psycological advice

MAISHA BAADA YA KUWA MAMA:JE NI MUDA GANI SAHIHI KUKUTANA KIMAPENZI NA MWENZI WAKO BAADA YA KUJIFUNGUA??

Habari yako Kaka wa bongohotz,mm naitwa Pendo,nna umri wa miaka 25 nimeolewa na nimebahatika kupata mtoto mmoja wa kiume wamepishana mwezi mmoja na siku moja na Zion huyu ni wa mwezi march tar 15.Napenda kuchukua fursa hii kukushukuru kwa kutupatia mwanga wa maisha,inshort kwamba wewe ni kioo changu napenda kuwa kama wewe msikivu, mwerevu, mpenda watu ,muelimishaji rika nk.




 

Nia na dhumuni la kuandika email hii naomba msaada wako kaka wa bongohotz kuna watu wanasema kwamba ukisha jifungua hupaswi kukutana na mumeo kimwili mpaka mtoto atembee la sivyo utambemenda mtoto, wengine wanasema kwamba unafanya ila ukimaliza pale ukaoge kabla hujamshika wala kumnyonyesha mtoto la sivyo utamuharibu atakuwa atembei atakuwa kutwa anafanya kazi ya kuharisha tuu na afya yake itakuwa hafifu kiujumla.Mimi mume wangu ameondoka mda tangu mimba yangu haija pea yupo UK anasoma na amepata kazi huko na mwishoni mwaka huu anarudi kuja kuiona familia yake pamoja na mm mkewe ss hapa ndo najiuliza akija nimwambie tusubiri mpaka mtoto atembee?na je atanielewa kweli? au kuna njia nyingine safe ya kukutana na mumeo bila mtoto kuharibika kiafya?nisaidie dada yangu yamenifika shingoni hata kwa watu niulizie me huwa situmii njia yeyote ya uzazi wa mpango zaidi ya calendar tu ndio safe kwangu.Pls naomba msaada wa mawazo.


*Tunaomba msaada wa kimawazo kulingana na unachofahamu.*


                                                   ENDELEA HAPA

Post a Comment

Post a Comment