Ada

Mirathi ya Mengi yazua balaa, Watoto Wadaiwa Kutokulipiwa Ada za Shule - Swahili Viuhapa

featured image





viuhapa

 

HABARI HIZI ZINAPATIKANA  KWENYE APP YA UDAKU SPECIAL, BONYEZA HAPA KUIDOWNLOAD KWENYE SIMU YAKO BURE

Dar ea Salaam. Wasimamizi wa mirathi ya aliyekuwa mfanyabiashara maarufu nchini, Reginald Mengi, wameburuzwa mahakamani wakidaiwa kukataa kuwahudumia watoto wadogo wa mfanyabiashara huyo aliowazaa na mkewe Jacquiline Ntuyabaliwe.

Kesi hiyo imefunguliwa na Jacquiline katika Mahakama ya Watoto iliyoko katika eneo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam.

Wasimamizi wa mirathi hiyo wanaokabiliwa na kesi ni mtoto wa marehemu, Abdiel Mengi na mdogo wa marehemu, Benjamini Mengi.

Habari ambazo Mwananchi limezipata na kuthibitishwa na wakili wa mjane huyo, Audax Kahendaguza, kwa ridhaa ya mteja wake, katika shauri hilo la madai namba 50 la mwaka 2022, Jacquiline anadai matunzo ya watoto hao ikiwamo ada ya shule.

Anadai kuwa watoto hao walikuwa wakigharimiwa ada na baba yao pamoja huduma nyingine zote walizostahili, kutokana na kipato alichokuwa anakipata kwenye shughuli zake za kibiashara, ambazo kwa sasa ziko mikononi mwa wasimamizi hao wa mirathi.

Anadai kuwa hata baada ya kifo cha baba yao, awali wasimamizi hao walikuwa wakiwalipia ada na huduma nyingine japo mara mojamoja; kwamba sasa wameacha kabisa kuwalipia ada ya shule pamoja na huduma nyingine licha ya kuwaomba mara kadhaa.

Mawakili wa wadaiwa walieleza kuwa hawajaandaa majibu ya madai hayo kwa kuwa wateja wao wako mikoani huku Mahakama ikiwataka kuwasilisha majibu yao Februari 17, mwaka huu siku ambayo pia kesi hiyo itatajwa tena.

Kesi hii imekuja wakati bado kuna mgogoro wa mirathi ya marehemu Mengi kati ya pande hizo mbili, kwani bado kuna shauri la mirathi linasubiri uamuzi.

 Join AJIRA YAKO Group for Daily Job Updates CLICK HERE








viuhapa

Viuhapa – habari tanzania kwa kiswahili

soma habari mbalimbali za tanzania na ulimwenguni kote kwa kiswahili hapa swahili Viu Hapa. Visit Swahili Viuhapa soma magazeti, habari za mastaa na udaku, umbea, mziki na hadithi za chombezo.

Viuhapa – Latest News and Gossip Leaks Celeb

The latest entertainment news and celeb leak staff worldwide can be found on Viu Hapa. Visit Viuhapa today for latest showbiz and celebrity.

Jobo escort – pata wadada wanaojiuza kutoka tanzania

Pata wadada wanaojiuza kutoka karibu yako hapa tanzania. wanatoa huduma zote. wapigie uongee nao..tembelea jobo escort tanzania. Malaya warembo wamejaa. Visit joboescort today for latest showbiz and celebrity.

vesgeta – Pata website kwa bei nafuu kwa ajili ya Kampuni au biashara yako.

Vesgeta Tech ni watengenezaji wa website / tovuti tanzania. wanatengeneza website kwa bei nafuu zaidi…. Visit vesgeta WATENGENEZA WEBSITE TANZANIA KWA BEI NAFUU.

https://www.swahili.viuhapa.com/mirathi-ya-mengi-yazua-balaa-watoto-wadaiwa-kutokulipiwa-ada-za-shule-swahili-viuhapa/
Post a Comment

Post a Comment