celeb

Wema Sepetu baada ya Heaven Sent, ‘kuna project za kutikisa mji’

Baada ya muigizaji Wema Sepetu kuachia filamu yake ya Heaven Sent, 2017 na kushinda tuzo, amefunguka kipi kinafuata kutoka kwake.
 



Mrembo huyo amesema kwa kushirikiana na timu yake kuna movie wanaandaa ambayo itakuja kubadili tasnia nzima, pia kuna event nyingine kubwa atafanya June mwaka huu.

“Heaven Sent imekuja imeshinda tuzo, so it good thing, tutegemee vitu vikubwa kama nilivyosema hapo awali kuna kitu kitatokea June kwa hiyo tukae mkao wa kula kitu kizuri kinakuja nadhani kitabadilisha tasnia ya filamu as a all, kuna project za kutikisa mji,” Wema ameiambia Bongo5.

Usiku wa April 01, 2018 filamu ya Heaven Sent ilimfanya Wema Sepetu kuwa mshindi wa tuzo mbili za Sinema Zetu International Film Festival Awards (SZIFF).
Post a Comment

Post a Comment