Na:bongohotz
|
Mhe. Stephen Wasira akichukuliwa vipmo vya suti na mbunifu wa mavazi, Sheria Ngowi. |
BAADA ya kuandamwa sana katika mitandao ya kijamii kuhusu kutofunga vizuri vifungo vya suti yake,
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mhe. Stephen Wasira ameamua
kumuona mbunifu wa mavazi wa kimataifa, Sheria Ngowi ili aanze
kumtengenezea suti zake.
|
Waziri Wasira akijaribu kurekebisha suti yake iliyokosewa kufungwa vifungo na kuzua mjadala mitandaoni. |
Mhe. Wasira ameamua kukutana na mbunifu huyo aliyeanza mara moja
kumchukua vipimo vyake ili amtengenezee mavazi yake ambayo atakuwa
akiyatumia katika shughuli zake mbalimbali za kiserikali.
Picha za Waziri Wasira zilienea mitandaoni alipopiga picha ya pamoja
akiwa na Viongozi wa Kanisa la Kisabato kwenye Uwanja wa Taifa, Dar huku
koti la suti yake likiwa limekosewa kufungwa vifungo.
|
Baadhi ya picha kutoka mitandaoni baada ya Mhe. Wasira kukosea kuvaa suti yake. |
Baadhi ya watumiaji wa mitandao ya kijamii walirusha picha mbalimbali
zikimuonesha Mhe. Wasira huku mmoja wa watangazaji akisema kuwa iwapo
akikubaliwa, atajitolea kuwa wabunifu wa suti zake za mitoko ili jambo
hilo lisijitokeze tena.
|
Mhe. Wasiara akiwa katika
picha ya pamoja na Viongozi wa Kanisa la Kisabato kwenye Uwanja wa
Taifa, Dar huku koti la suti yake likiwa limekosewa kufungwa vifungo. |
Baadhi ya watumiaji wa mitandao ya kijamii walirusha picha mbalimbali
zikimuonesha Mhe. Wasira huku mmoja wa watangazaji akisema kuwa iwapo
akikubaliwa, atajitolea kuwa wabunifu wa suti zake za mitoko ili jambo
hilo lisijitokeze tena.
Post a Comment