celeb

Dayna Nyange: Nina Tuzo Kibao Kutoka Nchini Nigeria



MSANII Dayna Nyanga aka  Binti Nyange aliyehiti na ngoma ya Komela aliyomshirikisha Billnass amesema yeye ni mmoja wa wasanii maarufu nchini wanaomiliki tuzo kibao.


Akiongea na East African Radio katika kipindi cha Planet Bongo, Dayna  na ngoma yake ya Komela alisema amewahi kushinda tuzo mbili kutoka nchini Nigeria na nyingine kutoka Morogoro, yaani  jumla tuzo tatu.

“Ukiangalia nyumbani nimekuwa nikiwania tuzo nyingi lakini sijawahi kuchukua.  Tuzo ambazo nimewahi kuchukua ni za huko Nigeria ambako nilichukua mbili na nyingine nilichukuwa mkoani Morogoro katika shindano la Uluguru Award.

Post a Comment

Post a Comment