Leo Jumamosi, Mei 14 kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) limefanyika kongamano la ‘Her Initiative’ linalosaidia kuwaelimisha watoto wa kike kujitambua na kuishi bila kutegemea watu wengine.
![IMG_6398](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_vbgXKDosi9MU5LU8kboEf0bV8bw8oogKHOXnm7ZNc_j2AEXVHQv1YJff4S9HddEHGjk13n3j95zaPC4qW-Bu5ZPysXUa_ClmC-gr9EaLn7VKLXwxlrHPB068Kbp1VXmAFOl73ShwXIUo9GItn23mhE_C3LjUllk1eVLo7HStkZuiJi9nLnxd-JwTACgjjy=s0-d)
Maza Sinare akiongea na watu waliohudhuria kwenye kongamano hilo
![IMG_6479](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_u0ID4mr7K2Wsfg4RC0V2v5dEVPY53xqf5w2HWH_1BottT5-kKKV3NbbW8s3J2wG9sauQzzBlU2vTLmf1RyRABcHfuGANQDqle9Ft_DdghZmHEMVggJKefq9-2ylcVhAwXaPRChIOhHgWnezJBSbfxPiMqDcGoAWu7vWoOHivrStxaKUmp8VurHWntqgu1S=s0-d)
Jennifer Shigoli akitoa neno kwenye kongamano la ‘Her Initiative’
![IMG_6529](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_sleQmfJxQasnY2cUD7uARnxXoG2W48BBtsoztBEGA2xQXNY8ctN136YoAch5vSnFj5kLaStniXZZ94a3vR-He8_o1E_sVd8LtESjggTGk-t5oniEff7pLZVFYKFYQnXspdZd4LqutCOPjtn-ZRXOnJuOsxiYbFHCI5PFWk4dhLqIVxmAvc2P6PYa0LQfFh=s0-d)
Aika wa kwanza kulia akiwatambulisha wasanii wao wapya kwenye lebo ya The Industry
![IMG_6536](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_tNsUEy_nEP0JHi3hmGEZ8XT4jgBbu4o3SwQzl8NTyxcKEURK_6RdCe_fvRVDRg-6igPCF6sC0BLqeAwZ7ybp4hqSS94xvPcfzeeBxx46Uj7kjG6u-pn7R3_Uz7nsLDx0qNjRruHCSL-I5JrhNOYFZL2LgoniDSoW7YEo3R9x2GXRTDz4iDXr0-lHK8EgPo=s0-d)
Mbunge wa Jimbo la Segerea, Bona Kaluwa aiongea na watu waliohudhuria kwenye kongamano hilo
Jiunge na BONGOHOTZ.COM sasa
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,
Twitter na Instagram
ili kupata habari zote za town! Usiache ku download application play store kupata habari ndani ya sekunde kila inapotufikia..Karibu
LIKE PAGE YA BONGOHOTZ KWENYE FACEBOOK
Kongamano hilo lililoandaliwa na taasisi ya HER INITIATIVE lilihudhuriwa na wanafunzi wa vyuo mbalimbali vya Dar es Salaam na wasichana wajasiriamali pamoja na wageni kadhaa wakiwemo, Ruge Mutahaba, Le Mutuz, Jennifer Shigoli, Maznat Sinare, Aika na Mhe Bona Kaluwa.
Akiongea na watu waliohudhuria kwenye kongamano hilo, Maza Sinare ambaye ni mmiliki wa kampuni ya Maznat Bridal alisema aliwahi kuvaa nguo moja kwa miaka saba kwa kuwa kipindi hicho hakuwa na hela lakini alijituma kwa kufanya kazi kwa bidii kwenye ajira yake aliyoanzanayo ya kuuza mitumba bila ya kutegemea mtu wala mwanaume yeyote mpaka kufikia leo anamiliki kampuni kubwa na kupata safari nyingi za kwenda nje na kununua nguo azitakazo.
Maza Sinare akiongea na watu waliohudhuria kwenye kongamano hilo
“Siyo muda wote mnakuwa mnaachia miguu mkiendekeza sana ile inachosha na unazeeka mapema. Fanya kazi kwa bidii hata kama biashara yako ni ndogo ila msisahau kujiwekea akiba kwa kufungua mifuko ya kuweka akiba fedha zako hata kama ni kidogo unauza mahindi hutaweza amini siku ukienda unapotaka kuzichukua,” aliongezea.
Jennifer Shigoli akitoa neno kwenye kongamano la ‘Her Initiative’
Naye Jennifer Shigoli ambaye ni Mkurugenzi wa kampuni ya Malkia Investments alisema, “nilipomaliza chuo nilifanikiwa kupata kazi kwenye ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali. Nilifanya kazi pale kwa miezi mitatu tu nikawaambia nyumbani naacha kazi nataka kujiajiri, walinishangaa.”
“Nilijiunga na Chuo cha Veta nikajifunza kutengeneza sabuni, baada ya muda nikafungua kampuni yangu ya manufacturing,” aliongeza.
Aika wa kwanza kulia akiwatambulisha wasanii wao wapya kwenye lebo ya The Industry
Hata hivyo, msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Aika alipata nafasi ya kuongea na kusema, “Usiige maisha ya Aika kwenye video, mimi nimelelewa maisha mazuri. Unavyoniona jukwaani tofauti na ninavyoishi maana wasichana wengi wanaishi kutokana na maisha ya kuiga.”
Mbunge wa Jimbo la Segerea, Bona Kaluwa aiongea na watu waliohudhuria kwenye kongamano hilo
Aidha mgeni rasmi wa kongamano hilo Mhe Bona Kaluwa aliwataka watoto wa kike wasikate tamaa kwani kila kazi ina changamoto zake, hata yeye amepitia changamoto nyingi mpaka kufikia ngazi ya kuwa mbunge wa kuchaguliwa na wananchi tena ukiangalia uchaguzi wa mwaka jana ulivyokuwa mgumu na alikuwa anashindana na wanaume na akafanikiwa kuwashinda.
Tazama picha zaidi.
Wageni wakisikiliza maneno yanayotolewa na watoa mada kwenye kongamano hilO
Lydia Charles ambaye ni Mwenyekiti wa Her Initiative akitoa neno kwa wageni
Jiunge na BONGOHOTZ.COM sasa
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook
LIKE PAGE YA BONGOHOTZ KWENYE FACEBOOK