IN SUMMARY
Akisoma tamko hilo jana, Janeth Mawinza alisema wanawake wana madeni mengi ambayo wameshindwa kulipa kwa sababu ya kukosa elimu ya biashara.
Dar es Salaam. Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), umekosoa bajeti ya mwaka 2016/17 kutokana na kuzifanya Sh50 milioni zilizoahidiwa na Rais John Magufuli kila kijiji, kuwa za mkopo badala ya kutolewa kama ruzuku.
Akisoma tamko hilo jana, Janeth Mawinza alisema wanawake wana madeni mengi ambayo wameshindwa kulipa kwa sababu ya kukosa elimu ya biashara.
“Tuwape unafuu sasa kwa kuwapa ruzuku, vinginevyo tutawasababishia msongo wa mawazo kwa kudaiwa na taasisi mbalimbali za fedha,” alisema
Post a Comment