa kumuokoa, alikua amebanwa na Mbao mgongoni, walimuinua na kutoka naye nje ili kumpa huduma ya kwanza,
Baada ya kusikia nafuu jina la kwanza kulitaja lilikuwa ni Catherine.
“Catherine mmempata?”
“hapana hatukufanikiwa”
“wacha nijaribu kuingia tena kumtafuta”
“hapana Enock hatuwezi kukuruhusu”
“haya ni MAISHA yangu hamuwezi kunizuia kwenda kumuokoa mchumba wangu,niacheni niende”
Haikuwa kazi rahisi kumzuia Enock kutaka kuingia ndani ya Moto,

Moyo ulimuuma sana kidonda kilichokua kinaanza kupona moyoni sasa kilitoneshwa na kuanza kutoa damu,
Mikono ilimtetemeka, bado alikua akibishana na polisi mpaka walipomfunga pingu ili asifanye kile anachotaka kukifanya.

Msako wa polisi ulizidi kufanyika wakizunguka nyuma ya nyumba huku wakianza kufanya mawasiliano na jeshi la Zanzibar, kilichotokea wakati huo bado

kilikua Gumzo, Mwanamke waliyeenda kumfuata ili kumuokoa hawakumkuta.
“Afande, nakuomba huku nyuma mara moja ova”
“sawa ova”
Koplo Kato alitoa taarifa kupitia redio upepo baada ya kuona miili mitatu ipo chini.
Haraka haraka walifika, mwili mmoja ulikua wa Inspector Mkumbo huku pembeni yake akiwa amelala na mtoto mdogo akiwa amemlalia huku akiwa anavuja

damu mkononi lakini walikua wanapumua kwa shida sana,
Mwili mwingine walishindwa kuutambua vizuri.
“Huyu ndiye Mwasha tuliyekua tunamtafuta”
Alisema Askari mwingine baada ya kufika eneo hilo la tukio aliloitwa, hawakuelewa ni kitu gani kimetokea.
Haraka haraka walibebwa mpaka kwenye magari ya polisi, huku Mzee Mwasha akiwa amefungwa pingu kwa nyuma,
Enock alipomuona Baba yake hasira zilimkaba na kuyabana meno yake, mapafu yake yalijaa hewa na kufanya kifua chake kipande juu na kushuka kwa hasira,

midomo ilimtetemeka kwa hasira na uchungu.kama angepewa bastola basi pale pale angemmaliza.
“Afande naomba nifungue pingu mimi sio muhalifu”
“subiri kwanza, zitafunguliwa”
“sasa kwanini umenifunga pingu?”
“Afande Juma, Enock yupo sahihi sio muhalifu embu mfungulie”
Hapo ndipo Enock aligeuka kwa nyuma na kufunguliwa pingu.

Ghafla kama umeme alichomoa bastola iliyokua kiunoni mwa askari mmoja wapo kisha kuikoki na kumuelekezea baba yake mzazi huku akiyabana meno yake.
Kila askari aliganda baada ya kumuona Enock kashika bastola,walijua ni lazima atafyatua risasi na kumuondosha Mzee Mwasha Duniani na hawakutaka hilo

litokee.
“Enock weka silaha chini tafadhali”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Aliamuru Polisi.
“hapana siwezi huyu Mzee Lazima nimuuwe siwezi kukubali aishi”
“Weka silaha chini Enock sheria itafuata mkondo wake,huyo atatusaidia kutuambia ni wapi Catherine alipo”
“hapana siwezi Afande”
“Enooooock”
Aliita Kway.
“Weka silaha chini tafadhali wacha jeshi la polisi lifanye kazi yake,punguza jazba”
Taratibu Enock alianza kushusha silaha chini lakini bado alikua mwenye hasira sana,polisi walimfuata na kumnyang’anya bastola aliyoshika.

Mzee Mwasha alipakizwa ndani ya diffenda ya polisi iliyokuwa teyari imefika kisha kuondoka naye. Bado Enock alikua akilitaja jina la Catherine kila dakika

moja ikipita, hakuelewa ni wapi mchumba wake alipo,aliona maisha ni bure kabisa bila ya kuwa na Catherine karibu yake.
“Enock”
Aliita mama Catherine.
“Naam Mama”
“Catherine amechukuliwa na watu ambao walikuja na helkopta”
“ilikuaje?”
“nashindwa kuelewa maana Mara ya mwisho nilikua naye Mimi na Christopher kisha tukasikia mlipuko mkubwa hapo ndipo sikujua kinachoendelea”
“zitakuwa ni njama za huyu mzee atataja tu”
Siku hiyo hiyo usiku walimsafirisha Mzee Mwasha mpaka mkoani Dar es salaam, baada ya kufika kivukoni walipanda magari mengine ya polisi yaliyokuwa

teyari yamefika.
Kila polisi alikuwa ni mwenye furaha sana baada ya kumtia nguvuni Mzee huyo hatari sana.
Ni kweli alisumbua sana jeshi la polisi hawakulala usiku kucha,Wenzao wengi walipoteza maisha,kila mtu alikuwa na hasira sana na mzee huyu.
Walimfikisha kituo kikubwa cha polisi oysterbay ili kusubiri sheria ifate mkondo wake.
Enock alizidi kuwa sumbua polisi akitaka kumuhoji baba yake ni wapi Catherine alipo, kila kukicha ilikua ni lazima aripoti oysterbay polisi.
“Dad mimi ni mwanao, naomba nirudi katika hali ya furaha,nini kilikupata lakini,haukuwa hivi, naomba nitajie ni wapi mchumba wangu alipo, sawa sikatai

unamchukia,hata kama amekufa niambie ili nione japo mwili wake”
Mzee Mwasha hakujibu kitu chochote na kugeukia upande wa pili hakutaka kusema lolote lile,

Enock alitafsiri hiyo kama dharau lakini hakuwa na namna nyingine ya kufanya, kwa upole alisimama na kutoka nje alishindwa ni wapi aanzie.

Hakuelewa ni njia gani atumie ili aweze kujua ni wapi mchumba wake alipo, habari za kuchukuliwa na Helkopta ndizo zilimuumiza sana mtima wake.
Ki ukweli alijiona ni mwanaume mwenye mkosi katika mapenzi, tangu alipoanza kuwa na mapenzi na mwanamke huyo miaka iliyopita,
vitu vingi sana walipitia na mateso mengi,lakini hiyo haikumfanya akate tamaa ya kuwa naye na alishaapia ndiye atakaye kuja kumzalia watoto wawe mke na

mume hapo baadaye.

Mama Catherine,Enock,Anderson Peter pamoja na Mtoto wa Becker wote waliunganisha nguvu zao ili kumtafuta Catherine kila kona ya jiji,
wakibandika picha zake kila mkoa na kutoa taarifa mbali mbali vituo vya Redio na tv.
Becker t.v kituo kikubwa kinachovuma ndani na nje ya Africa kwa ujumla kilichomilikiwa na Rafiki yake ndiko kilikuwa kinarusha matangazo juu ya upotevu

wa Mwanamke Catherine kila kukicha.
“Habari kwa ufupi,Mwanamke mwenye umri wa miaka ishirini na nne anatafutwa, anaitwa Catherine Ramsey Kidhirwa kwa yoyote atakaye muona basi atoe

taarifa kituo cha polisi kilichokua karibu yako”
Habari hizo zilidumu wiki nzima bila mafanikio yoyote yale,
Enock alitumia pesa nyingi sana kusafiri mikoa mbali mbali kumtafuta Mchumba wake.
Alipigiwa simu tofauti nyingi za pole lakini hazikuwa na maana kwake, akili yake ilishachoka sasa kuzunguka, lakini hiyo haikumfanya akate tamaa, siku hiyo

hiyo aliingia mpaka ofisi za Becker fm Msasani,na kuomba aongee machache studio!.
“Catherine mpenzi wangu, ni wiki tatu sasa zimepita nakutafuta kila mkoa, sijui ulipo mchumba wangu,nimesha hangaika sana, bila wewe siwezi, kama

unanisikia tafadhali naomba urudi nyumbani,..nakup…”
Enock alishindwa kumalizia maneno anayoongea na kuanza kububujikwa na machozi hapo hapo, moyo ulimuuma sana hakujali kuwa yupo hewani na

Watanzania wanamsikiliza kupitia redioni.
Becker ilibidi amuinue rafiki yake kisha waende nje, Leo hii Enock analia kisa mapenzi kitu ambacho hakutegemea kuja kukifanya katika maisha yake.
“Kaka usilie,Catherine tutampata nitakuwa nawewe bega kwa bega mpaka atakapo patikana”
“Becker, siweziii.. siweezii”
Alizidi kulia huku akifikicha pua zake.
Picha mbali mbali zilipita ndani ya ubongo wake wakiwa na Catherine na kumfanya azidi kulia kila kukicha,
Mawazo yalikula kabisa mwili wake wote kutokana na Mawazo aliyokuwa nayo.
***CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“tuku tuku tuku tuku”
Helkopta ilizidi kusonga mbele ikizidi kukata mawingu, Catherine hakuwa na fahamu zake baada ya kupuliziwa madawa makali sana puani na kuchukuliwa na

usingizi mkali.

Baada ya Helkopta kubwa kutoka visiwa vya Zanzibar ilitua visiwa vya chakechake hapo walimshusha Catherine na kumuingiza ndani ya boti ndogo.
Baada ya zoezi hilo kukamilika boti ilitoka kasi mpaka ilivyofika kati kati ya bahari hiyo ya Hindi na kusimama,
walivyo fanya mawasiliano ulisikika mlio wa ndege ndogo ya majini kisha kutua juu ya maji, hapo walimpakia Catherine ndani ya ndege, ilionekana mipango

hiyo ilipangwa na watu makini sana.
Kwa mbali sana Catherine alihisi kelele za Ndege alivyoyafumbua macho yake alikutana na sura aliyoifahamu na mara ya mwisho alipanda naye ndege

walivyokua wakitoka nchini Kongo.

Sura ya mwarabu huyu mwenye ndevu nyingi kama Osama bin Laden aliikumbuka sana na kukumbuka ndoto aliyoota.
Alishapata jibu tayari la swali lake kuwa ametekwa nyara.
Alivuta kumbu kumbu nyuma kuwa mara ya mwisho alikuwa yupo ndani ya jumba la Mzee Mwasha na Mama yake pamoja na mdogo wake Christopher,
Bado alishindwa kuelewa watu hao ni akina nani mpaka alipoiona ngozi nyeupe ya kizungu,hakuweza kumsahahu Carl Martin.
“Well well well well Catherine nice to meet you again,I am amprest(Catherine nimefurahi kukutana nawewe tena,nimevutiwa)”
Aliongea Carl Martin kwa nyodo huku akimshika shika Catherine mashavu yake.
Hata angewekewa kisu shingoni asingekubali kwenda nchini Germany ili akachezeshwe filamu za ngono.
Alishaelewa nini maana ya Carl Martin kumtafuta,
ubongo wake ulikusanya vitu haraka haraka na kukumbuka kuwa ana kisu cha kukunja kwenye kiatu chake,
alichotakiwa kufanya ni kutumia akili nyingi na umakini ili ajinusuru na watu hawa, na hayo ndiyo yalikua mahesabu yake kichwani.

Hapo hapo alianza kuwahesabu walinzi waliopo ndani ya ndege,
baada ya kujua idadi yao alianza kufikiria jinsi ya kutoka na kujitupa ndani ya maji.
Ndege ilianza kutoa kasi sana kisha taratibu kuanza kupaa angani baada ya kila mmoja kukaa kwenye kiti chake, kama umeme Catherine aliruka mlangoni akiwa

na kisu mkononi mwake na kumchoma nacho mlinzi aliyekua amezubaa anavuta sigara,
Kisha kufungua mlango haraka haraka na kujitupa nje ‘chubwi’ ndani ya maji….

“Halloo”
“Yes Halloo”
“Naongea na Mr.Enock?”
“ndiyo mimi,sijui nani Mwenzangu?”
“Naitwa Rama!,niilichukua namba yako jana Becker t.v nina habari nzuri,nimemuona Catherine sehemu”
“Unasema, upo wapi sasa hivi,niambie ulipo, ulimuona wapi?”
“Huku Dodoma Chamwino”
“Naweza nikaja huko?”
“sawa njoo”
Moyo wa Enock ulilia pah asubuhi hiyo.
Baada ya kusikia habari hizo kutoka kwa msamalia mwema aliyedai kuwa kamuona Mchumba wake Catherine huko Dodoma Chamwino,
hakutaka kujifikiria mara mbili hata kidogo, alichungulia gari yake kama ina mafuta ya kutosha na kuipiga funguo kwa safari moja tu kuelekea Dodoma kijiji cha Chamwino kwenda kumchukua Mchumba wake ambaye alimtafuta kwa takribani miezi minne bila dalili na mafanikio ya aina yoyote ile,
hakukata tamaa hata kidogo na sasa alikua yupo njiani anakimbiza gari kwa spidi sana kama mwendawazimu akitamani afike haraka ili akamuone tena mchumba wake,
wakati mwingine alitamani gari yake ipae ili aweze kufika dakika hiyo hiyo lakini hilo halikuwezekana hata kidogo,
njiani aliwaza mengi sana,hususani swala la yeye kufunga ndoa kubwa na Catherine hata kesho yake akimpata.
Jioni ya saa kumi na moja aliwasili Mkoani Dodoma kisha kupiga simu kwa Ramadhani aliyedai kuwa alimuona Mchumba wake,
hakutaka kupoteza muda wowote ule,maelekezo aliyopewa yalimfikisha mpaka kijiji cha Chamwino na kuonana na Ramadhani!.
“Jana nili muona maeneo ya huku twende nikupeleke”
“sawa”
Wote waliongozana mguu kwa mguu mpaka kwenye nyumba ndogo ya udongo iliyotengenezwa kwa mfumo wa nyasi zilizokauka.
Mwanamke aliyetoka ndani ya kijumba hiko ni kweli alifanana na Catherine lakini hakuwa yeye,
hapo hapo alinyong’onyea na kukaa chini akiwa amechoka.
“Kaka nipatie basi ile pesa uliyosema, Catherine huyo hapo”
Alisema Ramadhani.
Enock hakuwa na kitu chochote cha kuongea zaidi ya kutoa noti mbili za shilingi elfu kumi na kumkabidhi kisha kuondoka zake taratibu.
Alikaa Dodoma takribani wiki nzima akizidi kumuulizia Mchumba wake bila kuona dalili yoyote ya kumpata alimtafuta kwa hali na Mali,
wiki ya pili nayo ilikuwa ivyo ivyo mpaka inafika wiki ya tatu alikuwa yupo hoi bin taaban! Amechoka sana.
CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Siku hiyo akiwa ametoka bafuni kuoga anajiandaa ili kurudi mkoani Dar es salaam alikuta ujumbe wa video kwenye simu yake kupitia mtandao wa Watsap kisha kuufungua, hakuamini alichokiona, hakuamini baada ya kumuona Catherine yupo uchi wa mnyama tena anafanya mapenzi na wanaume wawili kwa mpigo,
wakati mwingine alidhani anaota yupo Ndotoni na angeshtuka,mambo aliyoyaona yalikua yana ukweli,alijikuta anakaa juu ya kitanda na kuitizama tena video hiyo kwa mara nyingi.
Alivyojaribu kuipiga namba iliyotuma video ya ngono haikuwa hewani, Moyo ulimwenda mbio sana, wakati mwingine alidhani wenda sio Catherine sababu Duniani watu wawili wawili,
Lakini alivyoivuta picha karibu sana kiunoni aliona kidoti cheusi hiyo ilimaanisha ni kweli alikuwa Catherine mchumba wake.

***
“Griii Griiiiiiii grriiiiiii”
Risasi zilirushwa kutokea juu ya ndege ndogo zikipigwa chini ya maji alipokuwa ametumbukia Catherine anaogelea kisha baadaye kuzamisha kichwa chake ndani ya maji, bado waliendelea kurusha risasi zao.
“Do not shoot,I said do not shoot, I need her alive, she is an asset”(msipige risasi,nasema msipige risasi,namuhitaji akiwa mzima,huyo ni mali”).
Kauli hiyo ilitoka kinywani mwa Carl Martins akifoka.
Ni kweli alimuhitaji Catherine ili kutengeneza pesa nyingi sana alishaini mikataba juu ya kumchezesha mwanamke huyo filamu za ngono,
kumuuwa Catherine ilikuwa ni sawa na kutumbukiza gunia la dhahabu ndani ya chemba la choo, na hakutaka hilo litokee.

Hapo ndipo alipoamuru ndege igeuzwe na kurudi nyuma,wazungu wawili walijitosa kutokea juu ya ndege mpaka ndani ya maji ili kumchukua Catherine,
kwani walipewa maagizo kuwa anahitajika akiwa mzima kabisa.
Maumivu ya Bega yaliyosababishwa na risasi aliyopigwa na Mzee Mwasha wakiwa huko visiwa vya Zanzibar akitaka kumuokoa mama yake ndiyo iliyomfanya ashindwe kuogelea vizuri,
Maji ya bahari yaliyokua na chumvi ndiyo yaliyomfanya asikie maumivu mengi sana,
licha ya yote hayo kutokea hakutaka kukata tamaa alizidi kupiga mbizi akiyakata maji huku akitingisha miguu yake, aliibua kichwa chake juu ili kuvuta pumzi kisha kukizamisha tena ndani ya maji ili asonge mbele.

Ilikuwa bora afe kuliko kupelekwa Nchini Germany akachezeshwe filamu za ngono na kuuzwa Dunia nzima,
hakutaka hiko kitu kitokee tena kwa mara nyingine hata kama angepewa kiasi cha bilioni mia mbili, aliuthamini sana mwili wake.
Kitendo cha kuibua kichwa chake juu aliona watu wawili wanaogelea tena wanakuja kwa kasi nyuma yake huku juu yake bado ndege ya Carl Martins ikiwa inamfuatilia,
hakufika mbali tayari alikuwa amekamatwa, alivyotaka kurusha ngumi alishindwa.

Alipojaribu kujitetea hakuweza baada ya kichwa chake kuchukuliwa na kuingizwa ndani ya maji, aliinuliwa na kutumbukizwa tena, zoezi hilo lilidumu mpaka alipoishiwa pumzi zake na kulegea kabisa na ndiyo hayo yalikua mahesabu yao.
Baadaye kidogo ndege ilishuka kisha kuchukuliwa na kuingizwa ndani,
walimfunga kamba mikononi na kumkalisha juu ya kiti.
Ndege ilitembea kwa kasi sana juu ya bahari ya Hindi kisha kupaa angani wakiwa tayari wapo na catherine mikononi mwao!.

Ndege ilizidi kusonga mbele ikiwa angani inakata mawingu,kwa mbali sana Catherine fahamu zake zilianza kumrudia taratibu,
lakini hakutaka kuyafumbua macho yake kwa haraka,bado hakutaka kukubali kushindwa hata kidogo,
alifumbua taratibu jicho lake moja la kulia na kumuona Carl Martins amelala na baadhi ya walinzi wanakunywa pombe kali, aliwahesabu na kugundua wapo watano kujumuisha na rubani wa ndege,
usiku ulikua teyari umeingia,mahesabu yake yalikua moja kwa moja kwa rubani wa ndege, ilikua ni lazima afanye kitu ili kuikwamisha safari hiyo ya Germany,
Taratibu sana alianza kucheza na kamba za katani alizofungwa mkononi kwa umakini sana, hazikupita hata dakika tano alikuwa keshazifungua na mikono yake kuwa huru na kuanza kuhesabu kimoyo moyo.
“Moja, Mbili, ta…”
Kama umeme alichomoka kwenye kiti mpaka kwa rubani aliyekua yupo bize haelewi chochote kisha kumvaa mpaka kwenye mitambo, alikamata kitu kilichofanana na gia na kuanza kukizungusha, kila alipokizungusha ndipo ndege ilipokua inapoteza muelekeo wake,
kila mtu alichanganyikiwa baada ya kuona ndege inaenda kombo, Catherine alizidi kubonyeza bonyeza vitu asivyovijua na ndege kuanza kurudi chini kwa kasi sana, hapo ndipo aliposali sala yake ya mwisho kwani chini kulikua kuna msitu uliokuwa na miti mingi sana,
walipojaribu kumtoa walishindwa haikuchukua hata dakika saba ndege ilianza kujipiga juu ya miti mingi, kila mtu alijigonga gonga lakini kwa Catherine alijishika kwenye kiti kwa nguvu zake zote mpaka ndege ilipogota juu ya tawi la mti mkubwa,CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Damu alizokua akivuja mkononi ndizo zilifanya ilegeze mikono yake na kuifanya iteleze,
alishindwa tena kujishikilia na kuanza taratibu kwenda chini, alijigonga kwenye kioo na kutoka nje, hapo alijipiga piga na miti na kuporomoka mpaka kwenye matawi puu chini,
Alihisi maumivu mengi sana kwenye paja lake na mgongoni,
alivyojiangalia vizuri aliona mti mkubwa umezama kwenye nyama,damu nyingi zilimtoka alihisi maumivu makali mno,
Taratibu alianza kujiburuza kama nyoka mpaka chini ya mti na kukaa huku akilia machozi ya uchungu,
hakuelewa ni wapi alipo zaidi ya kusikia sauti za wanyama pori tena wakali kama simba na Chui.

Mambo yanayomtokea katika maisha yake hakuelewa mkosi huo alipewa na mtu gani,
aliuangalia mguu wake jinsi mti ulivyoingia na nyama zake kutokeza nje,licha ya yote maumivu ilibidi asonge mbele na kuiokoa nafsi yake na siyo kukaa chini ya mti na pengine kuwa kitowewo cha wanyama.
Alivua shati lake la juu kisha kulichana kidogo,
Alichukua kipande cha mti na kukiweka mdomoni ili asiweze kuung’ata ulimi wake kwa jambo analoenda kulifanya.

Alivuta pumzi ndefu na kuzishusha kisha kuushika mti mkubwa uliozama juu ya paja lake, kwa nguvu zake zote aliuvuta mpaka ulipotoka na kufanya damu ziruke mfululizo.
“Aaaah!Mungu weeee”
Maumivu aliyoyasikia hakika hayakuweza kuelezeka hata kidogo, lakini ilibidi ajikaze, alichukua kipande cha shati na kukifunga kidonda kilichokuwa kinavuja damu nyingi ili kuzuia isiendelee kuvuja.

Alisimama kwa tabu sana na kuanza kutembea,hakuelewa ni wapi anaelekea Magharibi au Mashariki,kaskazini au Kusini.
Ghafla alihisi parakacha za mtu zinakuja nyuma yake, alivyogeuka alimuona mtu anavuja damu kichwani huku mkononi akiwa na bastola, alikua ni mmoja wa watu wa Carl Martins.
“Stay where you are bitch,you make a step I shoot you(hapo hapo ulipo Malaya,ukipiga hatua yoyote nakupiga risasi”)
Catherine alishakua tena chini ya ulinzi akiwa amewekewa bastola,
ilibidi asalimu amri na kuanza kuongozana wote huku wakisonga mbele akiwa anachechemea,
bado vita ilikua haijaisha,lakini alipofika mbele baada ya kupiga hatua chache alisimama na kumgeukia Mwanaume aliyeshika bastola.
“Do you want to kill me?”(unahitaji kuniua)
“if you wont cooperate, I will kill you”(kama hautoonesha ushirikiano,nitakuua)
“No!,you are lying if you wanted to kill me, I would be dead already,go ahead and pull the trigga, I said go ahead and pull the trigga(Hapana,sio kweli,kama ungehitaji kuniua,ningekuwa nishakufa tayari,fanya ivyo nipige risasi,nasema nipige risasi”)
“Move,”(songa)
“No I can’.t(hapana siwezi).
Catherine alishachezwa na machale kuwa alihitajika akiwa hai ivyo mtu aliyemuwekea bastola hakuwa na uwezo wa kumdhuru, alikua ni kama nyoka asiyekuwa na meno.
Alizidi kufoka kwa sauti ya juu huku akiyabana meno yake wakianza kulumbana, alimsogelea mpaka karibu ya bastola na kutegesha kichwa chake ili apigwe risasi.
“Pull the triga”
Alifoka Catherine kwa ujasiri na kurudisha kichwa chake nyuma kwa nguvu na kukirudisha kwa kasi mpaka juu ya pua za jambazi huyu aliyekua mbele yake na bastola.

Aliyumba yumba kutokana na maumivu makali mpaka chini chali hapo hapo.
Catherine hakufanya makosa alichukua bastola na kumfyatua na risasi ya utosi,
Alishusha pumzi ndefu baada ya kuiweka bastola kiunoni vizuri akielewa kuwa ndiyo itakayo kuwa msaada kwake huko mbeleni na kuanza kusonga mbele kwa tabu sana ndani ya msitu huo mnene ambapo kulikua kuna giza nene,
Nguvu zilimuishia na kukaa chini tena ya mti mkubwa na usingizi mzito kumchukua,
Kilichomshtua asubuhi ni muungurumo wa simba kwa mbali,
alizidi kuyatoa macho yake na kutega sikio kwani sauti hiyo ya mnyama huyu mkali ambaye akiunguruma lazima wanyama wote wakimbie ilikua karibu sana,
Hakuamini baada ya kugeuza shingo yake nyuma na kumuona simba mkubwa akiwa anaunguruma, dalili zilionesha kuwa alikua na njaa sana,

Taratibu alianza kumsogelea, Catherine alijaribu kujiburuza kurudi nyuma kisha kutoa bastola iliyokua kiunoni ili kumuuwa simba aliyekua anakuja kwa kasi mbele yake.
“karakacha karakacha”
Mlio wa bastola ulioashiria kuwa hakuna risasi ndani ya chemba baada ya kutaka kufyatua risasi ulimfanya Catherine azidi kuingiwa na hofu,CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
hakua na matumaini tena ya kupona simba alikua teyari mita chache na kuinua miguu yake ya mbele kisha kumvaa Catherine aliyekua chini amelala

Hakuwa anawaza kitu kingine zaidi ya kusubiri kifo chake alichojihesabia kuwa ataliwa na simba huyo mkali ambaye teyari ameupanua mdomo wake akijaribu kuingiza meno yake ndani ya shingo ya Catherine,
Japokua alikua hana nguvu za kutosha lakini ilimbidi ajaribu kujitetea,
aliyakumbuka vizuri mafunzo ya Baba Abushiri jinsi ya kupambana na wanyama wakali wa porini kipindi yupo Demokrasia ya Kongo baaada ya kunusurika na majangili waliodhani kuwa yeye ni Raia wa Rwanda,

Bado alipiga moyo konde na kurudisha fikra zake nyuma haraka haraka kama umeme na kumkamata simba shingo kisha kumkumbatia kwa nguvu zake zote,na kuanza kubiringika naye, alishaelewa kuwa kitendo cha kumuachia mnyama huyu Mkali ndiyo utakuwa mwisho wa maisha yake kwani alishapandwa na hasira na kuanza kuunguruma kwa sauti sana,

Kucha alizokuwa anarusha simba zilimfanya Catherine apate majeraha mengi na damu kumvuja mwilini kama maji, alihisi maumivu makali sana lakini hakutaka kuiachia shingo ya simba huyo.
Licha ya kujitahidi sana alionekana kuzidiwa nguvu na kuchoka kabisa, hapo ndipo aliposali sala yake ya mwisho na kudondoka chini,
Aliyafumba macho yake baada ya kumuona Mnyama huyo anapanua tena midomo yake na kuiweka usawa wa mbavu zake.
“paa paaaa”
Kilichosikika hapo ilikua ni milio ya gobole hakuelewa ilisababishwa na nini, Damu zilitapakaa alishindwa kumtoa Simba aliyekuwa juu yake amekufa tayari baada ya risasi mbili kupenya ndani ya tumbo lake, Watu wanne walitokea mbio mbio na kumbeba simba huyo kisha harakaharaka kuanza kumchuna ngozi yake,
Walimtizama Catherine na kuanza kuongea Lugha isiyoeleweka.
Catherine hakuwa na nguvu tena, nguvu zake zote alizimaliza kwa Simba aliyekuwa akipambana naye dakika mbili zilizopita,
Alikua akihema kwa shida alichokuwa akihitaji kwa wakati huo sio kitu kingine bali ni msaada wa kutolewa katika pori hilo lenye wanyama wakali.
“He…lp me”(nisaidie)
Alisema Catherine kwa tabu sana.
Sauti ya jitu moja jeusi lilisikika likiongea na wenzake kwa lugha isiyoeleweka kisha kumchukua Catherine na kumbeba mpaka ndani ya gari huku wakiwa wameshika ngozi ya simba,
gari lilijaa pembe za Tembo na Ngozi za simba kwa harakaharaka Catherine alishaelewa watu hao ni majangili wanaoiba wanyama, lakini hakutaka kufanya lolote alichohitaji yeye ni kujikwamua na kutoka kabisa msituni.
Landrover iliyokuwa imelemewa na mizigo ilianza kusogea mwendo wa kinyonga likipita pori kwa pori,
walisita kidogo baada ya kusikia muungurumo wa gari, haraka waliingiza gari porini ili kujificha walivyohakikisha kuna usalama waliendelea na safari kisha ilivyofika mchana waliegesha gari pembeni ili wasubiri usiku uingie na wasonge mbele.
Kweli walifanikiwa kujificha mpaka giza lilipoingia na kuanza kutembea porini bila ya kuwasha taa za gari lao kwa takribani lisaa lizima baadaye!.
Ghafla walisikia tena muungurumo wa magari unakuja nyuma yao huku likimulika taa zake, walivyotaka kukimbia waliwekwa chini ya ulinzi na jeshi linalolinda msitu.
Kisha kuwatoa wote nje ya gari.
Catherine alitetetemeka sana kuliko maelezo yaliyojitosheleza aliogopa sana, walimchukua na kumlaza chini chali akiwa na kamba zake,
dalili zilionesha kuwa walidhani ni jangili vile vile.
Jeshi la kulinda misitu halikuwa na masihala hata kidogo walishakoki mitutu yao na kuanza kuwamiminia watu hao waliokuwa majangili wanaiba wanyama pori.
walimfuata Catherine na kumuwekea bastola utosini ili wamuuwe hapo hapo.
“Msimuuwe”
Alitoa kauli hiyo mkuu wao wa kikosi kwa Lugha ya kwao.
“Kwanini?”
“Nimesema msimuuwe”
“sasa tumfanye nini?”
“tuondoke naye”
Hiyo ndiyo ilikua ponea ya Catherine ambapo tayari alidhani ataenda kufa dakika mbili baadaye,
Walimvuta mpaka ndani ya gari kisha kuondoka naye.

Safari ilidumu kwa masaa mawili tangu walipokuwa ndani ya msitu huo mpaka kwenye kambi ya maaskari hao waliokuwa muda wote wanamtizama Catherine kwa macho ya Matamanio.
Walifika kambini na kumshusha mpaka ndani ya chumba kidogo ili wampe huduma ya kwanza kwani alikuwa na majeraha mengi sana.
Walianza kukitibu kidonda chake cha mguuni kwanza kisha baadaye kumpaka dawa mgongoni mwake uliokuwa na majeraha ya kucha za Simba,
baada ya hapo walimpatia chakula ale kisha baadaye kumpa Maji anywe.
“Do you speak English?”(unaongea kiingereza)
Aliuliza muuguzi wa kike aliyekua anamtibu majeraha yake.
“Yes I do(ndio ninaongea)
“My name is Caroline, what is you are name(jina langu ni Caroline,unaitwa nani?)
“Catherine”
“Where do you come from?”(unatokea wapi)
“Tanzania”
“Ohh Tanzania”
Catherine alijibu kila swali aliloulizwa lakini ghafla alitokea Askari na kumtandika kofi zito muuguzi huyo kisha kumsukumiza pembeni na kuanza kuongea lugha ambayo Catherine hakuielewa hata kidogo!.
Lakini kwa haraka haraka alielewa kuna kosa kubwa alilifanya.

Catherine Alichukuliwa na kufungiwa ndani ya chumba kidogo kilichofanana na gereza, humo alikua akipewa chakula na maji lakini alinyimwa kitu kimoja tu uhuru,
lakini bado mpaka siku hiyo hakuelewa ni kwanini yupo mahali hapo na ni kitu gani wanahitaji kutoka kwake. CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Akiwa ndani ya chumba kidogo alifikiria mambo mengi sana hususani juu ya maisha yake,ni kweli alipitia mambo mengi sana yenye historia hapo nyuma kilichomuuma zaidi ni Enock mchumba wake, moyo ulimuuma sana alipomkumbuka Mama yake mzazi pamoja na Mdogo wake Christopher ambao alifunga safari ya kwenda kuwakomboa huko visiwa vya Zanzibar matokeo yake kujikuta mahali asipopajua.
Siku zilizidi kusonga bado akiwa mateka lakini Chakula na Vinywaji kila kitu alipewa.
“Heii,Heiii please help Me(tafadhali naomba msaada)”
Alisema Catherine baada ya muuguzi aliyemsaidia kipindi cha Nyuma kupita nje.
Licha ya kuita Muuguzi huyo alimtizama na kuondoka zake dalili zilionesha kuwa alikuwa akihofia kitu na kuogopa kumsaidia Catherine ambaye alikua akiomba msaada kwake.
“Please don’t leave me(tafadhali usiniache)
“No I can’t(hapana siwezi)
“Please I need help, I know you can(tafadhali naomba msaada najua unaweza)
Catherine alizidi kupiga kelele za msaada bila mafanikio ya aina yoyote ile.

Baadaye walisikia muungurumo wa magari nje,kisha kuingia wanaume nane walioshiba na mwanaume mmoja aliyewekwa mateka, alichukuliwa na kupigwa risasi hapo hapo kisha Catherine kufunguliwa ndani ya chumba kidogo alichofungiwa kilichofanana na selo kisha kuwekewa bastola kichwani tayari kwa kuuliwa.
“Embu subiri kwanza msimuuwe”
Alisema Mkuu wao akiongea kwa Lugha isiyoeleweka.
“kwanini mkuu hapaswi kuishi huyu Binti sasa aishi ili iweje?”
“Nasema asiuliwe kuwa mwelewa, hivi tangu lini umeanza kukiuka amri ninayo toa mimi?,hiko kiburi umekitoa wapi?”
“Samahani Mkuu sikuwa na nia mbaya kuuliza”
“haya nasema tena asiuliwe mleteni hapa”
Majasho yalimtoka Catherine sala ya Mwisho aliyokuwa akisali kwa Mungu wake ili atende miujiza hakika ilifanya kazi kabisa, japokuwa hakuelewa ni kitu gani walikuwa wakizungumza kwa wakati huo!.
Alizidi kumuomba Mungu wake aliye juu mbinguni atende miujiza sababu hakuwa na nguvu nyingine ya kujitetea.
Alichukuliwa na kupakiwa ndani ya gari mpaka walipofika umbali wa kilomita tisa mbele, kisha kuegesha gari pembeni ambapo Catherine alishushwa na kuingizwa chumbani.
Alikitizama chumba hiko kilivyokuwa kidogo chenye kitanda kidogo juu yake, hakuelewa ni kitu gani kinafuata, ilivyofika katikati ya Usiku mtu aliyemleta mahali hapo alitokea na kuanza kuvua nguo zake mwilini mwake.
Kisha kuufunga mlango na kumuendea Catherine aliyekua amekaa kitandani,
Hisia kali za kufanya Ngono na Catherine zilimpanda, baadhi ya maungo yake ya mwili yalisimama baada ya kumuona mwanamke huyu mzuri aliyekamilika kila idara, udenda ulimtoka na kuanza kumvuta asogee upande wake,
Catherine alivyotaka kupiga kelele alipigwa kofi zito na kumfanya atulie kimnya.
“Do you want to fu*** me?”
Aliuliza Catherine kwa sauti ya chini huku akitoa nguo zake za juu na kumfanya mwanaume huyo aliyekuwa na uchu asiweze kutumia nguvu za aina yoyote ile.
Udhaifu wa mwanaume siku zote ni mwanamke Catherine alilijua hilo, ilimbidi atumie akili ya ziadi ili aweze kujinasua katika mdomo wa mamba,
Alimvuta Mwanaume huyo kitandani kisha kuanza kumshika kifua chake akitumia mikono yake laini kabisa.
Mwanaume aliyeitwa Ngodu alikuwa hoi yupo mbali sana kihisia ameyafumba macho yake.
Catherine alimvua mkanda kisha suruali kufuata alivyohakikisha kalegea kabisa alichukua mkanda na kuuzungusha shingoni kwake kwa haraka huku akiwa ameikaza mikono yake.
Lakini alijikuta yupo chini baada ya Ngodu kumtupa pembeni,
alikua ni mwenye misuli na nguvu nyingi alimfuata Catherine kwa hasira na kumuinua na kumzaba kofi zito, Catherine alidondoka chini na kujibamiza kwenye stuli kisha kutulia tuli.
Mwanaume Ngodu mwenye misuli mikononi alipiga hatua mpaka alipolala Catherine lakini kabla ya kumfikia, Catherine aliinuka ghafla na kuishika miguu yake miwili na kuivuta na kumfanya adondoke na kubamiza utosi wake nyuma ya kitanda juu ya mbao,
hapo Catherine hakutaka kufanya makosa.
Alimfuata na kumkaba shingo yake na kuivunja hapo hapo,
alichungulia nje dirishani ili kujua usalama.

Aliinama kidogo na kuangalia ndani ya suruali ya Mwanaume maiti aliyekuwa chini hana kauli huku akivaa nguo zake, na kuchukua simu kisha kuanza kubonyeza bonyeza akijaribu kuikumbuka namba ya Enock mchumba wake ili amwambie kuwa yupo salama salmin,
lakini hakuelewa endapo akiulizwa ni wapi alipo atajibu nini.
Alibonyeza bonyeza namba kisha kuweka simu masikioni.
“Halloo Enock mimi Catherine”
Alisema Catherine baada ya simu kupokelewa upande wa pili.
“Catherine yupi?”
Moyo ulimwenda sana kasi Catherine na kuanza kutetemeka hakuamini alichosikia upande wa pili wa simu kuwa ni sauti ya mwanamke tena anaongea kwa kujiamini,wakati mwingine alidhani wenda amekosea namba,lakini namba ilikua sahihi baada ya kutoa simu masikioni mwake na kugundua ilikuwa ndiyo namba za Enock mchumba wake..
“Weeeka biaaa nyingineeee hapo,usinitumbulie macho binti”
“Pesa kwanza kaka”
“pumbaaaavu wewe,Mimi huwa nakunywa kwa biliii hapa niangalie vizuri kwa umakini,”
“Nishakuangalia!”
“Basi!.. Then Go and add me Another bottle now now!, before I call your boss, I know you not gonna like it(sasa nenda na uniongeze chupa moja sasa,kabla sijampigia bosi wako,najua hutopenda)
“Mhh!”
Dada huyo mhudumu aliguna kisha kuondoka zake,Kwa haraka haraka kilikua ni kiingereza cha kimarekani ndiko kilichomchanganya akili yake,
alimuendea mpaka meneja wake na kumueleza kila kitu.
“Umesema kuwa hataki kulipa?”
Aliuliza Meneja aliyeitwa Massatu.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Ndio hataki kulipa, na ana deni la elfu themanini”
“yuko wapi?”
“yupo kule”
“subiri nikamuoneshe adabu”
Meneja Masatu alifunga mahesabu kisha kumuendea Mteja aliyeambiwa kuwa ni mbishi kulipa deni la vinywaji alivyokunywa.
“oyaa amka amka!”
“Mmeleta Bia?”
Kitendo cha mwanaume huyo mlevi kuinua kichwa chake kilimfanya Massatu ashtuke sana, hakutegemea kuwa aliyekuwa akilewa pombe ni Enock Mwasha.

Alimfahamu vizuri sana tajiri huyo sababu mke wake ni miongoni mwa wafanyakazi wake katika kampuni ya Nissani, hakuelewa ni kitu gani kimemkumba mwanaume huyo mwenye heshima zake,
siku zote alimuheshimu kwa sababu tu ya roho yake nzuri ya kuwasaidia watu, hakuwa na ubaguzi wowote wa rangi, uwe mweusi au mweupe mfupi au Mrefu!

Kwa kumuangalia haraka haraka Massatu aligundua kuwa Enock ana tatizo kubwa tena ana hitaji msaada wa kimawazo na sio pesa sababu pesa alikuwa nazo pengine ni nyingi hata punda asiweze kuzibeba.
“Mr. Enock”
Aliita Massatu na kumfanya Enock amtizame na kucheua.
“Niletee bia kwanza na Red wine kishaaa tuzungumze, I have problems my friend, a lot of problems, wewee ni Masaaaatu kama sijakosea Mume wa Blandina, Yes yes nipo sahihi kumbu kumbu zangu zipo vizuri sana kama jiniasi, sijalewa Ha haaaa haaaaaaaaa!”
Enock alichanganya na kiingerza akijaribu kumueleza Masatu kuwa ana matatizo mengi sana pengine anahitaij msaada.
Pombe ililetwa kisha kumtizama Masatu kwa kitambo.
“I know kwamba it is hard for you to believe lakini wacha nikueleze, tafadhali naomba utunze hii siri na unishauri sababu kitendo cha wewe kwendaa and spread to every one utakuwa umeniweka bila nguo”
“sawa ninakuhaidi sitosema kwa mtu yoyote”
“Ni kuhusu Mchumba wangu unaamfahamu nadhani?”
“Ndio Catherine kama sijakosea”
“Huyo huyo,Yule Mwanamke ni mchafu Malaya sana,kumbee anacheza sinema za Ngono Motherfuck*** nikimkamata lazima nimuuwe kwa mikono yangu kisha namimi nifee,nisikilize siongei kwamba nimelewa NOOO…..
“Ujue Mungu ni wa ajabu sana,kanionesha kila kitu, each and everything alafu mimi ni muhuni, nimeishi Marekani Miami pale nimeishi nimekaa na balck Americans,najua michezo yote ya kimafia”
“Mr. Enock sijakuelewa”
“Hujaelewa nini, pumbavu nawewe.Catherine ni Malaya mchafu ameondoka kurudi kucheza Sinema za Ngono”
“Sio kweli”
Hapo ndipo Enock alipozama mifukoni na kutoa simu kubwa kisha kumkabizi Masatu nayeye aweze kujionea, lakini kwa sharti moja awe msiri juu ya hilo.
Massatu alibaki kinywa wazi hakuamini kama Catherine mwanamke anayejishemu kujiingiza katika maswala hayo,
hakuelewa ni kitu gani alikosa kutoka kwa Tajiri Enock.
“Kumbe Dad alikuwa sahihi kabisa,inabidi nikamtoe gerezani ili tuunge nguvu zetu tumsake huyu mwanaharamu, hawezi kuharibu familia yetu!”
Hayo yalimiminika kichwani mwa Enock.
**
Chuki dhidi ya Catherine ilizidi kujilimbikiza mara dufu ndani ya moyo wa Enock, alijuta sana kuwa na Catherine badala ya kumtafuta sasa ili wapatane na wafunge ndoa aliapia endapo akimtia mikononi atamuuwa kwa mikono yake,

japo Anderson Peter alipingana naye vikali juu ya mawazo yake, lakini hakumsikiliza mpaka wakafikia kugombana na kutukanana matusi ya nguoni bila kujali uzito, hakuwa na maelewano tena na Anderson Peter rafiki yake kipenzi,
alijua wote ni wale wale, alitamani siku hiyo hiyo Catherine atokeze na amuuwe ampoteze duniani ikiwezekana baada ya hapo nayeye ajitie kitanzi.
Dunia aliiona chungu mwanamke ambaye aliyejitolea kukinga kifua mbele ili apigwe risasi na Baba yake leo hii kagundua kuwa ni Malaya tena Gwiji na mcheza Ngono maarufu.

Hilo alilithibitisha baada ya kuingia mitandaoni na kukutana na picha nyingine chafu sana za Catherine ambazo amepiga na wanaume akiwa uchi wa mnyama hana hata nguo moja tena akiwa katika tendo la ndoa kaingiliwa,
Mtu kama Enock mwenye heshima zake hakupaswa hata kuwa karibu tena na mwanamke huyo.
Ni picha ambazo hakutaka kuziangalia mara mbili juu ya macho yake maana zilimuumiza sana!
Aliamua kunywa pombe na kulewa kabisa kila kukicha,aliona Dunia ya mapenzi imemkataa, moyo wake ulichanika chanika na kuvuja damu nyingi sana,
Starehe yake ilikua pombe, alikuwa habanduki vilabu vya pombe,haikupita hata siku kadhaa akabatizwa jina na kuitwa Chapombe.

Marafiki waliomuheshimu walimtenga na kumtupilia mbali,hawakuweza kukaa na mtu mlevi.
“Hatuwezi kukaa na walevi,mimi ni mtu na heshima zangu Raphael,Enock ni mlevi na anadaiwa na bank million saba,nina uhakika atafilisika tu”
“Hata kama ni mlevi haina maana ya sisi kumtenga yule ni rafiki yetu isitoshe katusaidia sana, haina maana ya sisi kumuacha ateseke, ana matatizo makubwa sana”
“khaaa!..kwani nani hana matatizo,kila binadamu ana matatizo yeye siyo wa kwanza kupata matatizo na wala hatokuwa wa mwisho. Mimi naondoka, wiki ijayo mwambie ile million saba inatakiwa”
Kila mtu alimzungumzia vibaya Enock, wengi walishatabiri kuwa baada ya miezi mitatu tu atakuwa mzigo kwa watu na atafilisika vibaya mno yaani ataangukia pua!
***
CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Hiyo ilikuwa kinyume kwa msichana mdogo wa makamo kati ya miaka ishirini na tano mpaka ishirini na saba aliyeitwa Dorothea, huyu aliajiriwa na Enock miaka mitatu iliyopita kama hafsa manunuzi, muda mrefu sana alitamani kujua nini tatizo la Bosi wake Enock,
alijua kabisa ni mwanaume anayeteseka na kitu Fulani, alitamani kuuliza lakini hakujua aanzie wapi, Alikua ni mchapakazi sana tangu aingie katika ofisi za NISSAN haikuwahi kupata hata hasara ya shilingi tano kama hapo miaka ya nyuma,
Enock alimpandisha cheo na kuwa Mkurugenzi Msaidizi, aliendelea kuongeza sana juhudi katika kazi yake,

Alilelewa katika misingi imara ya kumjua Mungu na wakati mwingi akimaliza kazi zake basi pembeni yake hushika Biblia na kuanza kusoma habari za Yesu Kristo.
Alijua kabisa Enock anahitaji mshauri, kila hatua aliyopiga Enock basi Dorothea yupo nyuma yake.
Siku hiyo asubuhi na mapema Enock aliingia macho yake yakiwa mekundu huku akiwa anayumba sana amelewa mpaka ofisini kwa Dorothea!
“Nahitaji Laki tisa sasa hivi Dorootheaaa, nina kiu sana ya bia Mama”
Dorothea BADALA ya kumjibu alimtizama bosi wake akimuonea huruma, aliamini kabisa ni pepo mchafu ndiye anamuongoza na wala sio kitu kingine.
“Usinitumbulie Machoo kama mjusi kafiri, nipatie pesa hizo”
“Bosi zipo bank, ndiyo nimepeleka sasa hivi” Alidanganya!
“okay,nipe elfu hamsini yako nitakulipa hapa sina hata dala mfukoni mwangu..changamka basi”
Dorothea alizamisha mkono wake ndani ya mkoba kisha kutoa noti tano za rangi nyekundu na kumkabidhi Enock bosi wake.
**
Aliondoka kwa kupepesuka na kuingia ndani ya gari lake badala ya kuliwasha alianza kulia mwenyewe,huku akipiga piga usukani, alishaelewa kabisa kuna utofauti mkubwa sana katika maisha yake,
alijionea huruma na kupata simanzi ndani ya mtima wake alimchukia sana Catherine, hapo hapo usingizi mzito ulimchukua, aliyemshtua alikuwa ni Dorothea akigonga kioo cha gari!
“Bosi vipi?”
“Safi tu, saa ngapi sasa hivi?”
“saa kumi jioni”
“Hapana sio kweli ina maana nimelala kiasi hiko?”
“Ndio bosi nenda kapumzike tu nyumbani .lakini….”
“Nini Dorothea?”
“kuna jambo nataka kuzungumza nawewe bosi tafadhali naomba uniruhusu”
“Jambo gani hilo?!”
“Ni mambo mengi sana”
“Sawa ingia ndani ya gari”
Dorothea aliingia ndani ya gari!
“Nakusikiliza”
“Ni maongezi marefu sana,naomba tutafute sehemu tuongee”
“sawa twende kwangu”
Enock aliwasha gari mpaka nyumbani kwake.
Kwa mara ya Kwanza Dorothea kufika nyumbani kwa Bosi wake alistaajabu sana kuona jumba kubwa la kifahari mbele yake iliyojengwa kisasa, aliyalinganisha mambo anayofanya bosi wake ya ulevi na hayakuendana kabisa na wadhifa wake.
Walifika nyumbani na kuingia ndani huku Enock akiwa ametangulia mbele na kufungua mlango,

Nyumba nzima ilinuka pombe kali sana, haikuchukua muda kwa Dorothea kutambua kuwa Bosi wake ndiye aliyekuwa anatumia vilevi ivyo vikali sana.
“Unatumia pombe Dorothea?”
“Hapana Bosi hata siku moja sitoweza”
“okay,ngoja nikuletee juice”
Enock alimkabidhi Dorothea Glass ya Juice huku yeye akiwa na yake ya pombe kali,
alibwia glass ya kwanza na kuisha aliongeza nyingine mpaka mzinga wa pombe kali ya VALUER kuisha yote kisha kuongeza nyingine, Dorothea aliogopa sana.
Enock alianza kuongea maneno ya ajabu yasiyoeleweka huku mara kadhaa akitaja jina Catherine akimlaani sana,kisha kulala papo hapo.
Ghafla simu ya Enock iliita usiku huo na Dorothea kuipokea yeye, alikunja sura yake baada ya kugundua ndiye Catherine aliyepiga simu…-

Moyo ulimuuma sana na kuzidi kusonga mbele hakuelewa ni wapi alipo,
Mvua na jua vyote vilimuishia mwilini mwake alipata mateso zaidi,njaa ilimuuma sana.
Alimchukia sana Enock kwa kumpa msichana wake aongee naye na akamtukana akimwambia kuwa yeye ni changudoa tena anayejiuza na hana thamani, japo hakuisikia sauti ya Enock, Mwanamke aliyeongea naye kwenye simu muda mfupi uliopita ndiye aliyemwambia maneno hayo yote,
alijiona ni mwanamke mwenye mkosi mapenzi.

Aliwakumbuka wanaume wote waliomtenda hapo nyuma alimkumbuka vizuri sana Darlington Shebby mwanaume aliyedhani kuwa atakuja kumsahaulisha kila kitu kilichotokea, kumbe yalikua ni yale yale, alijutia sana kurudiana na Enock ki ujumla alijichukia kupita kiasi.
Aliuona mwili wake hauna thamani tena hasa alipokumbuka jinsi alivyoteseka akichezeshwa filamu za Ngono na kusambazwa mitandaoni, hakuelewa kuwa atakuja kuwa mgeni wa nani.
“Lakini kwanini mimi?” Alijiuliza Catherine huku akitembea barabarani, alikuwa kama mwendawazimu, nywele zake chafu na nguo alizovalia zilitosha kabisa kuonesha kuwa alikuwa mwehu, hakuna aliyemjali walimpita mbali.

Hakuwa Catherine Yule wa miaka ya nyuma iliyopita aliyetishia kwa uzuri wa kipekee na tishio Tanzania Nzima na hata Afrika Mashariki na kati,nchi kama Kenya na Uganda wote walimfahamu na kutuma watu mbali mbali wamtafute ili tu wafanye naye matangazo.
Alisita kidogo alivyoona mbele kuna mama Ntilie akiosha Vyombo, ,bila ya kusema lolote alitembea na kwenda kukaa pembeni yake na kuanza kumsaidia kuosha vyombo, akiamini akimaliza hapo atapewa hata ukoko wa wali ili mradi aweze kupata nguvu na kusonga mbele.
CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Ni kweli baada ya kumaliza kuosha vyombo aliletewa Ugali mkubwa na mboga mboga kisha kuanza kula haraka haraka kama aliyekuwa vitani.
Alimshukuru sana Mama huyo kisha kutaka kuondoka lakini alishikwa mkono.
“Your name?”(jina lako).
“Elizabeth”.Alidanganya!
Baada ya hapo aliondoka zake.
**
Enock aliamka akiwa amechoka kichwa kinamuuma sana tena yupo kitandani uchi wa mnyama, hakuelewa ni wakati gani alivua nguo zake na kujilaza kitandani, alijaribu kuvuta kumbukumbu zake nyuma kwa haraka, lakini hakupata picha kamili, jambo alilokumbuka alikuwa na Dorothea wanarudi wote nyumbani kisha kuanza kulewa pombe, kilichotokea hapo hakuweza kuelewa tena mpaka alipozinduka asubuhi.
“Nani kanileta hapa kitandani na kunivua nguo zangu? Tangu nianze kulewa pombe sijawahi kulala kitandani”
Hayo ndiyo yalimiminika kichwani mwa Enock akijaribu kukorofisha kompyuta yake ya ubongoni.
Alitoka Mpaka seblen na kukuta Chai ipo tayari tena mezani imeshaandaliwa,
“NIMEKUANDALIA CHAI BOSI FROM DOROTHEA,”
Ujumbe huo aliusoma Enock uliokua juu ya meza.
Ni Dorothea ndiye aliyeandaa kila kitu hapo mezani kwa Kuwa alikua ana njaa alikula kisha kumtafuta kwenye simu.
“Jana nilikunywa sana eeeh?”
“Ndio Bosi ukaamka ukaniaga kwenda chumbani mwenyewe”
“Mimi?”
“Ndio bosi wewe”
“Haiwezekani, basi maajabu mimi nikadhani wenda wewe ndiye uliyenipeleka mpaka chumbani?”
“Hapana nisingeweza,hata chumba chako sikijui Bosi”
“Lakini Ahsante kwa kila kitu Dorothea japo hukuniambia ulitaka kuzungumza na mimi kuhusu nini”
“Jana nilishindwa muda ulikuwa umekwenda,usiku ulikuwa umeingia bosi nikashindwa, alafu isitoshe haukuwa vizuri, Mungu leo akipenda basi nitatoka mapema nije kukuona Bosi”
“sawa Dorothea,nashukuru sana”
Enock alikua ana hamu sana na kitu gani hasa alitaka kuambiwa na Dorothea,Muda ulisogea mwendo wa kinyonga Mzee.
“Lakiini mimi sindo bosi wake ndiye niliyemuajiri kwanini asije sasa hivi”
Enock aliwaza na kupiga simu kwa Dorothea tena.
“Njoo Nyumbani sasa hivi”
“lakini bosi kuna kazi nyingi leo”
“Achana nazo mpe Blandina”
“sawa Bosi, lakini kwako sipakumbuki vizuri”
Ilikuwa kazi rahisi kumuelekeza Dorothea mpaka nyumbani kwake.

Nusu saa baadaye Dorothea aliwasili ndani ya jumba la Enock kisha mlinzi kumfungulia mlango.
Kama kawaida Enock alimtolea Juice na kumkabidhi nayeye kuchukua pombe kali na kuanza kunywa.
Dorothea hakuelewa ni wapi aanzie kumuuliza bosi wake hakuwa ana uhakika kama anachotaka kumshauri kingewezakana au kuzaa matunda.
“Nakusikiliza Dorothea”
“Bosi”
“Naam nakusikiliza”
“Naelewa una matatizo makubwa sana pia naelewa mambo mengi hayanihusu pengine, lakini nilikuwa naomba unishirikishe ili namimi niweze kukusaidia,Mimi ni Mtumishi wa Mungu kwa Maombi tu nina uhakika utafunguliwa
“Nina amini huyo ni shetani ndiye anayekujaribu na kwa Yesu haya yote yanawezekana”
Enock alimsikiliza kwa umakini badala ya kujibu alibaki kimnya akimtizama huku akiendelea kupiga mafundo ya pombe kali.
“Umechelewa sana”
“Hapana Kwa Yesu hakuna kitu kama hiko, naomba unieleze”
Dorothea alisisitiza.

Enock Alimuamini sana Dorothea kutokana na upole wake hapo ofisini kwake, hapo ndipo alipoanza kumpa historia ya Catherine na mpaka chanzo cha yeye kuwa mlevi kiasi hiko.
“Ni huyu Catherine mchumba wako?”
Dorothea aliuliza kwa mshangao wa waziwazi.
“Ndiyo huyo huyo”
“Pole sana bosi kwa sasa hivi yupo wapi?”
“yupo huko anacheza hizo filamu chafu”
Alijibu Enock na ndivyo alivyoamini.

Dorothea alijaribu kumsihi Enock aweze kumtafuta Catherine na kumwambia kuwa wenda Mungu alimtumia yeye ili ambadili Catherine,
lakini kwa Enock ilikua vigumu sana kukubaliana na swala hilo, alimtoa moyoni kabisa Catherine, bado alitamani amuuwe lakini chuki za kumuuwa hakutaka kuziweka wazi kwa Dorothea alibaki nazo moyoni.
Alizidi kupiga mafundo ya pombe huku akimtizama Dorothea kwenye mpasuo wake ulioonyesha sehemu kidogo ya paja lake jeupe tena laini na kwa mwanaume yoyote Yule lijali ilikua ni lazima aibie ibie,
ki ufupi Dorothea alikua msichana mzuri tena mwenye umbo dogo ukimuona ungedhani wenda ni binti wa miaka kumi na minane.

Enock bila kusita aliweka mkono wake juu ya paja la Dorothea na kumfanya Dorothea ashtuke sana alimuheshimu sana bosi wake, kwa mara ya kwanza alijua wenda ni bahati mbaya lakini mkono wa Enock ulizidi kupanda mpaka juu karibu kabisa na ikulu, hapo ndipo Dorothea alipotoa mkono wa bosi wake.
“Oooh sorry Dorothea”
Alisema Enock kwa sauti ya kusinzia akiwa tayari yupo bwii!
Kwa pombe kali aliyokuwa anakunywa.
Hapo hapo alianza kumtukana tena Catherine akizidi kumlaani.
Usiku ulikuwa mnene sana macho yake yalimlegea aliona vitu viwili viwili.
“Enock mwanangu unakosea sana”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Sauti hiyo ilimfanya ajaribu kukaza macho yake, kwa mbali sana aliona sura ya Mama yake Mzazi Josephine, akiwa amekasirika sana tena yupo kwenye kochi pembeni yake.
“Mama yaaaangu kipenzi….”
Aliita Adrian na macho yake kuzidi kuwa mazito giza nene lilitawala machoni mwake kisha macho yake taratibu kuzima kama radio mbao iliyokua inaisha mabetri!
**
Ni saa tatu ya Asubuhi ndipo alipozinduka kitandani baada ya kuangalia saa kubwa ya ukutani,alishtuka tena baada ya kujiangalia na kujikuta yupo uchi wa mnyama hana nguo hata moja,bado hakuelewa mambo yanayotokea.
“Mhhh”
Aliguna baada ya kuona hereni moja ya Dorothea chini.

“Kosa Moja Magoli mia moja”
“Ha! Haa! Haa! Haa! Haaaa! shoga una misemo”
“wahenga walisema Ndondondo si chululu”
“Wacha we, kwanza umefikia wapi mdogo wangu?”
“ukiona maharage yanarukaruka ujue yanakaribia kuiva”
“Embu niambie hatua uliyofikia,maana ni muda mrefu kwelikweli hujanipa michapo Mdogo wangu”
“Mambo yanakaribia sasa wewe usijali”
Maongezi hayo yalifanyika Gerezani huko Segerea siku maalumu ya kuona wafungwa.
Naomi japo alikuwa miongoni mwa wafungwa lakini muda wote alikuwa ni mwenye furaha kuliko mfungwa yoyote yule,
furaha yake ilichangiwa na vitu viwili kimoja ni kugundua leo hii Dorothea ni mdogo wake pili ni Dorothea kukubali vile vile kuwa naye bega kwa bega ili wamkomoe Enock na Catherine ikiwezekana wawauwe kabisa.

Baba yao Mzee MASUNGA alikuwa ni tishio la kuogopeka miaka ya tisini iliyopita, alikuwa ni miongoni mwa Wauza madawa ya kulevya akiyasambaza nchi za Israel,china na mpaka Amerika ya Kusini na JAMAICA vile vile, alikua ana mtandao mkubwa sana,aliiishi na mke wake Janeth wote walishirikiana wakiishi Kenya Mombasa japo asili yao ilikuwa Tanzania,

hakuna mtu hata mmoja aliyewahi kuwashtukia kuwa familia hiyo inajihusisha na biashara haramu iliyopigwa vita nchi zote karibu Dunia nzima lakini walijikinga na mwavuli wa Dini ya kilokole, tena Mzee Masunga alikuwa ni mwenyekiti wa kanisa kubwa huko Elidoreti akitangaza Injili,hapo alifanikiwa kuwapumbaza watu wote, aliposimama madhabauni mamia na maelfu walifurika viwanjani na hata viwanja kutapika.

Kizuri zaidi alishirikiana na watu wa serikali walikuwa wakimtuma nchi tofauti kama Israeli kutangaza dini lakini akirudi basi ndani ya begi lake alijaza madawa ya kulevya aina ya Coccaine na Herroin.
Habari nzuri zilizomfurahisha ni baada ya mke wake kujifungua Mtoto mwingine wa kike huyu walimpa jina Dorothea, alikuwa ni mwenye afya alipendwa na kila mtu, kila alipoenda baba yake basi Dorothea yupo mkononi, alimpenda kuliko Naomi ambaye kipindi hiko alionesha kuwa kiburi na sio mtiifu.
Baba yake alimchukia sana.
Mafanikio ya Masunga yalizidi mara mia moja, serikali ilianza kumuhisi vibaya lakini Raisi wa Kenya alimtetea.
“Inawezekana vipi bwana,come on huyu ni mtumishi wa Mungu,amepewa utajiri na Mungu kama Ayubu”
Ivyo ndivyo Raisi Okello alivyomtetea Masunga kila alipotaka kuguswa.
Miaka Mitano baadaye! Raisi Okello alipinduliwa na ndiyo hapo Maisha ya Masunga yaliingia dosari na kukosa muhimili,
serikali ilimfuatilia kila kona anayokwenda, ‘Mungu hadhiakiwi’ alikamatwa nchini China mji wa Hongkong akiwa na kete mia tano za madawa makali aina ya Herroin kwenye begi lake la Biblia, hakuna mtu aliyemtetea alipelekwa jela siku hiyo hiyo na kusubiri kunyongwa na ndiyo iyo sheria ya iliyowekwa na Serikali ya China.

Raisi wa Kenya mpya pamoja na wananchi waliichukia familia yao kiujumla na kuwafukuza Jannet na Watoto wake Naomi na Dorothea nchini kwao.
Hapo ndipo walikimbilia Mwanza kuishi huko kwa Tabu, haikuchukua muda Mama yao alifariki dunia kwa ugonjwa wa kipindupindu uliozuka ghafla, huku nyuma yake akiwaacha watoto wake bado wadogo na kuwa watoto wa mitaani wakiwa omba omba barabarani na mitaani hakuna mtu aliyewajali.
Operesheni ya safisha jiji ilianza, hapo ndipo omba omba wote walisombwa na serikali na kupelekwa mikoa tofauti.

Naomi na Dorothea walipoteana na baadaye kukutana ukubwani baada ya Naomi kusomewa kesi hapo kisutu.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Dorothea alikuwepo ili kumsikiliza sababu bosi wake Enock ndiye aliyeshtakiwa, alivyofuatilia aligundua kuwa Naomi ni dada yake, alisikitika sana na ndiyo hapo walipounga nguvu zao ili kutaka kumkomesha Enock.

Mpaka alipofikia Dorothea ilikua ni hatua kubwa sana,Enock alimuamini kupita kiasi au pengine kupita Mfanyakazi yoyote Yule katika kampuni yake,hakuwahi hata kumuhisi kuwa ana undugu na Naomi hata siku moja na kuwa maisha yake yapo matatani,
laiti angelijua hilo asingethubutu hata kumkaribisha nyumbani kwake na kumuamini kiasi hiko.
Hakujua nini kinaendelea ndani ya akili ya Dorothea alichojua yeye ni binti mpole,mchaMungu na Mchapakazi hodari.
Lakini licha ya yote hayo kilichomfanya aanze kuhisi vitu vibaya ni juu ya Hereni ya Dorothea aliyokuta chumbani kwake chini,dalili zilionesha kuwa Dorothea ndiye kila siku huingia naye chumbani na kumvua nguo zake zote lakini hakuelewa kwanini.
“Lazima nifanye uchunguzi usikute nahisi vibaya namsingizia tu binti wa watu,lakini sio vizuri kumuhisi mtu”
Aliingia bafuni na kuoga huku akiwa bado na mawazo juu ya Hereni hiyo aliyoikuta.
Alitoka seblen na kukuta Chai imeandaliwa kama kawaida.
Alichukua simu na kumpigia Dorothea na kumuuliza juu ya Hereni aliyoikuta chumbani kwake, hakutaka kuzunguka zunguka Mbuyu! alimuuliza swali hilo wazi wazi.
“Hereini Hereini?”
Baada ya Dorothea kujibu alibabaika kidogo, hata yeye alishtuka.
“Ndio Hereni yako nimeikuta chumbani kwangu, jana uliingia?”
“Ndio niliingia chumbani kwako”
“Uliingia kufanya nini?”
“Baada ya wewe kuingia chumbani kwako, nilisikia ukiniita na nilivyofika ukaanza kulitaja jina la Mama yako kuwa anakutokea”
“Nani Mimi?”
“Ndio wewe bosi,”
“Mhhh”
Enock Aliguna baada ya kuvuta kumbukumbu nyuma na kutokumbuka kitu chochote kile kuhusiana na yeye kupiga kelele alichokumbuka ni kuona mtu kama Mama yake juu ya kochi.
“Hiyo ndoto iliniogopesha hata mimi”
“Sasa hiyo kali sana, anyway hakuna tabu,samahani kwa kukusumbua endelea na kazi lakini uje jioni pia unipe kampani, ujue nishakuzoea Dorothea”
“Sawa Bosi”
Walikata Simu lakini Enock hakutaka kukubali.

Alielewa kuna mchezo anachezewa na ni lazima awe mwangalifu sana kwani Tangu Dorothea awe anakuja kwake mambo yalibadilika kabisa.
“Huyu anayenifanyia hivi inaelekea anasubiri mpaka nilewe, subiri ipo siku nitajua za mwizi ni arobaini,nitamfahamu tu,hata kama ni jini nitapambana nalo tu”
Enock aliwaza.

Siku hiyo hiyo alienda mpaka kwenye chupa moja ya Wisky na kumwaga pombe hiyo kisha kuweka maji ya kawaida. Hakutoka nyumbani ili kuandaa mitego yake, ilikua ni lazima aujue ukweli kuwa ni nani aliyekuwa anampeleka chumbani kwake na kumvua nguo zake zote.
Masaa yalienda mwendo wa Ajuza!
kisha kufika jioni na Dorothea kuwasili, alifunguliwa mlango na Enock kisha kuingia mpaka seblen na kupewa juice kisha Enock kuchukua chupa ya wisky aliyoweka maji kisha kuimimina kwenye glasi yake.
“Vipi Dorothea za Kazi?”
“Safi tu bosi , leo kuna foleni sana ndiyo maana nimechelewa kufika hapa kwako,hata ivyo leo kulikua kuna wateja wengi”
“Nani aliniulizia?”
“Wakina Daniel,walikuwa wanahitaji ile pesa yao uliyokopa benki”
“Aisee”
“Usiwaze bosi, nilishawalipa kwaio kampuni haina deni lolote lile, na sasa hivi nimeomba TENDER bandarini za kusupply injini za meli”
Maongezi hayo yalimfurahisha sana Enock alikenua meno yake, hakujua kuwa amekaa na jini kabula ambaye amevaa ngozi ya binadamu,

Uso Mzuri wa Dorothea ulikuwa tofauti kabisa na Moyo wake,uliojaa chuki.
Dorothea alitoa Biblia na kuanza kusoma maneno yaliyoandikwa, alimsimulia habari za Manabii wakina Ezekiel,Isaya pamoja na Eliya, wote hao aliwachambua na kumpa mifano mbali mbali kuhusu Wana waisrael walivyokombolewa na Musa kutoka kwa Farao.
Na kuwapeleka nchi ya ahadi Kanani, aliubadilisha mfano huo na kuupeleka kwa Catherine alimwambia kuwa aweze kumtafuta ili waweze kusameana wawe wapenzi kisha wafunge ndoa kwani hayo yalikua ni majaribu ya Shetani aliyekuwa kuzimu.
Alijaribu kumpumbaza Enock afanye ivyo ili iwe rahisi kuwaweka wote wawili kirahisi.
Lakini Enock alitingisha kichwa na kuanza kusinzia na kujifanya amelewa pombe kali.
“Mhhhh Mussa sindo Moses namfahamu na kuna Nabiii Umemsahau Elisha huyu ni nabii safi sanaaaaa… ali ali aliii….”
Hapo hapo Enock aliyafumba macho yake lakini Masikio yake aliyatega vizuri kama antena ya king’amuzi.

Kwa mbali alihisi lips zake zinanyonywa na kuanza kupapaswa na mikono laini kifuani mwake kisha suruali yake kufunguliwa.
Dorothea alianza kuchua Koki ya Enock taratibu ilivyosimama alipiga magoti na kuanza kuiweka mdomoni mwake, yote yaliyotokea Enock alisikia vizuri na kupata jibu la kitendawili chake cha siku nyingi, lakini alitaka kujua mpaka mwisho wake.
Dorothea alivyoona Mashine ya Enock imesimama imara alivua Sketi yake kisha kupanua miguu yake na kujiweka vizuri juu ya mashine, alijua Enock amelala fofofo, hakuelewa kuwa anachorwa na anachokifanya Enock alikitambua na hakuwa amelewa kama anavyodhani.
“Aaaaah sshsss aaah En…ock”
Dorothea alipiga kelele za Puani huku akijaribu kukizungusha kiuno chake taratibu kama feni lililoanza kuwashwa..
CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Watu walizidi kufurika nje ya kibanda cha mgawaha wa Mama Milanto, Kila mtu alitaka kushuhudia kilichokuwa kikiendelea ndani yake, watu walishika vichwa na kubaki vinywa wazi maana kulikuwa na heka heka sio masihala!
wanaume walitupwa nje wakiwa wanaugulia maumivu,
kilichowashangaza watu sio watu kutupwa bali mtu aliyekuwa akiwapiga mapigo hatari na kuwaumiza alikuwa ni mwanamke Mrembo aliyebana nywele zake kwa nyuma, alikuwa si mwingine bali ni Catherine Kidhirwa, alichoshwa na tabia za wanaume kuja na kumfanyia vituko Mama huyo hawalipi baada ya kula chakula kisha kumdhalilisha huku wakimshika baadhi ya sehemu za mwili wake kama makalio na maziwa.
kama mwanamke mwenzake alijisikia vibaya.

Na siku hiyo ndiyo aliyoamua kuwatolea uvivu, alikua akipambana na wanaume kumi na watano, aliona ngumi inakuja na kuinama, hapo alirudi kidogo nyuma na kurusha ngumi iliyomfikia mzee huyo Mwenye mvi kwenye taya zake na kudondoka mbali juu ya vyombo, alivyokuja mwingine alitulizwa na kifuti cha tumbo na chembe, alijipinda pinda na kukaa chini bila kupenda.
Ndani ya Dakika kumi na tano wanaume wote walikuwa chini wengine wamevunjwa vibaya mno hawajiwezi.
“Are okay Madam?”
Catherine alimuuliza Mama Milanto aliyekuwa chini analia kwa kwikwi.
“Who are you?,your going to put me in trouble, those people are very Dangerous(Wewe ni nani, unaenda kuniweka kwenye matatizo, hao watu ni hatari).
Mama Milanto badala ya kushukuru aliogopa alishaelewa wanaume hao ni hatari kiasi gani kutoka katika kikundi cha Black Serial Ninjas,

walikuwa ni vibaka waliotishia mtaa mzima wa Kazak, ki ufupi waliogopwa kuliko hata mnyama mkali yoyote Yule, walikuwa ni watemi na wavuta bangi na waonevu.
Catherine alishaelewa kuwa yupo katika visiwa vya Madagascar na ndege iliyomilikiwa na Carl Martins ilidondoka katika msitu wa Azerbaijan,
huko hakuwa na ndugu wala rafiki zaidi ya kuzoeana na Mama Milanto wakiwa wanaishi katika nyumba yake ya udongo, mbavu za mbwa, wakisaidiana kuuza chakula na kilichopatikana basi hiko ndo hushindia, hakutaka kufungua kinywa chake kusimulia historia yake na asili yake, alidanganya kuwa yeye ni mkimbizi kutoka nchini Libya baada ya vita vya Gadaffi kutokea, tena alikuwa ni mtoto yatima.

Mama Milanto alimuonea huruma na kumchukulia kama Mtoto wake wa kumzaa wakiishi pamoja na kula pamoja.
Ndani ya dakika mbili habari za mwanamke aliyepiga wanaume kumi na watano zilitapakaa kila kona ya mtaa huo, wengi walitamani kumuona, kikundi cha Black Serial Ninjas kilikasirishwa kwa kitendo kilichotokea katika mgahawa huo, haikuwezekana hata mara moja mkuu wao kukubaliana na aliyoyasikia kuwa Mwanamke mmoja kawazidi nguvu wanaume kumi na tano, zilikuwa ni habari za kuchekesha kwake.
“Ha ha ha ha ha ha ha haaa, hata wewe Ismigo, unabondwa na mtoto wa kike?, kwanza ilikuwaje?”
Aliuliza Mkuu wao aliyeitwa Mackdonald Pelegreen, ungebahatika kumuona usingethubutu kusema kuwa ndiye mkuu wao, alikuwa amekondeana mwembamba kama kijiti cha meno pengine hata upepo ukija angepeperushwa mbali lakini alikua ni mwingi wa maneno mdomoni pengine ndiko kilikomsaidia.
“Hatujui mkuu, atakuwa ni jini yule mwanamke tulijikuta wote tupo chini, mara ayayuke mara atokee kule,”
Alidanganya mmoja wao na wenzake kumuunga mkono.
“Anaishi wapi?”
“Pale kwa Mama Milanto, binti mwenyewe anaitwa Elizabeth”
Hilo ndilo jina alilojitambulisha Catherine hata kwa Mama Milanto, kila mtu alimtambua kutokana na upole wake aliokuwa nao lakini alivyopigana ndipo umaarufu ulizidi, waliokuwa wakionewa kila siku walielewa walipata mkombozi wa wanyonge.
“Twendeni tukamsake”
“Poa twenzetuni washkaji,Mimi ndiyo nitakuwa wa kwanza kupambana naye”
“Haina noma”
Kikosi cha pili kilijipanga na kuanza safari ya kuelekea kwenye mgahawa wa Mama Milanto, hawakujua wanacheza na mwanamke hatari kiasi gani, laiti wangelijua wasingewahi hata kufikiria kwenda,

walitembea huku wakiwa wenye hasira, Umbali wa mita kama mia mbili walikuwa wamefika nje ya kibanda cha Mama Milanto kisha mkuu wao kusimama mlangoni akiwa ameitanua mikono yake.
“Karibuni”
Catherine alijua ni wateja na kuwakaribisha kwa lugha ya kiingereza.
“Tunamuhitaji Elizabeth haraka sana, kabla sijapiga mgawaha huu mzima kwa sekunde sifuri!”
Mackdonald alipiga mkwara na wateja kuanza kutetemeka sababu walijua nini kingefuata endapo huyo Elizabeth aliyemuulizia asingejitokeza mbele yake.
“Napenda kurudia Mara ya mwisho, kama jina lako ni Elizabeth tafadhali choma mbele upesi kabla sijatembeza kibano”
“Mack”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Aliita Mama Milanto kabla ya Catherine kujibu lolote.
“Unasemaje?”
“Njoo nje tuongee”
“hakuna cha kuongea,Elizabeth ndiye nani?”
“Unaongelea ni…”
Kabla ya Mama Milanto kujibu kitu alipokea ukofi mzito uliompeleka mpaka Chini kifudifudi, Catherine alilishuhudia hilo,na kumsogelea Mama Milanto kisha kumsimamisha wima.

Ngumi ya nguvu ilirushwa usawa wa tumbo la Mama Milanto lakini kabla haijafika Catherine aliipangua na kumsukuma Mackdonald, kutokana na afya yake mgogoro alijikuta yupo kwenye masufuria ya ukoko ameyadondokea.
Catherine alimtizama na kumsogelea.
“Naomba uinuke uwende,usilete matatizo bure”
“Unasema nini wewe Malaya?”
Neno Malaya ndilo liliamsha mzimu wa Catherine na kupandwa na hasira upya, alimkwida Mackdonald na kumtwanga kichwa puani kikali mno,hakuishia hapo alimburuza mpaka nje kisha kuanza kumshambulia na ngumi zisizokuwa na idadi kamili, hakuna hata mmoja wa wenzake aliyeingilia katikati kusuluisha ugomvi huo hata watu wa Mackdonad waliopanga kumpiga Catherine wote walikaa kando walijifanya hawaoni kitu, walishaelewa ni kiasi gani mwanamke huyo aliyekuwa hatari anachanganya mapigo ya karate,Judo mpaka Kick boxa.
“Eliza! Eliza! Elizaaa!”
Watu walianza kuimba huku wakipiga makofi, walionekana walifurahishwa sana kwa kitendo cha Catherine kutembeza kichapo hiko kwa watu hao waliokuwa waonevu ndani ya mtaa huo na wakorofi pia.
***
Dorothea alizidi kukizungusha kiuno chake taratibu sana kisha baadaye kuzidisha kasi huku akilitaja jina Enock na kutoa mihemo ya Puani, alikuwa mbali kihisia, MARA ya Mwisho kukutana kimwili na mwanamme ilikua ni miaka Mitatu iliyopita kutokana na aibu aliyokuwa nayo, ivyo aliogopa kumvulia mwanamme nguo, kwaiyo aliitumia fursa hiyo kwa juhudi zote, hakuelewa kuwa kila kinachoendelea Enock alikitambua sana,

Enock alikuwa katika maigizo kisha baadaye nayeye kuanza kuhisi raha alijitahidi sana kujikaza ili asitingishike na kufanya Dorothea ajue kuwa yupo macho bado.
Mpaka anamwaga oil chafu hakujitingisha, alichofanya Dorothea ni kwenda bafuni kisha kurudi na kitambaa kilicholowana na kuanza kujipangusa na kumsafisha Enock, zoezi hilo lilivyokamilika alimvuta Enock na kumuweka mgongoni kisha kwenda naye chumbani huko alimvua nguo na kumlaza chali.
Alivyoridhika alimpiga Denda na kuondoka mpaka Seblen na kuandaa chai.

Bado masikio ya Enock yalikuwa yamejitega mpaka alivyosikia mlango umefungwa na kuhakikisha kuwa Dorothea ameshaondoka.
“Sasa kwanini anafanya hivi lakini?,ana ajenda gani namimi, huyu mlokole gani? hapa hamna kitu inabidi niendelee kumchunguza,lakini ngoja nitambana mpaka aniambie ukweli kwanini ananitegea mpaka nilale ndiyo afanye mambo yake”
Aliwaza Enock akizidi kutafakali,ghafla alikunja sura baada ya kukumbuka binadamu aliyeitwa Catherine, alitetemeka kwa hasira kupita kiasi,majasho yalimtoka.
“Catherine lazima nikumalize,umenipotezea muda wangu,..popote ulipo, uwe Marekani, Jamaica,Bangladesh au Msumbiji lazima nikutie mikononi mwangu nikumalize Malaya mchafu”
Usiku mzima alikuwa akiwaza mbinu za Kumkamata Catherine tena kwa gharama yoyote ile swala la Dorothea aliliweka kwanza kando usiku huo, Baada ya kuwaza kama Lisaa lizima alipata jibu ni jinsi gani ya kumpata.
“Labda uwe umekufa! as long as you are alive I will find you Catherine”
Alimaliza Enock kisha kuanza kutafuta usingizi.

***

KULIVYOKUCHA tu alienda seblen na kukuta Chai iliyoandaliwa na Dorothea kabla ya kunywa alimtafuta kwenye simu, lakini siku hiyo alionesha mabadiliko kiasi kwamba hata Dorothea alianza kuhisi alishtukiwa, lakini alitii amri kutoka kwa bosi wake, baada ya Dakika sabini na Mbili walikuwa meza moja seblen kwa Enock wameanza mazungumzo.
“Kwanini ulinivua nguo zangu kisha ukafanya Ngono na mimi na unajifanya umeokoka wewe ni nani?”
Kinyesi cha ghafla kilimbana Dorothea mkojo ulimpenya na kulowanisha nguo yake ya ndani baada ya kusikia swali hilo kutoka Kwa Enock aliyekuwa mbele yake amekunja sura kama aliyekuwa anakunywa togwa.

Kichwa cha Sabrina kilivurugika vibaya mno, hakuweza kufikiria vizuri,kompyuta yake ya kichwani haikufanya kazi sawasawa kama siku zote! Mambo makuu mawili ndiyo yaliyomchanganya akili, Moja kupotelewa kwa Mwanae Catherine na kingine ni kuuguliwa Kwa Christopher.

Usiku Mzima alisumbuliwa na Christopher akilia mfululizo huku mwili wake ukichemka, alijitahidi kumbembeleza lakini hilo halikuwezekana, hapo ndipo aliposubiri kukuche kisha kumpeleka Hospitali ya Watoto kwa Dokta Hameer Kariakoo.
Akiwa anasubiri majibu kwenye Benchi ghafla sura ya Catherine ilimjia, hakujua ni wapi alipo
“Mzee Mwasha yupo Gerezani, sasa ametekwa na nani?”
Hilo ndilo swali kubwa alilojiuliza kila kukicha na kukosa jibu la haraka,
akili yake iligota kufikiria nje ya boxi.
Alishatoa taarifa polisi na kufuatilia lakini hakuambulia kitu chochote kile.
Ilibidi kwanza ashughulikie tatizo la Christopher kwanza alafu mengine baadaye.
Alichukua simu yake na kumtafuta Kway mzazi mwenzake hewani, ilikuwa ni lazima ampe taarifa za mtoto wao Christopher kuumwa.
“Upo hospitali gani?”
“Kariakoo kwa Dokta Hameer”
“Sawa Nakuja”
Kwa kuwa ofisi ya Kway ilikuwa sio mbali na hospitali, Dakika hamsini baadaye alifika kisha kuonana na Sabrina,hakuonesha kinyongo chochote kile, kilichowaunganisha watu hawa wawili ni Christopher tu na wala sio kitu kingine, kitanda hakizai haramu.Alimpenda Christopher.
“Vipi imekuaje, Mbona anachemka hivi?”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Kway alimtupia Swali Sabrina huku akimshika shika shingoni Christopher.
“Hali ilianza Juzi, alikua hataki kula sasa nikaona kawaida, usiku wa jana ndipo alipoanza kulia mfululizo akaanza kuchemka ndipo nikamleta hapa hospitalini”
“Itakuwa Malaria tu pole sana”
“Ahsante”
Japokuwa Sabrina alikuwa keshazaa watoto wawili lakini umbo lake lilibaki vile vile, ukimwangalia usingethubutu kusema ni Mama wa watoto wawili umbile lake lilifanana na binti wa miaka kumi na nane hivi.
Dokta alitoka na kuwaita ofisini kwake ili kupatiwa majibu.Wote walifika na kuketi.
“Huyu ndiye Baba wa mtoto?”
Aliuliza Daktari.
“Ndiyo ndiye Baba yake”
“okay! Mtoto wenu ana homa kali ya mapafu yaani Limonia,msingemuwahisha mngempoteza”
“Atapona?”
Kway aliuliza Kwa hamaki!
“uwezakano wa kupona upo asilimia themanini kama mtafuata dawa nitakazo muandikia hapa”
“Ndio Ndio”
Matibabu ya haraka yalianza mara moja na kupewa dawa za matibabu.

Moyoni mwa Sabrina alionekana kuwa ana kitu anachotaka kukitoa lakini alishindwa na kubaki kumtizama Kway aliyekuwa makini kusikiliza Maelezo ya Daktari, kila kitu kilivyokamilika alilipa matibabu yote.
“Vipi?”
Kway alihoji baada ya kumuona Sabrina kaganda ana mtizama aliyetaka kuuliza kitu.
“Catherine!”
“Nayeye anaumwa?”
“Hapana,bado hajapatikana”
“Unanitania Sabrina sio kweli”
“Kwanini nikudanganye sasa”
Wote walikaa chini!
Sabrina alianza kumueleza kila kitu mpaka hatua aliyofikia na jeshi la polisi kumuhaidi kuwa wangempata lakini hakukuwa na dalili yoyote.
Sabrina aliongea kwa kutia huruma huku machozi yakimlenga, Catherine ndiye alikuwa kila kitu kwake, Maisha bila mwanae aliyaona ni bure tena machungu alimpenda sana binti yake na ndiyo maana alitumia gharama zake zote kumtunza na kumlinda kwenye mikono ya Mzee Mwasha.
“Sasa atakuwa wapi?”
“Hata nashindwa kuelewa naomba unisaidie”
“Nitakusaidiaje unadhani?”
“una watu wengi unafahamiana nao Kway, tafadhali nipo chini ya miguu yako”
“Kwani Yule mchumba wake, huyu nani huyu huyu jina lake limentoka nanii..”
Kway alionekana kufikiria jina la mtu akijaribu kuvuta kumbukumbu.
“Enock”
“Enhee..,anajua?”
“Ndio anajua, lakini nayeye hapatikani,”
“Kwake hupajui?”
“Sijawahi kufika”
“wenda atakuwa huko, sasa inakuwaje usipajue nyumbani kwa Mkweo?”
“Kway naomba nisaidie acha kuniuliza maswali”
“Sabrina sikiliza nikwambie ukweli, mke wangu unajua kabisa yupo katika hali gani,cha kukusaidia mimi nitakuelekeza Kwa huyo Enock, uwende mkaongee mjue mtafanya nini,Mimi msaada wangu utaishia hapo,Kwanza kinachotuunganisha mimi nawewe ni Christopher lakini si vinginevyo,ungeishia kunisikia tu”
“Tafadhali usiseme ivyo,embu tafakari vizuri kumbuka Marehemu Ramsey rafiki yako kipenzi kumbuka Yule ni mtoto wake”
“Sabrina”
“Abee”
“Naomba uniache niende kazini”
Sabrina hakutaka kukubali!

kesho yake asubuhi na mapema aliamka na kunyoosha nyumbani kwa Kway asubuhi sana.
Ni kweli alimkuta akiwa na Julia ndiyo anajiandaa kwenda Kazini, hakusita kusema shida yake mbele yao huku akilia machozi.
“Cherie, musikilize tu, njo ana matatizo mukabisa Musaidie baby”
Kauli Kutoka kwa Julia ndiyo iliyokunjua Moyo wa Kway.
“Sawa njoo jioni ofisini kwangu twende kwanza kwa Enock, wenda atakuwa anajua ni wapi Cate alipo”
Alishauri Kway.
**CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Saa kumi ya jioni Sabrina alipaki gari yake kando ya Ofisi ya Kway kisha kushuka,Wafanyakazi walishajua ujio wake.
“pita ndani anakusubiri”
Alisema Zuhura secretary wa Kway, Ofisini hawakukaa sana waliingia ndani ya gari na safari ya Kwenda Kibamba kuanza, kutokana na foleni iliwachukua masaa mawili kuwasili nyumbani kwa Enock.
walifunguliwa na mlinzi geti kisha kuingiza gari yao ndani.

Enock alishtuka kuona ugeni huo akiwa na Dorothea anamfokea ajibu maswali juu ya yeye kumvua nguo zake na kufanya naye ngono bila ridhaa yake, hapo ndipo alipoghairisha mahojiano kisha kusalimiana na wageni aliowaona.
“Karibuni”
“Ahsante”
“Enock, tunataka tuzungumze nawewe tutoke hapa kidogo”
“Sawa”
Wote waliinuka na kutoka na gari mpaka nje kwenye moja ya Mgahawa wa pombe, kabla ya yote Enock aliagiza pombe kali.
“Nipatie Shot” Aliletewa.
Alikunywa ya kwanza, ya pili kisha ya tatu aliagiza mzinga mkubwa, Kway na Sabrina walionekana kuwa na mshangao lakini walibaki kimnya bila kusema lolote, wao waliagiza Soda.
“Naam Mr.Kway naona mnenivamia ghafla bin Vuu, leteni swaga”
Enock aliongea Kiswahili cha Geto!
“Ni kuhusu Catherine”
“Ndio kafanya nini?”
“Sasa Mr. Enock”
Kway alianza kuongea huku akipooza koo lake na soda ya baridi coca cola.
“Naaam naam”
“nadhani una habari kuhusu Catherine kupotea kwake?”
“Nina habari hiyo ndiyo”
“Nafikiri hata wewe ulifanya juhudi za Kumtafuta”
“Hapana”
Jibu hilo fupi liliwashtua sana. Enock hapo hapo alikunja sura yake na kuwatizama kwa macho ya hasira.
“Kwanini?”
Sabrina alimrushia swali nayeye akitaka jibu la haraka.
Enock alishusha pumzi zake na Kuinamisha kichwa chake chini kisha kuinuka, ilikuwa ni lazima awape makavu yao kuwa Catherine ni malaya, na ivyo hakusita sababu pombe zilikua kichwani tayari na kumpa ujasiri.
“Catherine hanifai ni Malaya mmoja Mbwa,na bora mmekuja mapema ili mjue kuwa ni kiasi gani namchukia na simpendi”
Enock aliongea huku akionesha hasira za waziwazi.
“unasemaje Enock? Usimuite Mwanangu Malaya”
“Sabrina Tulia kwanza”
Kway Aliingilia, sababu alishaelewa upepo umebadilika, kwa mara ya kwanza alidhani wenda Enock anaongea kutokana na Pombe, lakini neno KAMA Malaya,changudoa ndilo lililotawala kinywani mwa Enock hata kudiriki kumtukana na Sabrina.
“Mtoto wa nyoka ni nyoka, inaelekea aliyemzaa alikuwa Malaya vile vile, kama sio wewe basi baba yake..kama mna lingine semeni lakini kama kuhusu Catherine msinipotezee muda wangu, nina mambo mengi ya kufanya, sawa?”
Sabrina alikasirika sana na kuanza kurusha maneno Makali kwa Enock huku akilia kwa Kwikwi lakini alisukumizwa chini, Kway alivyoingilia nayeye alisukumizwa pia, hali ilishakuwa tete Sabrina alishashikwa na Pepo la hasira kali.
“Msitafute vita vya tatu vya dunia.Nadhani hamnijui vizuri mimi, naomba haya mambo yaishe”
Katika hali ya kushangaza Sabrina alisimama na kuchomoa bastola ya Kway iliyokuwa kiunoni mwake, kisha kumuwekea Enock aliyekuwa mbele yake huku akilia machozi ya hasira,
dalili zilionesha kuwa ni lazima angefyatua, kutokana na hasira mbaya alizokuwa nazo.
Ni kweli ndani ya dakika moja ulisikika Mlio mkubwa wa bastola baada ya risasi mbili kuchomoka ndani ya chemba.
“Paaa! paaaaaa”
Enock alikua yupo chini ametulia, Sabrina alibaki akilia machozi ya hasira!.

Jasho jingi lilimtoka akiwa chini, pombe zote alizokunywa sasa ziliyeyuka na kwa mbali alimuona Israeli mtoa roho za watu mita mia mbili tisini na saba kusini kwake.
Licha ya kusikia mlio wa bastola uliyofyatuliwa na Sabrina kwa kusudi la kumlenga yeye lakini hakuhisi maumivu ya aina yoyote ile mwilini mwake. Hakuelewa ni kitu gani kimetokea wenda alidhani ameikwepa risasi na ikapita juu lakini baadaye aligundua kuwa risasi zilipigwa hewani.
“Sabrina tafadhali naomba iyo silaha,hupaswi kufanya ivyo, Hasira hasara”
Alisema Kway kwa hofu, hata yeye ilibidi awe mpole sababu ya hasira mbaya aliyokuwa nayo Sabrina na mpaka kuanza kulia.
Ilichukua dakika kumi na mbili mpaka kuzituliza hasira za Sabrina aliyekuwa ameambiwa maneno machafu na mtoto mdogo Enock aliyekuwa Mkwe wake.
Alimchukia ghafla,alimkabidhi Kway bastola yake kisha kutokomea na kuondoka zake.

***
Bado akili ya Enock haikufanya kazi sawasawa, kila mtu alikuwa adui yake hasa kwa yoyote yule aliyezungumzia habari za Catherine, alimtukana vibaya mno! Hakuwa Enock Yule aliyekinga kifua chake na kupigwa risasi kwa ajili ya Catherine miaka kadhaa nyuma iliyopita.
Alimpenda sana Catherine kuliko kitu chochote kile chini ya Jua la Mungu pamoja na viumbe viishivyo majini,Mapendo aliyompa Mama yake baada ya kufariki dunia aliyahamisha kwa Catherine, lakini sasa ilikuwa kinyume, Picha za Ngono na sinema za utupu ndizo zilimchanganya akili yake kabisa na kumbadilisha kiujumla,alijua Catherine ni mwanamke changudoa tena Malaya hafai kabisa,Picha zake zilitapakaa Duniani kote alijuta kuwa naye kimapenzi, hakuelewa ukweli uliojificha nyuma ya pazia.
“Lazima nikutafute Catherine, popote ulipo kwanza unijibu kwanini ulinipotezea muda wangu”
Aliwaza Enock alivyotoka kujimwagia maji asubuhi hiyo.Alivaa nguo zake haraka haraka kisha kuvaa koti jeusi, alitoka nje na kuwasha gari mpaka Ofisini kwake NISSAN,
CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
wafanyakazi wake walivyomuona walianza kugongana vikumbo huku na huku, walitetemeka sana, walijua kabisa siku hiyo bosi wao hakuamka vizuri kutokana na macho yake kuwa mekundu sana, sura kaikunja mno,walielewa ni lazima siku hiyo mtu afukuzwe kazi kama sio kupigwa makofi hadharani, kila mtu alikuwa bize kwenye meza yake na ukimnya kutawala.
“Shikamoo Bosi, shikamoo bosi”
Waliamkia lakini Enock hakuwajibu.

“Dorothea nifate ofisini”
Maneno matatu tu aliyatoa Enock huku akiwa ameukunja uso wake kwa hasira, maneno hayo yaliutetemesha moyo wa Dorothea, alivyotaka kusimama alirudi tena kwenye kiti kutokana na kukosa nguvu za Miguu, alishaelewa ni kitu gani ameitiwa na Bosi wake!Alifungua mlango wa kioo na kuingia ndani ya ofisi ya bosi wake Enock!.
“Abee.. !Abee! Bosi”
“You are fired”(hauna kazi)
Enock aliongea kwa sauti kubwa kwa hasira huku akipiga meza,hakua hata na mzaha katika neno aliloongea kutokana na sura yake ilivyojionesha.

Dorothea aliangua kilio hapo hapo na kudondoka chini kwa magoti huku akiomba asamehewe, Bosi wake asimfukuze kazi japo hakuelewa ni kosa gani alilitenda la kiofisi!.
“No! I don’t want stupidity, Am done talking with you, No excuse!, Get out bitch, I don’t want to see your face here infront of me,for what you have done For God sake! don’t expect any apology from Enock…..(Hapana! Siihitaji ujinga,nishahitimisha mazungumzo nawewe,nenda nje Malaya sitaki kuiona sura yako mbele yangu, kwa ulichokitenda Nimemaliza,usitegemee msamaha kutoka kwa Enock)
Sauti hiyo ilipaa na kuwafikia wafanya kazi wote waliokuwa kwenye viti vyao, hata wao walielewa ni kiasi gani Enock bosi wao ana hasira, ni kitendo cha Kumfokea Dorothea mfanyakazi aliyemuamini kuliko wengine wote aliowahi kufanya nao kazi hapo Nissan kila mfanyakazi alihaha!
“Bosi naomba unisamehe nitakueleza kila kitu,naomba usifikie huko kwani nategemewa na ukoo wangu wote,ume..fika mbali naelewa nimekukosea sana,ila tafadhali naomba unipe japo dakika mbili nikueleze”
“No! no! I said No”(Hapana,Hapana nimesema hapana)
Enock alijibu huku akisimama na kumuacha Dorothea ofisini kwake akiacha ujumbe nyuma yake kuwa asikute kiwiliwili chake.
“Naomba uchapishe barua, Dorothea sio mfanyakazi wa Nissan tena. Endeleeni na kazi”Aliacha Maagizo Enock kwa secretary.
“Lakini Bosi”
“What?”(Nini)
“Sasa niandike alifanya kosa gani?”
“Nawewe hauna kazi, Michael chapa barua Dorothea na huyu Marry, sitaki kuwaona katika ofisi yangu, baada ya nusu saa nataka wote muwe conference room kuna kikao”
Kila Mtu alishaelewa kuwa Akili ya Enock imevurugika kiasi kwamba wafanyakazi wake wote walikaa mbali naye, hawakutaka hata kuuliza chochote kile.
Alivyorudi ofisini kwake bado alimkuta Dorothea amekaa chini analia macho mekundu na yamemvimba sana!
“Bado upo mahali hapa?”
“Naomba unisa…..me..he”
“Labda kwa kuwa niliongea kiingereza ndiyo maana hukunielewa, hapa hutakiwi kuonekana kabisa hauna kazi”
Dorothea alikua kama Ruba king’ang’anizi hakutaka kubanduka ofisini mwa Enock muda wote alilia akiomba msamaha kwa mambo aliyotenda.
“Unajua sitaki kabisa ukaribu na watoto wa kike,nawachukia sana nyie viumbe,ni waongo sana”
“Naomba unipe nafasi nyingine bosi wangu,kwa hisani yako, kosa sio kosa bali kurudia kosa ndiyo kosa”
Dorothea alijaribu kumshawishi Enock akitumia kila methali,
hapo ndipo alipoingizia historia yake kuwa alikuwa ni mtoto yatima hakuwahi kuwajua wazazi wake hata siku moja, analelewa na ndugu zake kitendo cha Enock kumfukuzisha kazi kingeharibu muhimili wa maisha yake yote, Maneno hayo yalifanikiwa kubadili akili ya Enock aliyekuwa nyuma ya meza anamsikiliza huku akiwa ameshika mikono yake miwili kifuani anamtizama kwa huruma,

Dorothea aliongea huku akitoa machozi na makamasi. Kweli ungemuona Msichana huyu mdogo usingesita kumsaidia au kutoa kitu chochote mfukoni na kumpatia,
Enock hakuelewa kuwa anaigiziwa na maneno aliyosema Dorothea au historia yake asilimia themanini ilikuwa ni uwongo mtupu!
“Niliambiwa kuwa Mama yangu aligongwa na nyoka alivyokuwa akinitafutia dawa kipindi nipo mdogo, alikufa siku hiyo hiyo, Baba yangu naye kwa mshtuko na shinikio la damu nayeye umauti ukamkuta, niliteseka sana nikajuta kwanini nilizaliwa,mimi ndiye nilikua nikijisomesha mwenyewe kwa kufanya biashara ya kuuza mboga mboga mpaka nakuwa”
Historia hiyo ilipenya masikioni mwa Enock na kugota ndani ya moyo wake, ki ufupi aliumia sana,
hata siku moja hakuwahi kufikiria kuwa Dorothea ni msichana mdogo aliyepita kwenye matatizo mengi kiasi hiko pengine kuliko yoyote Yule ulimwenguni,CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
alielewa nini maana ya kufiwa na Mama mzazi,alijikuta anatoa leso yake na kujifuta machozi huruma ilimjaa hasa alipokumbuka alivyomtukana na kutaka kumfukuza kazi.
“Ilikuwa niende kujiua nife kabisa kuliko mateso ambayo ningeteseka huko mitaani”
Dorothea alizidi kupigilia misumari uwongo wake!
Mambo yalikuwa kinyume, badala ya Dorothea kuomba msamaha sasa iligeuka kuwa Enock!
Alimuinua Dorothea akiwa chini kisha kumuweka juu ya kiti akizidi kumuomba msamaha sana!
**
Dorothea alijiona mshindi sana pengine kuliko msanii yoyote Yule wa Bongo movie.
Maigizo aliyoyafanya jana yake kwa Enock na kushinda yalimtia moyo na kuona sasa ushindi ni wake, ilibaki sasa kumuweka Catherine karibu ili awamalize.

Ndani ya moyo wake aliwachukia watu hawa wawili ni kitendo cha Dada yake Naomi kutupwa ndani, ilibidi afanye juu chini ili ajuwe ni wapi catherine alipo lakini hakujua ni njia gani atumie.
“Mimi ndiye Dorothea Masunga nitahakikisha hawa watu wanakufa tu, tena taratibu sana, na hata mtu mmoja hatofikiria kuwa ndiye nilifanya mauaji”
Alivaa nguo zake haraka haraka kwa furaha na kukiendea kioo kikubwa kilichokuwa mbele yake na kuweka kidole gumba kumaanisha kuwa amejikubali amependeza au ametoka chicha! Kwa Kiswahili cha uswazi!
***
Dorothea Alifanya kazi kwa juhudi zote hata wakati mwingine kuzidi muda, Enock alifurahishwa na jambo hilo na kufanya amuongeze mshahara asilimia thelathini, hakuna mfanyakazi ambaye aliyeonesha kujali kampuni isipokuwa Dorothea,
hiyo ilimfanya hata Enock kutoka naye mchana kwenda kula chakula cha mchana akimpa Ofa.
Na ikitokea Enock amekasirika ofisini basi wafanyakzi humuendea Dorothea ili awatetee kutokana na ukaribu aliokuwa nao na Bosi Enock ambaye haikuwa rahisi kuzoeleka na mfanya kazi wake yoyote yule kirahisi rahisi,
alikuwa mgumu kama mfupa! Lakini kwa Dorothea alikua mlaini kama Maini ya Ng’ombe.
***
Maisha yalisonga lakini Enock hakuweza kumsahau Catherine hata mara moja.
“Ngoja kesho niende gerezani nina imani ndiyo siku ya kuwaona wafungwa naenda kumuona Dad kule, anipe ushauri”
Usiku huo Enock aliwaza, Na kulivyokucha tu aliwasha gari na kununua chakula cha Baba yake aliyefungwa Gereza la Keko ambapo hata Naomi alihamishiwa gereza hilo hilo kutokea segerea.

Mzee Mwasha alishtuka sana baada ya kumuona Mwanaye Enock amekuja kumuona tena, mazungumzo aliyoongea naye yalizidi kumfanya atabasamu.
“Nilijua ipo siku ungenitafuta Son!, ngoja nikwambie kitu tutaonana wiki ijayo uraiani…”
Kauli ya kuonana na Baba yake uraiani ilimshtua sana lakini hakutaka kuonesha wazi wazi kuwa alishtuka.
“Kivipi baba?”
“KUNA vijana wangu watafanya kazi yao, kipindi naamishwa gereza kwenda Mwanza”
Mzee Mwasha aliongea kwa kujiamini, dalili zilionesha ni lazima atakuwa huru siku za usoni sababu hakuwa na wasiwasi,
Katika hali ya kushangaza Enock alivyopiga jicho pembeni alimuona Dorothea, kwa mara ya kwanza hakuelewa ni kitu gani alifuata gerezani mpaka alipomuona wapo na Naomi tena wanacheka na kugonganisha mikono yao, hakuelewa kuwa watu hao ni Ndugu tena wanampangia mikakati mibaya sana.
Hakutaka kupoteza wakati alisimama mpaka sehemu walipokuwepo Dorothea na Naomi.
“Habari zenu”
Alisalimia Enock na kumkataka jicho kali Dorothea aliyekua anatetemeka kwa hofu!

KITENDO cha Enock kumuona Dorothea akiwa na Naomi kilimtibua sana akili yake,hakuelewa walijuana vipi isitoshe walikuwa wakicheka na kufurahi wote ki ujumla ilionekana ni watu waliofahamiana kwa kipindi kirefu.
“Karibu bosi”
Alisema Dorothea huku akitabasamu kuashiria kuwa kila kitu kilikuwa sawa lakini bado Enock alikunja sura yake,ki ukweli alimchukia Naomi na kila mtu aliyekuwa karibu yake, dalili zilionesha kuwa hata Dorothea angeenda kuchukiwa na Enock.
Mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea yalimfanya Naomi asiseme lolote aliwatizama tu na kukaa kimnya kabisa!
“inakuaje unaongea na adui yangu ambaye ni muuaji asiyestaili kuishi mna mikakati gani?”
“Sina mikakati naye yoyote ile, nimeamua tu kuja kumsalimia leo bosi,hata mimi ninamchukia kwa kitendo alichofanya ….”
“Hujajibu swali langu”
“Ndio naenda huko bosi. Ni hivi Naomi ni rafiki yangu tulizoeana sana kipindi cha nyuma sasa kuna mambo Fulani tunazungumza ya kawaida bosi”
Dorothea alizidi kumshawishi Enock ili asiweze kuhisi chochote kinachoendelea, hususani mipango yao.
CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Kitendo cha Enock kugundua kuwa Naomi na Dorothea ni ndugu kingesababisha kikwazo kikubwa na hawakutaka hilo litokee, ilibidi Dorothea ampumbaze na kumzuzua akijaribu kuibadili akili ya Enock taratibu sana, ni kweli alifanikisha hilo, uwaminifu wake na ukaribu wake ndiyo uliyonunua akili ya Enock jumla na kuachana na kwenda kuendeleza mazungumzo na Baba yake.
Hakuna walichozungumza zaidi ya kutafuta njia za kumnasa Catherine popote alipo ili mradi yupo hai, Mzee Mwasha alimuhakikishia mwanae kuwa Catherine ni lazima apatikane kama yupo kwenye sayari inayoitwa Dunia.
“Kama yupo Duniani hapa lazima apatikane,Nadhani sina haja ya kuongea mengi sana Enock, nafikiri unanifahamu kuliko mtu yoyote Yule”
Aliongea Mzee Mwasha kwa kujiamini.
“Nina hasira naye sana Dad!, sijui nimfanye nini”
“Usiwe na hasira hizo, mambo mazuri hayataki haraka wewe nenda, nadhani wiki ijayo tutakua wote uraiani huko, tutapanga lakini ibaki kuwa siri yako”
Maneno ya Mzee Mwasha yalimfariji kiasi kwamba alitabasamu na moyo wake kuwa mweupe, alijawa na furaha mno, alivyopita kwenye meza ya Naomi na Dorothea hakuwaona tena!
***
Karandinga lililobeba Wafungwa ishirini na tano lilizidi kusonga mbele usiku wa saa mbili kuelekea mkoani Mwanza,Huku nyuma yake likisindikizwa na Difenda zilizobeba askari kumi wakiwa na mitutu mikononi mwao kwa ajili ya usalama.
Baadaye Waliimaliza Chalinze sasa walikuwa wakiitafuta Morogoro Msamvu!
“Bwana Mapua, leo naenda kuonana na Yule kigoli mtoto wa kisukuma Mwanza nilikuwa nina hamu sana kuchaguliwa na hii safari”
“Inabidi namimi unitafutie kasichana kamoja kazuri sio unakula mwenyewe, nikwambie kitu Fupi?”
“Nambie”
“Mimi na utu uzima wangu wote huu sijawahi kuonja watoto wa kisukuma nasikia wanajua sana mapenzi”
“Kweli nakwambia wewe subiri ufike uwone”
“Wacha we”
“Ndio Mapua usifanye mchezo, nakumbuka huyo mtoto wa kisukuma nilimpa mambo vibaya mno,ki ufupi nilimpania,sema nayeye alinipeleka sana puta, Mtoto ana pumzi kama mcheza mpira”
Maongezi hayo yalifanyika ndani ya Difenda wakiwa katika msafara wa kuwafikisha wafungwa Mkoani Mwanza wakiwa katika mwendokasi!.
Lisaa limoja lizima walikuwa wakiitafuta Msamvu hapo walivuka na baadaye kuanza kupita Mbuga ya mikumi, Dereva wa karandinga alianza kushusha gia kidogo na kupunguza mwendo baada ya kuona kuna gari kubwa mbele yake lililobeba mafuta, tena limetanda katikati ya barabara, alipiga honi ili apite lakini gari hilo lilijongea mwendo wa kobe!
“Huyu jamaa mbona analeta mambo ya kihuni”
Alifoka Dereva wa karandinga lililobeba Wafungwa.
Ivyo ndivyo ilivyokuwa hata nyuma ya difenda kulikuwa kuna gari kubwa pia aina ya Canter likitembea taratibu sana kisha kupita mbele yao, bila kuchelewa watu saba walitoa nyuso zao wakiwa wamevaa ninja na mitutu mikononi, walianza kumwaga risasi wakishambulia difenda za polisi.

Askari walikuwa bado hawakujiandaa, haikuchukua hata dakika saba Diffenda zote mbili zilikuwa Porini zinawaka Moto kisha kuriamuru karandinga lisimame kwani wasingefanya ivyo polisi Wote wangeuwawa.
“Shukeni chini ya gari mlale kwenye majani haraka iwezekanavyo”
Askari walitii amri na kushuka ndani ya karandinga mikono yao hewani wakiwa chini ya ulinzi.
“Masela tumekuja kuwakomboa, kuanzia leo mpo huru kama vipi sepeni”
Kila mfungwa alifunguliwa, Mzee Mwasha tayari alikuwa huru ndio sababu iliyowafanya majambazi hao walifuatilie gari hilo, mipango ilipangwa tangu siku nyingi sasa ilitimia.
“Inukeni”
Polisi mmoja wapo alikuwa teyari amejikojolea kwa uwoga. Kilichosikika hapo ilikuwa ni milio ya risasi kisha majambazi kutokomea na mzee Mwasha kurudi Dar es salaam.
“Kakunguru safi sana. Wewe ni jembe”
Mzee Mwasha aliwapongeza vijana wake.
“sisi ndio wazee wa kazi,usicheze na sisi hii ni kazi ndogo kama ya kuuwa mbu ndani ya neti,kila kitu kitaenda sawa, tukifika mbele hapo tunatia magari kiberiti tunazama ndani ya ndinga ingine Mzee”
Mzee Mwasha alijawa na Furaha sana kurudi tena uiraiani hakuamini kabisa.

**
Taratibu za kumtafuta Catherine zilianza mara moja, picha yake ilipelekwa mpaka polisi wakisingizia kuwa ni jambazi ivyo akamatwe haraka iwezekanavyo,Enock alichukua wazo hilo kutoka kwa baba yake na kuzidi kumwaga pesa nyingi akitaka swala hilo lipelekwe mpaka CNN na Aljazeera, aliamini kupitia njia hizo hata kama Catherine angekuwa nchi gani angekamatwa tu, ndani ya wiki moja picha ya Catherine ilikua katika kila chombo cha habari ikirusha picha zake kuwa ni gaidi kutoka katika kikundi cha Al shaabab, ivyo alitafutwa kwa wudi na uvumba, mbali na hapo Enock aliweka kiasi cha dolla elfu tatu endapo watafanikiwa kumtia mikononi Mwanamke huyo.
polisi waliingia kazini sasa na kuacha shughuli zao. Habari zake ziliruka nchi zote na kutapakaa dunia nzima kwa ujumla.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
**
“Ndio namfahamu,anajiita Elizabeth”
“Wewe ulimuona wapi?”
“Mama Milanto Yule Mama muuza chakula”
“ una uhakika ndiye mwenyewe?”
“Asilimia elfu moja kwanini nidanganye wakati nataka hiyo midola”
“Ole wako tusimkute utajiweka kwenye matatizo”Polisi alisema.
Unoko huo ulitolewa na Ismigo alienda mpaka kituo cha Polisi mjini, baada ya kuona picha ya Catherine kwenye magazeti pamoja na Aljazeera. Taarifa za Catherine zilifika mpaka visiwani Madagascar na ndipo alipokuwa.
Askari watatu waliwasha magari yao wakiwa na Ismigo kwa safari moja tu ya kwenda kumkamata Catherine.
**
Uonevu ulitulia tabia hiyo ilikomeshwa na Catherine kila mtu alimuheshimu,lakini kila mtu alitaka kujua Catherine au Elizabeth ni raia wa wapi,hakuna aliyetegua kitendawili hiko hata siku moja!
Catherine alikuwa ni mwenye furaha muda wote,alishayazoea mazingira na kupata baadhi ya marafiki. Siku hiyo akiwa anapika na Mama Milanto walisikia muungurumo wa Magari walivyochungulia tu dirishani waliwaona askari tena wakiwa wana picha zake mikononi, hakuelewa ni kwanini, mpaka mmoja wa maaskari alivyotoa bastola na kumuweka chini ulinzi.
“Weka mikono yako juu binti upo chini ya ulinzi”
Askari alifoka huku akimsogelea Catherine karibu.

Ndoto za kuchapwa na Mama yake huku wakati mwingine akimkaba zilizidi kumtesa Enock kila kukicha, hakuelewa ni kwanini Mama yake ana mjia ndotoni na kumkaba kohoni tena wakati mwingine akimkimbiza na visu kutaka kumuuwa, hakuweza kupata usingizi wa raha mustarehe kama binadamu au wanyama wengine waishio nchi kavu na majini,kila usiku aliweweseka.
“Mom, usiniue tafadhali Mom nisamehe sana, nini nimefanya Mamaaa?”
Alikurupuka kitandani baada ya kuweweseka kwa lisaa limoja lizima, majasho yalilowanisha mwili wake, hakuwa na utofauti na mtu aliyemwagiwa ndoo ya maji.

Mapigo ya moyo yalimwenda kasi sana kama aliyetoka kukimbia riadha. Kilichomchanganya haswa ni baada ya kusikia maumivu makali sana shingoni, dalili zilionesha ni kweli alikuwa akikabwa na wala haikuwa ndoto.
Alipitisha mkono wake kwenye kitanda na kuwasha taa, alitizama huku na kule lakini hakuona dalili ya kuwa na mtu yoyote Yule kuingia chumbani kwake, kwani hata mlango wa chumba chake ulifungwa na funguo! Hakulala mpaka kunakucha.

Siku hiyo hakuamua kwenda ofisini wala kwenda kwenye vyombo vya habari ili kujua walifikia wapi kuhusu Catherine, alinyoosha mpaka kwa Shekh Mohamedi Omary aliyesifika kwa kutafsiri ndoto, huyu alizipata habari zake siku nyingi sana nyuma,japokuwa hakuwa na imani na watu hao kutokana na elimu aliyokuwa nayo lakini hakuwa na jinsi zaidi ya kwenda Magomeni Mwembe chai ili akajue nini maana ya ndoto hiyo inayomsumbua kila kukicha, Ndoto ilimtisha sana moyoni alihisi kuna kitu Fulani alitakiwa kukijua.
“Samahani ndugu”
Enock alimuuliza mpita njia Baada ya kufungua kioo cha gari alivyohisi amepotea.
“Bila samahani kaka”
“Naomba kuuliza”
“Uliza tu”
“Namuulizia Shekh Mohammedi Omary ni wapi?”
“Mbona ushafika, ni nyumba hiyo hapo yenye nguzo”
“Ahaa aise asante sana,sikuwa nina uhakika napo ndiyo maana”
“Basi ndiyo hapo”
Enock alisogeza gari mbele na kuliweka kando ya nyumba ya Shekh Mohammedi Omary kisha kushuka na kugonga geti jeusi,Ki ukweli alitaka kujua nini maana ya ndoto hiyo iliyomuanza muda mfupi kabla na kumfanya akose usingizi mnono!
“Karibu”
“Aaasalam Aelekuy”
Enock alimsalimia mwanamke aliyetoka amevaa ushungi na kuziba nywele zake baada ya kumfunguliwa mlango,
“Waalekuy Muislam, karibu sana”
“Samahani, nimemkuta Shekh Mohamedi”
“Ndio yupo pita ndani”
Ndani ya nyumba hiyo kulinukia harufu ya wudi na ubani.

Mwanamke aliyevaa ushungi aliingia chumbani kisha baadaye Shekh Mohammedi Omary alitokea, Enock alimtambua sababu humuona kwenye runinga mara kadhaa akiwa anatafsiri ndoto na kutabiri vitu mbali mbali, alisimama na wote kupeana mikono kisha Enock kuanza kusema shida yake kuhusu ndoto inayomsumbua, alitaka kujua maana yake.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Bora umewahi kuja mahali hapa, maana ungeweza kufa hizi siku za karibuni”
Alisema Shekh Mohammedi kisha kusimama na kwenda kuchoma wudi, nyumba nzima ilijaa Moshi, alichukua karata zake kisha kuziweka mezani.
“Nipe mkono wako wa kulia”
Enock aliuweka mezani.Shekh Mohammedi alianza kuongea kwa lugha ya kiarabu na kumtizama Enock kwa macho makali.
“Hii ndoto imeaza lini?”
“ina wiki sasa”
“Mama yako anakupenda sana”
“Una maana gani?”
“kuna kitu anajaribu kukuonesha, kuna moja wapo kati ya haya mawili kuna jambo ambalo unataka kulifanya yeye halipendi au kuna watu wabaya wanataka kukuangamiza, tena inaelekea huyo mtu au hao watu ni wa karibu sana nawewe, kwenye ndoto huwa anasemaje?”
“Huwa ananikaba namuona analia sana anatoa machozi, haongei kitu”
“Basi siku akiongea ujue ndiyo unakufa,na ndiyo mwisho wako utakuwa”
Enock alistaajabu sana, alishindwa kuelewa ni mambo gani anaambiwa, ndani ya akili yake alishindwa kuchanganua pumba au mchele.
“Mzimu wa mama yako bado unakulinda inaelekea kuna mengi sana kakuepusha nayo na bado anakupigania”
“Unaweza kunitajia hao watu?”
“Mimi siyo kazi yangu hiyo, kazi yangu mimi nishaimaliza tayari”
Maneno ya Shekh Mohamedi Omary yalizidi kuukoroga ubongo wa Enock na kumfanya ayatoe macho yake akitafakari.

***
Mama Catherine kila kukicha yeye alilia mfululizo hakuamini kuwa leo hii Mwanaye anatangazwa kwenye vyombo mbali mbali kuwa ni Alshabab na alihusika kwenye mauaji mengi.

Aliumia moyoni na kusononeka lakini licha ya kulia sana alijua hizo ni njama za Enock na wala sio mtu mwingine, alimkombatia mwanaye Christopher huku akiwa mwenye machungu!
***
Hakuna siku ambayo Mzee Mwasha alifurahi kama siku hiyo ya kuwa huru mambo yaliyo mfurahisha ni mawili moja, kuwa uraiani mbili kumpata Catherine na Enock kiurahisi kisha baadaye Sabrina ili afanikishe zoezi lake la kutaka kuwauwa! Kuwauwa watu hao watatu kwake ilikuwa kama ndoto ya miaka mingi ambayo ilikuwa ni lazima itimie, hatimaye yupo huru na Catherine kutangazwa kwenye vyombo vya habari mbali mbali, alichukulia huo ndiyo ushindi tosha.
“Bwana Masawe,wiki ijayo itabidi niondoke zangu kwenda mbali nikajifiche kuna kitu nakisubiri kwanza hapa”
“Hakuna tabu wewe kaa hapa, hakuna hata mmoja atakaye jua upo mahali hapa”
Mzee Mwasha alijificha kwenye nyumba ya mchaga rafiki yake aliyemiliki magorofa mawili kariakoo.
Alifichwa gorofa namba kumi hapo Kariakoo Mtaa wa Gerezani, akisubiri tu Catherine akamatwe ili akamuuwe wakiwa pamoja na Enock hilo ndilo lilikuwa kusudi la kumfanya asubiri na kujificha Kariakoo Mtaa wa Gerezani.
**
Catherine Kidhirwa alikuwa chini ya Ulinzi mkali anasafirishwa kurudishwa nchini Tanzania ili akahukumiwe tayari, alikamatwa na kesi ya mauaji ili mkabiri, hakuelewa mambo yanayotokea!
Saa kumi ya jioni ndipo alipanda ndege na maaskari wawili ili kumlinda kisha kupaa mpaka Doha, hapo walichukua ndege nyingine iliyotuwa moja kwa moja Mwalimu Nyereere Jijijni Dar es salaam nchini Tanzania. Kitendo cha Ndege kukanyaga ardhi ya Tanzania Catherine alilia machozi alikumbuka mengi sana yaliyotokea akiwa Tanzania, mtu wa kwanza kumkumbuka alikuwa Mama yake mzazi kisha picha ya Enock kumjia hapo hapo!

Taratibu walianza kushuka ngazi za ndege mpaka nje, Waandishi wa habari walikuwa wengi wamejaa wakipiga picha za mnato sababu ya muhalifu aliyekuwa akitangazwa kukamatwa huko Visiwa vya Madagascar.
Watu wa Mwasha hawakucheza mbali walipewa amri ya kummaliza Catherine hapo hapo uwanja wa ndege mwalimu Nyerere kabla ya kwenda kituoni, aliamini kitendo cha Catherine kupelekwa rumande ingekuwa vigumu kumtia mikononi mwake.
Jerry na Tyson walipaki gari yao kwenye maegesho kisha kushuka kuweka viwamba kwenye bastola zao ili zisiweze kutoa milio.
Enock naye alifika kimnya kimnya, habari za Catherine kufika Tanzania alizisikia ivyo alitamani kumuona, alipaki Marced Benz yake kando na kushuka akitembea kwa haraka akifuata watu waliokuwa na kamera waandishi wa habari.
Kamera za mnato zilimulika kila wakati, Catherine alikua amefungwa pingu kwa nyuma kichwa chake kakiinamisha,taratibu alikiinua na macho yake kugongana na Enock aliyekuwa nyuma kabisa.
Moyo ulimdunda sana, alivyogeuka pembeni aliona mwanaume aliyevaa koti jeusi na Miwani,
alimkazia macho,alivyoangalia kulia kwake alimuona mwanaume mwingine mfupi pia amevaa miwani kisha wakapeana ishara.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Kengele ililia kichwani mwake kuwa kuna kitu kibaya kinafuata.
Ni kweli mawazo yake yalikuwa yana ukweli, alimshuhudia Mmoja wa wanaume waliovaa nguo nyeusi anatoa gazeti huku ndani yake kukiwa na bastola.
“Pyuu pyuuuu”
Risasi zilitoka kwa mlio wa chini bahati nzuri zilimkosa Catherine baada ya kuinama na kuwapiga askari wa nyuma yake,watu walianza kutawanyika huku na kule.Mambo yaliharibika.
“Shiit, Nimemkosa Catherine, mtafute hawezi kwenda mbali”
Alifoka Mwanaume mfupi mweusi huku akizidi kumtafuta Catherine.

MWISHO


viuhapa

Viuhapa – habari tanzania kwa kiswahili

soma habari mbalimbali za tanzania na ulimwenguni kote kwa kiswahili hapa swahili Viu Hapa. Visit Swahili Viuhapa soma magazeti, habari za mastaa na udaku, umbea, mziki na hadithi za chombezo.

Viuhapa – Latest News and Gossip Leaks Celeb

The latest entertainment news and celeb leak staff worldwide can be found on Viu Hapa. Visit Viuhapa today for latest showbiz and celebrity.

Jobo escort – pata wadada wanaojiuza kutoka tanzania

Pata wadada wanaojiuza kutoka karibu yako hapa tanzania. wanatoa huduma zote. wapigie uongee nao..tembelea jobo escort tanzania. Malaya warembo wamejaa. Visit joboescort today for latest showbiz and celebrity.

vesgeta – Pata website kwa bei nafuu kwa ajili ya Kampuni au biashara yako.

Vesgeta Tech ni watengenezaji wa website / tovuti tanzania. wanatengeneza website kwa bei nafuu zaidi…. Visit vesgeta WATENGENEZA WEBSITE TANZANIA KWA BEI NAFUU.

https://www.swahili.viuhapa.com/bikira-yangu-5-swahili-viuhapa/
Post a Comment

Post a Comment